< Mambo ya Walawi 10 >
1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
And whanne Nadab and Abyu, the sones of Aaron, hadden take censeris, thei puttiden fier and encense aboue, and offriden bifor the Lord alien fier, which thing was not comaundid to hem.
2 Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
And fier yede out fro the Lord, and deuouride hem, and thei weren deed bifor the Lord.
3 Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
And Moises seide to Aaron, This thing it is which the Lord spak, Y schal be halewid in hem that neiyen to me, and Y schal be glorified in the siyt of al the puple; which thing Aaron herde, and was stille.
4 Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
Sotheli whanne Moises hadde clepid Mysael and Elisaphan, the sones of Oziel, brother of Aaron's fadir, he seide to hem, Go ye, and take awey youre britheren fro the siyt of seyntuarie, and bere ye out of the castels.
5 Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
And anoon thei yeden, and token hem, as thei laien clothid with lynnun cootis, and castiden out, as it was comaundid to hem.
6 Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
And Moises spak to Aaron, and to Eliasar and Ithamar, the sones of Aaron, Nyle ye make nakid youre heedis, and nyle ye reende clothis, lest perauenture ye dien, and indignacioun rise on al the cumpany; youre britheren and all the hows of Israel byweile the brennyng which the Lord reiside.
7 Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
But ye schulen not go out of the yatis of the tabernacle, ellis ye schulen perische; for the oile of hooli anoyntyng is on you. Whiche diden alle thingis bi the comaundement of Moises.
8 Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
Also the Lord seide to Aaron,
9 “Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
Thou and thi sones schulen not drynke wyn, and al thing that may make drunkun, whanne ye schulen entre in to the tabernacle of witnessing, lest ye dien; for it is euerlastynge comaundement in to youre generaciouns,
10 ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
that ye haue kunnyng to make doom bytwixe hooli thing and vnhooli, bitwixe pollutid thing and cleene;
11 ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
and that ye teche the sones of Israel alle my lawful thingis, whiche the Lord spak to hem bi the hond of Moyses.
12 Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
And Moises spak to Aaron, and to Eliazar and Ythamar, hise sones, that weren residue, Take ye the sacrifice that lefte of the offryng of the Lord, and ete ye it with out sour dow, bisidis the auter, for it is hooli `of the noumbre of hooli thingis.
13 lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
Sotheli ye schulen ete in the hooli place that that is youun to thee and to thi sones, of the offryngis of the Lord, as it is comaundid to me Also thou,
14 Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
and thi sones, and thi douytris with thee, schulen ete in the clenneste place the brest which is offrid, and the schuldur which is departid; for tho ben kept to thee and to thi fre sones, of the heelful sacrifices of the sones of Israel;
15 Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
for thei reiseden bifor the Lord the schuldur and brest, and the ynnere fatnessis that ben brent in the auter; and perteynen tho to thee, and to thi sones, bi euerlastynge lawe, as the Lord comaundide.
16 Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
Among these thingis whanne Moises souyte the `buk of geet that was offrid for synne, he foond it brent, and he was wrooth ayens Eliazar and Ythamar, `the sones of Aaron that weren left.
17 “Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
And he seide, Whi eten not ye the sacrifice for synne in the hooli place, which sacrifice is hooli `of the noumbre of hooli thingis, and is youun to you, that ye bere the wickydnesse of the multitude, and preye for it in the siyt of the Lord;
18 Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
moost sithen of the blood therof is not borun yn with ynne hooli thingis, and ye ouyten ete it in the seyntuarie, as it is comaundid to me?
19 Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
And Aaron answeride, Sacrifice for synne, and brent sacrifice is offrid to dai bifor the Lord; sotheli this that thou seest, bifelde to me; how myyte Y ete it, ether plese God in cerymonyes with soreuful soule?
20 Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.
And whanne Moises hadde herd this, he resseyuede satisfaccioun.