< Mambo ya Walawi 10 >

1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
And the sons of Aaron, Nadab and Abihu, each take his censer, and put fire in them, and put incense on it, and bring strange fire near before YHWH, which He has not commanded them;
2 Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
and fire goes out from before YHWH and consumes them, and they die before YHWH.
3 Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
And Moses says to Aaron, “It [is] that which YHWH has spoken, saying, By those drawing near to Me I am sanctified, and in the face of all the people I am honored”; and Aaron is silent.
4 Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
And Moses calls to Mishael and to Elzaphan, sons of Uzziel, uncle of Aaron, and says to them, “Come near, carry your brothers from the front of the holy place to the outside of the camp”;
5 Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
and they come near, and carry them in their coats to the outside of the camp, as Moses has spoken.
6 Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
And Moses says to Aaron and his sons, to Eleazar and to Ithamar, “You do not uncover your heads, and you do not tear your garments, that you do not die, and He is angry on all the congregation; as for your brothers, the whole house of Israel, they lament the burning which YHWH has kindled;
7 Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
and you do not go out from the opening of the Tent of Meeting, lest you die, for the anointing oil of YHWH [is] on you”; and they do according to the word of Moses.
8 Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
And YHWH speaks to Aaron, saying,
9 “Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
“You do not drink wine and strong drink, you and your sons with you, in your going into the Tent of Meeting, and you do not die—a continuous statute throughout your generations,
10 ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
so as to make a separation between the holy and the common, and between the unclean and the pure;
11 ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
and to teach the sons of Israel all the statutes which YHWH has spoken to them by the hand of Moses.”
12 Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
And Moses speaks to Aaron and his sons, to Eleazar and to Ithamar, who are left, “Take the present that is left from the fire-offerings of YHWH, and eat it unleavened near the altar, for it [is] most holy,
13 lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
and you have eaten it in the holy place, for it [is] your portion, and the portion of your sons, from the fire-offerings of YHWH; for so I have been commanded.
14 Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
And you eat the breast of the wave-offering and the leg of the raised-offering in a clean place, you, and your sons, and your daughters with you; they have been given for your portion and the portion of your sons, out of the sacrifices of peace-offerings of the sons of Israel;
15 Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
the leg of the raised-offering, and breast of the wave-offering, besides fire-offerings of the fat, they bring in to wave [as] a wave-offering before YHWH, and it has been to you, and to your sons with you, by a continuous statute, as YHWH has commanded.”
16 Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
And Moses has diligently sought the goat of the sin-offering, and behold, it is burned, and he is angry against Eleazar and against Ithamar, sons of Aaron, who are left, saying,
17 “Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
“Why have you not eaten the sin-offering in the holy place, for it [is] most holy—and He has given it to you to take away the iniquity of the congregation, to make atonement for them before YHWH?
18 Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
Behold, its blood has not been brought into the holy place within; eating you eat it in the holy place, as I have commanded.”
19 Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
And Aaron speaks to Moses, “Behold, today they have brought their sin-offering and their burnt-offering near before YHWH; and [things] like these meet me, yet I have eaten a sin-offering today; is it good in the eyes of YHWH?”
20 Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.
And Moses listens, and it is good in his eyes.

< Mambo ya Walawi 10 >