< Mambo ya Walawi 10 >

1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
و ناداب و ابیهو پسران هارون، هر یکی مجمره خود را گرفته، آتش بر آنهانهادند. و بخور بر آن گذارده، آتش غریبی که ایشان را نفرموده بود، به حضور خداوند نزدیک آوردند.۱
2 Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
و آتش از حضور خداوند به در شده، ایشان را بلعید، و به حضور خداوند مردند.۲
3 Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
پس موسی به هارون گفت: «این است آنچه خداوندفرموده، و گفته است که از آنانی که به من نزدیک آیند تقدیس کرده خواهم شد، و در نظر تمامی قوم جلال خواهم یافت.» پس هارون خاموش شد.۳
4 Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
و موسی میشائیل و الصافان، پسران عزیئیل عموی هارون را خوانده، به ایشان گفت: «نزدیک آمده، برادران خود را از پیش قدس بیرون لشکرگاه ببرید.»۴
5 Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
پس نزدیک آمده، ایشان را در‌پیراهنهای ایشان بیرون لشکرگاه بردند، چنانکه موسی گفته بود.۵
6 Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
و موسی هارون وپسرانش العازار و ایتامار را گفت: «مویهای سرخود را باز مکنید و گریبان خود را چاک مزنیدمبادا بمیرید. و غضب بر تمامی جماعت بشود. اما برادران شما یعنی تمام خاندان اسرائیل بجهت آتشی که خداوند افروخته است ماتم خواهند کرد.۶
7 Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
و از در خیمه اجتماع بیرون مروید مبادا بمیرید، زیرا روغن مسح خداوند برشماست.» پس به حسب آنچه موسی گفت، کردند.۷
8 Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
و خداوند هارون را خطاب کرده، گفت:۸
9 “Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
«توو پسرانت با تو چون به خیمه اجتماع داخل شوید شراب و مسکری منوشید مبادا بمیرید. این است فریضه ابدی در نسلهای شما.۹
10 ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
و تا درمیان مقدس و غیرمقدس و نجس و طاهر تمیزدهید،۱۰
11 ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
و تا به بنی‌اسرائیل همه فرایضی را که خداوند به‌دست موسی برای ایشان گفته است، تعلیم دهید.»۱۱
12 Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
و موسی به هارون و پسرانش العازار و ایتامار که باقی بودند گفت: «هدیه آردی که از هدایای آتشین خداوند مانده است بگیرید، و آن را بی‌خمیرمایه نزد مذبح بخورید زیراقدس اقداس است.۱۲
13 lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
و آن را در مکان مقدس بخورید زیرا که از هدایای آتشین خداوند این حصه تو و حصه پسران توست چنانکه مامورشده‌ام.۱۳
14 Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
و سینه جنبانیدنی و ران افراشتنی را تو و پسرانت و دخترانت با تو در جای پاک بخورید، زیرا اینها از ذبایح سلامتی بنی‌اسرائیل برای حصه تو و حصه پسرانت داده شده است.۱۴
15 Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
ران افراشتنی و سینه جنبانیدنی را با هدایای آتشین پیه بیاورند، تا هدیه جنبانیدنی به حضور خداوندجنبانیده شود، و از آن تو و از آن پسرانت خواهدبود، به فریضه ابدی چنانکه خداوند امر فرموده است.»۱۵
16 Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
و موسی بز قربانی گناه را طلبید و اینک سوخته شده بود، پس بر العازار و ایتامار پسران هارون که باقی بودند خشم نموده، گفت:۱۶
17 “Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
«چراقربانی گناه را در مکان مقدس نخوردید؟ زیرا که آن قدس اقداس است، و به شما داده شده بود تاگناه جماعت را برداشته، برای ایشان به حضورخداوند کفاره کنید.۱۷
18 Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
اینک خون آن به اندرون قدس آورده نشد، البته می‌بایست آن را در قدس خورده باشید، چنانکه امر کرده بودم.»۱۸
19 Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
هارون به موسی گفت: «اینک امروز قربانی گناه خود وقربانی سوختنی خود را به حضور خداوندگذرانیدند، و چنین چیزها بر من واقع شده است، پس اگر امروز قربانی گناه را می‌خوردم آیا منظورنظر خداوند می‌شد؟»۱۹
20 Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.
چون موسی این راشنید، در نظرش پسند آمد.۲۰

< Mambo ya Walawi 10 >