< Mambo ya Walawi 10 >
1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
[Two of] Aaron’s sons, Nadab and Abihu, took the pans in which they burned incense. They put some burning coals in them and put incense on top of the coals, but this fire was not acceptable [to Yahweh] because it was not the kind that he had commanded them to burn.
2 Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
So suddenly a fire from Yahweh appeared and burned them up [DOU] in the presence of Yahweh.
3 Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
Then Moses/I said to Aaron, “That is what Yahweh predicted. He said, ‘Those priests who come near to me, I will show them that they must (respect me/treat me as being holy); in the presence of all the people I am the one who must be honored.’” But Aaron said nothing.
4 Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
Then Moses/I summoned Mishael and Elzaphan, who were the sons of Aaron’s uncle Uzziel, and said to them, “Take [the corpses of] your cousins outside the camp, away from the front of the Sacred Tent.”
5 Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
So they carried the corpses, which still had their special gowns on, outside the camp, [and buried them].
6 Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
Then Moses/I said to Aaron and his [other two] sons Eleazar and Ithamar, “[You are sad because Nadab and Abihu died, but you must act like you always do]. Do not allow the hair on your [heads] to remain uncombed, and do not tear your clothes. But your relatives and all your fellow Israelis are allowed to mourn for those whom Yahweh destroyed by fire.
7 Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
But you must not leave the entrance of the Sacred Tent [to join those who are mourning], because if you do that, you also will die, and Yahweh will punish [MTY] all the people of Israel. Do not forget that Yahweh has set you apart [MTY] to work for him here, [and he does not want you to become defiled by touching a corpse].” So they did what Moses/I told them to do.
8 Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
Then Yahweh said to Aaron,
9 “Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
“You and your [two] sons [who are still alive] must not drink wine or other fermented drinks before you enter the Sacred Tent; if you do that, you will die. That is a command that you and your descendants must obey forever.
10 ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
You must do that in order to learn what things are holy and what things are (not holy/common), and [from the things that are not holy] you must learn what things are acceptable to me and what things are not.
11 ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
And you must teach to the Israeli people all the laws that I gave to the Israeli people by telling them to Moses.”
12 Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
Moses/I said to Aaron and his two sons who were still alive, Eleazar and Ithamar, “Take the offering made from grain that is left after a portion of it has been offered to Yahweh to be burned, and eat it alongside the altar. [It should not be eaten elsewhere], because it is very holy.
13 lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
Eat it in a holy place; it is the share for you and your sons from the offerings that were burned; I have commanded that it be your share.
14 Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
But you and your sons and daughters are permitted to eat the breast and the thigh that were lifted up in front of Yahweh. Eat them in any place that is (holy/acceptable to him). They have been given to you and your descendants as your share of the offerings to enable the Israelis to maintain fellowship [with Yahweh].
15 Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
The thigh and the breast that were lifted up in front of Yahweh must be brought with the portions of fat to be burned, to be lifted up in his presence. They will be the regular share for you and your descendants, as Yahweh has commanded.”
16 Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
When Moses/I inquired about the goat that had been sacrificed to enable the people to be forgiven by Yahweh for the sins they had committed, he/I found out that it had been completely burned. So he/I was angry with Eleazar and Ithamar and asked them,
17 “Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
“Why did you not eat near the Sacred Tent the meat of the offering for sin? It was very holy, and it was given to you to enable the Israeli people to no longer be guilty for their sins and to be forgiven for their sins.
18 Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
Since its blood was not taken into the holy place inside the Sacred Tent, you should have eaten the [meat of] the goat near the Sacred Tent, as I commanded.”
19 Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
Aaron replied to Moses/me, “Today the people brought to Yahweh their offering to be forgiven for the sins they had committed, and the offering to be completely burned, [and surely that pleased Yahweh], but [think about the terrible thing] that happened to my other two sons! Would [RHQ] Yahweh have been pleased if I had eaten some of the offering to cause the people to become acceptable to God?”
20 Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.
When Moses/I heard that, he/I was satisfied.