< Mambo ya Walawi 1 >

1 Mungu alimwita Musa na alisema naye kutoka kweye hema la kukutania, akasema,
I wezwał Pan Mojżesza, i rzekł do niego z namiotu zgromadzenia, mówiąc:
2 “Sema na wana wa Israeli na uwaambie, 'Mwanaume yeyote miongoni mwenu akileta sadaka kwa Bwana, aleta kama matoleo katika wanyama wako, iwapo mifugo au katika kundi.”
Mów do synów Izraelskich, a rzecz im: Gdyby kto z was ofiarował ofiarę Panu, z bydła, z wołów, i z drobnego bydła, ofiarować będziecie ofiarę waszę.
3 Kama matoleo yake ni ya sadaka ya kutekezwa kutoka katika kundi, atatoa dume asiyekuwa na kasoro. Atamtoa katika mlango wa kuingilia katika hema ya kukutania, ili iwe imekubaliwa mbele za Bwana.
Jeźli całopalona ofiara jego będzie z rogatego bydła, samca zupełnego ofiarować będzie; u drzwi namiotu zgromadzenia ofiarować go będzie dobrowolnie przed obliczem Pańskiem.
4 Ataweka mikono yake kichwani pa sadaka ya kuteketezwa, na ndipo itakuwa imekubaliwa badala yake kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe.
I położy rękę swą na głowę ofiary całopalenia, a będzie przyjemną zań na oczyszczenie jego.
5 Ndipo atapaswa kuchinja ng'ombe mbele ya Bwana. Watoto wa Aroni, makuhani wataleta damu na kuinyunyizia katika madhabahu iliyo katika mlango wa kuingilia katika hema la kukutania.
Zabije tedy cielca tego kapłan przed oblicznością Pańską; a synowie Aaronowi, kapłani, ofiarować będą krew, a pokropią tą krwią ołtarz z wierzchu w około, który jest przede drzwiami namiotu zgromadzenia.
6 Ndipo ataichuna sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande.
A wziąwszy skórę z ofiary całopalenia rozrąbie ją na sztuki.
7 Kisha wana wa Haruni kuhani wataweka moto katika madhabahu na kuweka kuni ili kuchochea moto.
Potem nałożą synowie Aarona kapłana, ogień na ołtarzu, a ułożą drwa na ogień.
8 Wana wa Haruni, makuhani wataweka vipande, kichwa na mafuta, watazipanga juu ya kuni zilizoko juu ya moto ulio madhabahuni.
Potem porządnie włożą synowie Aaronowi, kapłani, one sztuki, głowę, i tłustość, na drwa, które są na ogniu, który jest na ołtarzu.
9 Lakini matumbo yake na miguu lazima ataiosha kwa maji. Kisha kuhani atateketeza kila kitu kilicho juu ya madhabahu kama sadaka ya kuteketeza. Italeta harufu nzuri sana kwangu; itakuwa sadaka iliyotolewa kwa moto kwa ajili yangu.
A wnętrzności jego, i nogi jego, opłucze wodą, i zapali kapłan to wszystko na ołtarzu; całopalenie jest ofiary ognistej ku wdzięcznej wonności Panu.
10 Kama sadaka kwa ajili ya sadaka ya kuteketeza kutoka kundi, kondoo au mbuzi, lazima atoe dume asiye na kasoro.
A jeźliżby z drobnego bydła kto chciał ofiarować z owiec albo z kóz, na ofiarę całopalenia, samca zupełnego ofiarować będzie;
11 Lazima atamchinja juu ya madhabahu iliyo katika upande wa kaskazini mbele ya Bwana. Wana wa Haruni makuhani, watanyunyiza damu kila upande wa madhabahu.
I zabije go po bok ołtarza ku północy przed oblicznością Pańską; a pokropią synowie Aaronowi, kapłani, krwią jego po wierzchu ołtarza w około.
12 Kisha ataikata katika vipande, pamoja na kichwa na mafuta yake, kuhani atavipanga juu ya kuni zilizo katika moto ulio madhabahuni,
I rozrąbie go na sztuki, i głowę jego, i tłustość jego; a włoży je kapłan porządnie na drwa, które są na ogniu, który jest na ołtarzu.
13 lakini matumbo yake na miguu yake lazima ioshwe kwa maji. Kisha kuhani atatoa yote na kuiteketeza juu ya madhabahu. Ni sadaka ya kuteketezwa, italeta harufu nzuri kwa ajili ya Bwana; itakuwa sadaka ya Bwana iliyotolewa kwa moto.
A wnętrzności i nogi opłucze wodą; i będzie ofiarował kapłan to wszystko, i zapali to na ołtarzu. Całopalenie jest ofiary ognistej ku wdzięcznej wonności Panu.
14 Kama sadaka yake kwa Bwana itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa ni ndege, ndipo ataleta kama sadaka yake aidha ni huwa au kinda la njiwa.
A jeźliby z ptastwa całopalenia ofiarę chciał kto ofiarować Panu, tedy niech przyniesie z synogarlic, albo z gołąbiąt ofiarę swoję.
15 Kuhani ataileta madhabahuni, atamnyonga kichwa chake, na kuiteketeza juu ya madhabahu. Kisha damu yake itachuruzishwa juu ya pande za madhabahu.
A będzie ją ofiarował kapłan na ołtarzu, i paznogciem nadrze głowę jego, i zapali na ołtarzu, wycisnąwszy krew jego na stronie ołtarza.
16 Kisha atakiondoa kibofu chake pamoja na uchafu wake, na kukiweka upande wa mashariki mwa madhabahu, katika sehemu ya majivu.
Odejmie też gardziel jego z pierzem jego, a porzuci je blisko ołtarza ku wschodniej stronie, na miejsce, gdzie popiół bywa;
17 Kisha atapasua mabawa yake, lakini hatagawanya katika vipande viwili. Kisha Kuhani atamtekeza katika madhabahu, juu ya kuni amabazo ziko juu ya moto. Itakuwa sadaka ya kuteketezwa, na italeta harufu nzuri sana kwa Bwana; itakuwa sadaka ya Bwana iliyotolewa kwa moto.
I rozedrze mu skrzydła jego, a wszakże ich nie oderwie; i spali to kapłan na ołtarzu, na drwach, które są na ogniu; całopalenie jest ofiary ognistej ku wdzięcznej wonności Panu.

< Mambo ya Walawi 1 >