< Mambo ya Walawi 11 >

1 Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
And the Lord spoke unto Moses and to Aaron, saying unto them,
2 “Sungumzeni na watu wa Israeli muwaambie, 'Hivi ndivyo viumbe vyenye uhai ambavyo mwaweza kula miongoni mwa wanyama walioko juu ya nchi.
Speak unto the children of Israel, saying, These are the beasts which ye may eat among all the beasts that are on the earth.
3 Mnaweza kula mnyama yeyote aliye na kwato zenye kugawanyika na ambaye pia hucheua.
Whatsoever divideth the hoof, and is cloven-footed, and cheweth the cud, among the beasts, that may ye eat.
4 Hata hivyo, kuna baadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika, nanyi msiwale hao, wanyama kama ngamia, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika. Kwa hiyo ngamia ni najisi kwenu.
But these shall ye not eat, of those that chew the cud, or of those that divide the hoof: the camel; because he cheweth the cud, but divideth not the hoof; he is unclean unto you.
5 Pimbi pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyo pia ni najisi kwenu.
And the cony; because he cheweth the cud, but divideth not the hoof; he is unclean unto you.
6 Na sungura pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyu naye ni najisi kwenu.
And the hare; because he cheweth the cud, but divideth not the hoof; he is unclean unto you.
7 Na nguruwe pia: ingawaje yeye anazo kwato zilizogawanyika lakini hacheui, kwa hiyo yeye ni najisi kwenu.
And the swine; because he divideth the hoof, and is cloven-footed, but he cheweth not the cud; he is unclean unto you.
8 Msile aina yoyote ya nyama yao, wala msiiguse mizoga yao. Hao ni najisi kwenu.
Of their flesh shall ye not eat, and their carcass shall ye not touch; they are unclean unto you.
9 Nao wanyama waishio majini mnaoweza kuwala ni wale wote walio na mapezi na magamba, iwe waliomo baharini au mitoni.
These may ye eat, of all that are in the waters: all that have fins and scales in the waters, in the seas, and in the rivers, them may ye eat.
10 Lakini viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni, pamoja na wale waendao majini na viumbe hai waliomo majini —watakuwa chukizo kwenu.
But all that have not fins and scales in the seas, and in the rivers, of whatever moveth in the waters, and of any living thing which is in the waters, shall be an abomination unto you:
11 Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
And an abomination shall they remain unto you; of their flesh shall ye not eat, and their carcasses ye shall have in abomination.
12 Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
Whatsoever hath not fins and scales in the waters, shall be an abomination unto you.
13 Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
And these shall ye have in abomination among the fowls; they shall not be eaten, they are an abomination: The eagle, and the ossifrage, and the osprey,
14 mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
And the vulture, and the kite after his kind;
15 kila aina ya kunguru,
Every raven after his kind:
16 kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
And the ostrich, and the night-hawk, and the cuckoo, and the hawk after his kind;
17 Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
And the little owl, and the cormorant, and the great owl,
18 bundi mweupe na mwari,
And the swan, and the pelican, and the gier-eagle,
19 korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
And the stork, the heron after his kind, and the lapwing, and the bat.
20 Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
All flying insects that walk upon four feet, shall be an abomination unto you.
21 Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
Yet these may ye eat, among all the flying insects that walk on four feet, which have spring-legs above their feet, to leap therewith upon the earth.
22 Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
These of them may ye eat: The locust after its kind, and the sol'am after its kind, and the chargol after its kind, and the chagab after its kind.
23 Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
But all flying insects, which have four feet, shall be an abomination unto you;
24 Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.
And through these shall ye be rendered unclean: whosoever toucheth the carcass of them shall be unclean until the evening;
25 Na yeyote atakayeokota mojawapo wa mizoga yao ni lazima atazifua ngua zake naye atakuwa najisi hata jioni.
And whosoever beareth aught of their carcass shall wash his clothes, and be unclean until the evening.
26 Mnyama yeyote ambaye anazo kwato ziliachana ambazo hazikugawanyika kabisa au hacheui huyo ni najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa najisi.
Every species of beast, which divideth the hoof and is not cloven-footed nor cheweth the cud, is unclean unto you: every one that toucheth the same shall be unclean.
27 Mnyama yeyote anayetembea kwa vitanga vyake miongoni mwa wanyama waendao kwa miguu yote minne ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mzoga kama huo atakuwa najisi hata jioni.
And all that walk upon their paws, among all manner of beasts that walk on four feet, are unclean unto you; whosoever toucheth their carcass shall be unclean until the evening.
28 Na yeyote aokotaye mzoga kama huo ni zazima atazifua nguo zake na kuwa najisi hata jioni. Wanyama hawa watakuwa najisi kwenu.
And he that beareth their carcass shall wash his clothes, and be unclean until the evening: unclean shall they be unto you.
29 Kuhusiana na wanyama wataambaao juu ya ardhi, hawa ndiyo walio najisi kwenu: kicheche, panya, aina zote za mijusi mikubwa, guruguru,
And these shall be unclean unto you among the creeping things that creep upon the earth: The weasel, and the mouse, and the tortoise after its kind,
30 kenge, mijusi ya ukutani, goromoe, na kinyonga.
And the hedgehog, and the chameleon, and the lizard, and the snail, and the mole.
31 Wanyama hawa wote ambao hutambaa, hawa ndiyo watakuwa najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa njisi hata jioni.
These shall be unclean to you among all that creep: whosoever doth touch them, when they are dead, shall be unclean until the evening.
