< Mambo ya Walawi 1 >

1 Mungu alimwita Musa na alisema naye kutoka kweye hema la kukutania, akasema,
Yahvé llamó a Moisés y le habló desde la Tienda del Encuentro, diciendo:
2 “Sema na wana wa Israeli na uwaambie, 'Mwanaume yeyote miongoni mwenu akileta sadaka kwa Bwana, aleta kama matoleo katika wanyama wako, iwapo mifugo au katika kundi.”
“Habla a los hijos de Israel y diles: ‘Cuando alguno de vosotros ofrezca una ofrenda a Yahvé, ofreceréis vuestra ofrenda del ganado, de la manada y del rebaño.
3 Kama matoleo yake ni ya sadaka ya kutekezwa kutoka katika kundi, atatoa dume asiyekuwa na kasoro. Atamtoa katika mlango wa kuingilia katika hema ya kukutania, ili iwe imekubaliwa mbele za Bwana.
“‘Si su ofrenda es un holocausto del rebaño, ofrecerá un macho sin defecto. Lo ofrecerá a la puerta de la Tienda del Encuentro, para que sea aceptado ante el Señor.
4 Ataweka mikono yake kichwani pa sadaka ya kuteketezwa, na ndipo itakuwa imekubaliwa badala yake kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe.
Pondrá su mano sobre la cabeza del holocausto, y le será aceptado para hacer expiación por él.
5 Ndipo atapaswa kuchinja ng'ombe mbele ya Bwana. Watoto wa Aroni, makuhani wataleta damu na kuinyunyizia katika madhabahu iliyo katika mlango wa kuingilia katika hema la kukutania.
Matará el toro delante de Yahvé. Los hijos de Aarón, los sacerdotes, presentarán la sangre y la rociarán alrededor del altar que está a la puerta de la Tienda de reunión.
6 Ndipo ataichuna sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande.
Desollará el holocausto y lo cortará en pedazos.
7 Kisha wana wa Haruni kuhani wataweka moto katika madhabahu na kuweka kuni ili kuchochea moto.
Los hijos del sacerdote Aarón pondrán fuego en el altar y pondrán la leña en orden sobre el fuego;
8 Wana wa Haruni, makuhani wataweka vipande, kichwa na mafuta, watazipanga juu ya kuni zilizoko juu ya moto ulio madhabahuni.
y los hijos de Aarón, los sacerdotes, pondrán los trozos, la cabeza y la grasa en orden sobre la leña que está sobre el fuego que está en el altar;
9 Lakini matumbo yake na miguu lazima ataiosha kwa maji. Kisha kuhani atateketeza kila kitu kilicho juu ya madhabahu kama sadaka ya kuteketeza. Italeta harufu nzuri sana kwangu; itakuwa sadaka iliyotolewa kwa moto kwa ajili yangu.
pero lavará sus entrañas y sus patas con agua. El sacerdote lo quemará todo sobre el altar, como holocausto, ofrenda encendida, de aroma agradable para Yahvé.
10 Kama sadaka kwa ajili ya sadaka ya kuteketeza kutoka kundi, kondoo au mbuzi, lazima atoe dume asiye na kasoro.
“‘Si su ofrenda es del rebaño, de las ovejas o de las cabras, para un holocausto, ofrecerá un macho sin defecto.
11 Lazima atamchinja juu ya madhabahu iliyo katika upande wa kaskazini mbele ya Bwana. Wana wa Haruni makuhani, watanyunyiza damu kila upande wa madhabahu.
Lo matará en el lado norte del altar, delante de Yahvé. Los hijos de Aarón, los sacerdotes, rociarán su sangre alrededor del altar.
12 Kisha ataikata katika vipande, pamoja na kichwa na mafuta yake, kuhani atavipanga juu ya kuni zilizo katika moto ulio madhabahuni,
Lo cortará en pedazos, con su cabeza y su grasa. El sacerdote los pondrá en orden sobre la leña que está sobre el fuego que está sobre el altar,
13 lakini matumbo yake na miguu yake lazima ioshwe kwa maji. Kisha kuhani atatoa yote na kuiteketeza juu ya madhabahu. Ni sadaka ya kuteketezwa, italeta harufu nzuri kwa ajili ya Bwana; itakuwa sadaka ya Bwana iliyotolewa kwa moto.
pero las entrañas y las patas las lavará con agua. El sacerdote ofrecerá el conjunto y lo quemará sobre el altar. Es un holocausto, una ofrenda hecha por el fuego, de aroma agradable para Yahvé.
14 Kama sadaka yake kwa Bwana itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa ni ndege, ndipo ataleta kama sadaka yake aidha ni huwa au kinda la njiwa.
“‘Si su ofrenda a Yahvé es un holocausto de aves, ofrecerá su ofrenda de tórtolas o de pichones.
15 Kuhani ataileta madhabahuni, atamnyonga kichwa chake, na kuiteketeza juu ya madhabahu. Kisha damu yake itachuruzishwa juu ya pande za madhabahu.
El sacerdote la traerá al altar, le arrancará la cabeza y la quemará sobre el altar, y su sangre se derramará a un lado del altar;
16 Kisha atakiondoa kibofu chake pamoja na uchafu wake, na kukiweka upande wa mashariki mwa madhabahu, katika sehemu ya majivu.
y le quitará el buche y las plumas, y la echará junto al altar, en la parte oriental, en el lugar de las cenizas.
17 Kisha atapasua mabawa yake, lakini hatagawanya katika vipande viwili. Kisha Kuhani atamtekeza katika madhabahu, juu ya kuni amabazo ziko juu ya moto. Itakuwa sadaka ya kuteketezwa, na italeta harufu nzuri sana kwa Bwana; itakuwa sadaka ya Bwana iliyotolewa kwa moto.
La arrancará por las alas, pero no la separará. El sacerdote lo quemará sobre el altar, sobre la leña que está sobre el fuego. Es un holocausto, una ofrenda hecha por el fuego, de aroma agradable para Yahvé.

< Mambo ya Walawi 1 >