< Mambo ya Walawi 10 >

1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
Aaron's sons, Nadab and Abihu, set light to their incense burners using ordinary fire and put in incense, and in this way offered forbidden fire in the Lord's presence, something he had not authorized.
2 Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
Fire came out from the Lord's presence and burned them up. They died in the Lord's presence.
3 Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
Moses explained to Aaron, “This is what the Lord was talking about when he said: ‘I will show my holiness to those who approach me; I will reveal my glory so everyone can see.” But Aaron didn't reply.
4 Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
Moses called Mishael and Elzaphan, sons of Aaron's uncle Uzziel, and told them, “Come and carry away the bodies of your cousins and take them outside the camp, away from the front of the sanctuary.”
5 Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
They came and picked them up by their clothes, and took them outside the camp, as Moses had ordered.
6 Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
Then Moses told Aaron and his sons Eleazar and Ithamar, “Don't leave your hair uncombed, and don't tear your clothes in mourning, otherwise you will die, and the Lord will be angry with everyone. But your relatives and all the other Israelites may mourn for those the Lord killed by fire.
7 Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
Don't go outside the entrance to the Tent of Meeting, or you will die, because you have been anointed by the Lord.” They did what Moses said.
8 Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
The Lord told Aaron,
9 “Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
“You and your descendants must not to drink wine or any other alcohol when you go in to the Tent of Meeting, otherwise you will die. This regulation is for all time and for all future generations.
10 ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
You must realize the difference between the holy and the ordinary, between clean and unclean,
11 ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
so you can teach the Israelites all the regulations that the Lord has given to them through Moses.”
12 Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
Moses told Aaron and his two sons who were left, Eleazar and Ithamar, “Take the grain offering that is left over from the food offerings given to the Lord and eat it without yeast beside the altar, because it is most holy.
13 lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
You must eat it in a holy place, because it is the share for you and your descendants from the food offerings given to the Lord. This is what I have been ordered.
14 Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
You and your male and female descendants can eat the breast of the wave offering and the thigh contribution anywhere that is ceremonially clean, because you and your descendants have been given these as your share from the peace offerings of the Israelites.
15 Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
The thigh contribution and the breast of the wave offering, as well as the fat portions of the food offerings made, they are to bring and wave as a wave offering before the Lord. They belong to you and your children forever as the Lord has ordered.”
16 Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
Moses checked what had happened to the goat of the sin offering, and found out that it had been burned. He got angry with Eleazar and Ithamar, the sons Aaron had left, and asked them,
17 “Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
“Why didn't you take the sin offering and eat it in the holy place, because it is most holy and it was given to you to take away the people's guilt by making them right before the Lord.
18 Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
As its blood was not taken into the holy place, you should have eaten it in the sanctuary area, as I ordered.”
19 Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
So Aaron explained to Moses, “Look, it was today that they presented their sin offering and their burnt offering before the Lord. After all that's just happened to me, would the Lord have been pleased if I'd eaten the sin offering today?”
20 Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.
When Moses heard what Aaron had to say, he accepted the explanation.

< Mambo ya Walawi 10 >