< Maombolezo 5 >
1 Kumbuka, Yahweh, yaliyo tutokea na uone aibu yetu.
Ricordati, Signore, di quanto ci è accaduto, guarda e considera il nostro obbrobrio.
2 Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni; nyumba zetu kwa wageni.
La nostra eredità è passata a stranieri, le nostre case a estranei.
3 Tumekuwa yatima, bila baba, na mama zetu ni kama wajane.
Orfani siam diventati, senza padre; le nostre madri come vedove.
4 Lazima tulipe fedha kwa maji tunayo kunywa, na tulipe fedha kupata mbao zetu.
L'acqua nostra beviamo per denaro, la nostra legna si acquista a pagamento.
5 Hao wanakuja kwetu wamekaribia nyuma yetu; tumechoka na hatuwezi pata mapumziko.
Con un giogo sul collo siamo perseguitati siamo sfiniti, non c'è per noi riposo.
6 Tumejitoa kwa Misri na kwa Assiria tupate chakula cha kutosha.
All'Egitto abbiamo teso la mano, all'Assiria per saziarci di pane.
7 Baba zetu walifanya dhambi, na hawapo tena, na tumebeba dhambi zao.
I nostri padri peccarono e non sono più, noi portiamo la pena delle loro iniquità.
8 Watumwa walitutawala, na hakuna wa kutuokoa na mikono yao.
Schiavi comandano su di noi, non c'è chi ci liberi dalle loro mani.
9 Tunapata mkate wetu pale tunapo hatarisha maisha, kwasababu ya upanga wa nyikani.
A rischio della nostra vita ci procuriamo il pane davanti alla spada nel deserto.
10 Ngozi zetu zimekuwa na moto kama jiko kwasababu ya joto la njaa.
La nostra pelle si è fatta bruciante come un forno a causa degli ardori della fame.
11 Wanawake wanabakwa Sayuni, na mabikra katika mji wa Yuda.
Han disonorato le donne in Sion, le vergini nelle città di Giuda.
12 Watoto wa mfalme wamenyongwa na mikono yao, na hakuna heshima inayoonyeshwa kwa wazee.
I capi sono stati impiccati dalle loro mani, i volti degli anziani non sono stati rispettati.
13 Wanaume vijana wanalizimishwa kusaga mbegu kwa jiwe la kusagia, na wavulana wanajikwa chini ya vifurushi vya kuni.
I giovani han girato la mola; i ragazzi son caduti sotto il peso della legna.
14 Wazee wameacha lango la mji, na vijana wameacha miziki.
Gli anziani hanno disertato la porta, i giovani i loro strumenti a corda.
15 Furaha ya moyo imekoma na kucheza kwetu kumegeuka kilio.
La gioia si è spenta nei nostri cuori, si è mutata in lutto la nostra danza.
16 Taji limeanguka kichwani mwetu; ole wetu, kwa kuwa tumetenda dhambi!
E' caduta la corona dalla nostra testa; guai a noi, perché abbiamo peccato!
17 Kwa kuwa moyo wetu umekuwa unaumwa, na machozi yetu ya fifia, kwa vitu hivi macho yetu yanafifia
Per questo è diventato mesto il nostro cuore, per tali cose si sono annebbiati i nostri occhi:
18 maana Mlima Sayuni umelala ukiwa, mbwa wa mitaani wacheza juu yake.
perché il monte di Sion è desolato; le volpi vi scorrazzano.
19 Lakini wewe, Yahweh, unatawala milele, na utaketi katika kiti chako cha enzi vizazi na vizazi. Kwanini unatusahau milele?
Ma tu, Signore, rimani per sempre, il tuo trono di generazione in generazione.
20 Kwanini unatutelekeza kwa siku nyingi?
Perché ci vuoi dimenticare per sempre? Ci vuoi abbandonare per lunghi giorni?
21 Turejeshe kwako, Yahweh, na sisi tutarejea. Fanya upya siku zetu kama zilivyo kuwa hapo zamani -
Facci ritornare a te, Signore, e noi ritorneremo; rinnova i nostri giorni come in antico,
22 vinginevyo labda uwe umetukataa na una hasira kwetu kupita kiasi.
poiché non ci hai rigettati per sempre, nè senza limite sei sdegnato contro di noi.