< Maombolezo 3 >
1 Mimi ni mwanaume nilyeona maangaiko chini ya gongo la hasira ya Yahweh.
Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake.
2 Amenifukuza na kunisababisha kutembea kwenye giza kuliko kwenye nuru.
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
3 Hakika amenigeuzia mkono wake dhidi yangu tena na tena, siku yote.
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
4 Amefanya mwili wangu na ngozi yangu kufifia; amevunja mifupa yangu.
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
5 Amejenga vifusi vya udogo dhidi yangu, na kunizingira na uchungu na ugumu.
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
6 Amefanya ni ishi sehemu za giza, kama hao walio kufa zamani.
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
7 Amejenga ukuta kunizunguka na siwezi kutoroka. Amefanya minyororo yangu mizito
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
8 na japo nina ita na kulilia msaada, anazima maombi yangu.
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
9 Ameziba njia yangu kwa ukuta wa mawe ya kuchonga; amefanya njia yangu mbaya.
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
10 Yeye ni kama dubu anasubiri kunishambulia, simba katika maficho;
Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni,
11 amegeuza pembeni njia zangu, amenifanya ukiwa.
ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada.
12 Amepindisha upinde wake na kunifanya mimi kama lengo la mshale wake.
Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake.
13 Ametoboa maini yangu kwa mishale ya mfuko wake.
Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake.
14 Nilikuwa kichekesho kwa watu wangu wote, kielelezo cha dhihaka yao siku nzima.
Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.
15 Amenijaza kwa uchungu na kunilazimisha kunywa maji machungu.
Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo.
16 Alivunja meno yangu na kokoto; amenisukuma chini kwenye fumbi.
Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini.
17 Nafsi yangu imenyimwa amani; nimesahau furaha ni nini.
Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini.
18 Hivyo na sema, “Ustahimilivu wangu umeangamia na pia tumaini langu kwa Yahweh.”
Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”
19 Kumbuka mateso yangu na kuangaika kwangu, maji machungu na uchungu.
Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo.
20 Ninaendelea kukumbuka na nimeinama ndani yangu.
Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.
21 Lakini ni vuta hili akilini mwangu na hivyo nina matumaini:
Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini.
22 Upendo dhabiti wa Yahweh haukomi na huruma zake haziishi,
Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.
23 ni mpya kila asubui; uaminifu wako ni mkubwa.
Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu.
24 “Yahweh ni urithi wangu,” Nilisema, hivyo nitamtumainia.
Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”
25 Yahweh ni mwema kwao wanao msubiri, kwa anaye mtafuta.
Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta;
26 Ni vizuri kusubiri taratibu kwa uwokovu wa Yahweh.
ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana.
27 Ni vizuri kwa mtu kubeba nira katika ujana.
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
28 Acha aketi peke yake katika utulivu, inapo kuwa imewekwa juu yake.
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
29 Acha aeke mdomo wake kwenye vumbi - kunaweza bado kuwa na matumaini.
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
30 Acha atoa shavu lake kwa yeye anaye mpiga, na ajazwe tele kwa aibu.
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
31 Kwa kuwa Bwana hatatukataa milele,
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.
32 lakini japo anatia uzuni, ata kuwa na huruma kwa kadiri ya mwingi wa upendo wake dhabiti.
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
33 Kwa kuwa haadhibu kutoka moyoni mwake au kutesa watoto wa mwanadamu.
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
34 Kukanyaga chini ya mguu wafungwa wote wa dunia,
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
35 kumnyima haki mtu mbele ya uwepo wa Aliye Juu,
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
36 mkunyima haki mtu - Bwana hataidhinisha vitu kama hivyo!
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
37 Ni nani aliye zungumza na ikatimia, kama sio Bwana kutamka?
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
38 Sio kutoka mdomoni mwa Aliye Juu majanga na mazuri yanakuja?
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
39 Mtu aliye hai anawezaje kulalamika? Mtu anawezaje kulalamika kwa adhabu ya dhambi zake?
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
40 Natujichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Yahweh.
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
41 Na tunyanyue mioyo yetu na mikono yetu kwa Yahweh mbinguni:
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
42 “Tumekosea na kuasi, na haujasamehe.
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
43 Umejifunika na hasira na kutukimbiza, umeua na haujanusuru.
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
44 Umejifunika na wingu ili kwamba kusiwe na ombi linaloweza kupita.
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
45 Umetufanya kama uchafu na taka miongoni mwa mataifa.
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
46 Maadui wetu wote wametulaani,
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
47 wasiwasi na shimo limetujia, maafa na uharibifu.
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
48 Macho yangu yanatiririka na miferiji ya machozi kwasababu ya watu wangu.
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
49 Macho yangu yatatoa machozi pasipo kikomo; pasipo hauweni,
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
50 mpaka atakapo tazama chini na Yahweh ataona kutoka mbinguni.
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
51 Macho yangu yana ni sababishia uzuni kwasababu ya mabinti wa mji wangu.
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
52 Nimewindwa kama ndege hao walio kuwa maadui zangu; wameniwinda pasipo sababu.
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
53 Wamenitupa kwenye shimo na wakanitupia jiwe,
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
54 na maji yaka mwagika juu ya kichwa changu. Nilisema, “Nimekatwa mbali!”
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
55 Nililiita jna lako, Yahweh, kutoka kina cha shimo.
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
56 Ulisikia sauti yangu. Ulisikia sauti yangu nilipo sema, “Usifunge sikio lako kwa kilio changu cha msaada.”
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
57 Ulikuja karibu siku niliyo kuiita; ulisema, “Usiogope”
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
58 Bwana, ulitetea kesi yangu, uliokoa maisha yangu!
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
59 Yahweh, umeona mabaya waliyo ni fanyia, hukumu kesi yangu.
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
60 Umeona matusi yao, mipango yao yote dhidi yangu -
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
61 Umesikia dhihaka yao, Yahweh, na mipango yao kunihusu.
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
62 Midomo ya hao wanao inuka kinyume changu, na mashtaka yao, inakuja dhidi yangu siku nzima.
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
63 Ngalia jinsi wanavyo keti na kuinuka; wana nidhihaki na nyimbo zao.
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
64 Walipize, Yahweh, kwa kadiri ya waliyo fanya.
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
65 Utaacha mioyo yao bila lawama! Hukumu yako iwe juu yao!
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
66 Una wakimbiza kwa hasira na kuwaharibu nchini ya mbingu, Yahweh!
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.