32 Na iwapo mmoja wao anakufa na kuanguka juu ya chombo, chombo hicho kitakuwa najisi, ama kiwe kimetengenezwa kwa mbao, nguo, ngozi, au gunia. Kiwe chombo cha namna gani na kiwe kwa matumizi gani, ni lazima kitalowekwa katika maji nacho kitakuwa najisi hata jio. Kisha kitakuwa safi.
And every thing upon which any part of them, when they are dead, doth fall, shall be unclean; whether it be any vessel of wood, or raiment, or skin, or sack, every vessel wherewith any work can be done, must be put into water, and it shall be unclean until the evening, when it shall be clean.
33 Kwa hiyo kila chungu ambacho mnyama najisi atakiangukia juu yake au ndani yake, chochote kilichomo kwenye chungu hicho kitakuwa najisi, na ni lazima mtakivunja chungu hicho.
And every earthen vessel whereinto any part of them falleth, whatsoever is in it shall be unclean; and itself shall ye break.
34 Vyakula vyote ambavyo ni safi na kilichuhusiwa kuliwa, lakini kikaingiwa na maji kutoka kwenye chungu najisi kilichoanguka, nacho kitakuwa najisi.
All kinds of food which may be eaten, on which water cometh, shall be unclean: and all drink that may be drunk, shall be rendered unclean in every vessel.
35 Na kitu chochote kinachoweza kunywewa kutoka kwenye chungu kama hicho kitakuwa najisi. Kila kitu kitakachoangukiwa juu yake na kipande cha mzoga wa mnyama najisi nacho kitakuwa najisi, ama liwe ni jiko au vyungu vya kupikia. Ni najisi na ni lazima kiwe najisi kwenu.
And every thing whereupon any part of their carcass falleth, shall be unclean; an oven, or ranges for pots, shall be broken down, they are unclean; and unclean shall they be unto you.
36 Chemchemi au kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika patabaki kuwa safi iwapo kiumbe najisi kama hicho kitaangukia humo. Lakini ikiwa yeyote anaugusa mzoga wa mnyama aliye najisi uliomo ndani ya maji, yeye atakuwa najisi.
Nevertheless, a fountain, or pit, receptacles for water, shall be clean; but he that toucheth their carcass shall be unclean.
37 Iwapo sehehemu yoyote ya mzoga wa mnyama aliyenajisi inaangukia juu ya mbegu zozote zilizo kwa ajili ya kupanda. Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi.
And if any part of their carcass fall upon any sowing-seed which hath been sown, it shall be clean.
38 Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu, na kama sehemu ya mzoga unaangukia juu yake, nazo zitakuwa najisi kwenu.
But if any water be put upon the seed, and any part of their carcass fall thereon, it shall be unclean unto you.
39 Iwapo mnyama yeyote awezaye kuliwa anakufa, naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni.
And if any cattle die, which is allowed to you as food: he that toucheth its carcass shall be unclean until the evening.
40 Na yeyote alaye chochote cha mzoga huo atalazimika kufua nguo zake naye atakuwa anjisi hata jioni. Na yeyote aokotaye mzoga kama huo atafua nguo zake na kuwa najisi hata jioni.
And he that eateth of its carcass shall wash his clothes, and be unclean until the evening; he also that beareth its carcass shall wash his clothes, and be unclean until the evening.
41 Kila mnyama atambaaye juu ya ardhi atakuwa chukizo; hatakuwa wa kuliwa.
And every creeping thing that creepeth upon the earth is an abomination, it shall not be eaten.
42 Chochote kitambaacho kwa kujivuta juu ya tumbo lake, na chochote kitembeacho kwa miguu yake yote minne, au chochote kilicho na miguu mingi—wanyama wote ambao hutambaa juu ya nchi, hawa msiwale, kwa sababu watakuwa machukizo.
Whatsoever goeth upon the belly, and whatsoever goeth upon four feet, down to whatsoever hath many feet among all creeping things that creep upon the earth, shall ye not eat; for they are an abomination.
43 Msijinajisi wenyewe kwa kiumbe chochote nnajisi kitaambacho; msijinasi wenyewe kwavyo, ili kwamba msije mkachafuliwa navyo.
Ye shall not make yourselves abominable with any creeping thing that creepeth; and ye shall not make yourselves unclean with them, that ye should be defiled thereby.
44 Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu. Nanyi lazima muwe watakatifu, kwa hiyo na iweni watakatifu, kwa sababu Mimi ni mtakatifu. Haiwapasi kujichafua kwa aina yoyote ya kiendacho juu ya nchi.
For I am the Lord your God; ye shall therefore sanctify yourselves, and ye shall be holy; for I am holy: neither shall ye make yourselves unclean with any manner of creeping thing that creepeth upon the earth.
45 Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh, aliyewaleta ninyi kutoka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo lazima muwe watakatifu, kwa kuwa Mimi ni mtakatifu.
For I am the Lord that have brought you up out of the land of Egypt, to be your God; ye shall therefore be holy, for I am holy.
46 Hii ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho majini, na ya kila kiumbe kitambaacho juu ya nchi,
This is the law of the beasts, and of the fowl, and of every living creature that moveth in the waters, and of every creature that creepeth upon the earth:
47 kwa jili ya kilie kinachopaswa kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi, na kati ya vitu vilivyokufa na vilivyo hai ambavyo vyaweza kuliwa na vitu vyenye uihai visivyoweza kuliwa.”
To distinguish between the unclean and the clean, and between the beast that may be eaten and the beast that may not be eaten.

< Mambo ya Walawi 11 >