< Maombolezo 3 >

1 Mimi ni mwanaume nilyeona maangaiko chini ya gongo la hasira ya Yahweh.
אני הגבר ראה עני בשבט עברתו׃
2 Amenifukuza na kunisababisha kutembea kwenye giza kuliko kwenye nuru.
אותי נהג וילך חשך ולא אור׃
3 Hakika amenigeuzia mkono wake dhidi yangu tena na tena, siku yote.
אך בי ישב יהפך ידו כל היום׃
4 Amefanya mwili wangu na ngozi yangu kufifia; amevunja mifupa yangu.
בלה בשרי ועורי שבר עצמותי׃
5 Amejenga vifusi vya udogo dhidi yangu, na kunizingira na uchungu na ugumu.
בנה עלי ויקף ראש ותלאה׃
6 Amefanya ni ishi sehemu za giza, kama hao walio kufa zamani.
במחשכים הושיבני כמתי עולם׃
7 Amejenga ukuta kunizunguka na siwezi kutoroka. Amefanya minyororo yangu mizito
גדר בעדי ולא אצא הכביד נחשתי׃
8 na japo nina ita na kulilia msaada, anazima maombi yangu.
גם כי אזעק ואשוע שתם תפלתי׃
9 Ameziba njia yangu kwa ukuta wa mawe ya kuchonga; amefanya njia yangu mbaya.
גדר דרכי בגזית נתיבתי עוה׃
10 Yeye ni kama dubu anasubiri kunishambulia, simba katika maficho;
דב ארב הוא לי אריה במסתרים׃
11 amegeuza pembeni njia zangu, amenifanya ukiwa.
דרכי סורר ויפשחני שמני שמם׃
12 Amepindisha upinde wake na kunifanya mimi kama lengo la mshale wake.
דרך קשתו ויציבני כמטרא לחץ׃
13 Ametoboa maini yangu kwa mishale ya mfuko wake.
הביא בכליותי בני אשפתו׃
14 Nilikuwa kichekesho kwa watu wangu wote, kielelezo cha dhihaka yao siku nzima.
הייתי שחק לכל עמי נגינתם כל היום׃
15 Amenijaza kwa uchungu na kunilazimisha kunywa maji machungu.
השביעני במרורים הרוני לענה׃
16 Alivunja meno yangu na kokoto; amenisukuma chini kwenye fumbi.
ויגרס בחצץ שני הכפישני באפר׃
17 Nafsi yangu imenyimwa amani; nimesahau furaha ni nini.
ותזנח משלום נפשי נשיתי טובה׃
18 Hivyo na sema, “Ustahimilivu wangu umeangamia na pia tumaini langu kwa Yahweh.”
ואמר אבד נצחי ותוחלתי מיהוה׃
19 Kumbuka mateso yangu na kuangaika kwangu, maji machungu na uchungu.
זכר עניי ומרודי לענה וראש׃
20 Ninaendelea kukumbuka na nimeinama ndani yangu.
זכור תזכור ותשיח עלי נפשי׃
21 Lakini ni vuta hili akilini mwangu na hivyo nina matumaini:
זאת אשיב אל לבי על כן אוחיל׃
22 Upendo dhabiti wa Yahweh haukomi na huruma zake haziishi,
חסדי יהוה כי לא תמנו כי לא כלו רחמיו׃
23 ni mpya kila asubui; uaminifu wako ni mkubwa.
חדשים לבקרים רבה אמונתך׃
24 “Yahweh ni urithi wangu,” Nilisema, hivyo nitamtumainia.
חלקי יהוה אמרה נפשי על כן אוחיל לו׃
25 Yahweh ni mwema kwao wanao msubiri, kwa anaye mtafuta.
טוב יהוה לקוו לנפש תדרשנו׃
26 Ni vizuri kusubiri taratibu kwa uwokovu wa Yahweh.
טוב ויחיל ודומם לתשועת יהוה׃
27 Ni vizuri kwa mtu kubeba nira katika ujana.
טוב לגבר כי ישא על בנעוריו׃
28 Acha aketi peke yake katika utulivu, inapo kuwa imewekwa juu yake.
ישב בדד וידם כי נטל עליו׃
29 Acha aeke mdomo wake kwenye vumbi - kunaweza bado kuwa na matumaini.
יתן בעפר פיהו אולי יש תקוה׃
30 Acha atoa shavu lake kwa yeye anaye mpiga, na ajazwe tele kwa aibu.
יתן למכהו לחי ישבע בחרפה׃
31 Kwa kuwa Bwana hatatukataa milele,
כי לא יזנח לעולם אדני׃
32 lakini japo anatia uzuni, ata kuwa na huruma kwa kadiri ya mwingi wa upendo wake dhabiti.
כי אם הוגה ורחם כרב חסדו׃
33 Kwa kuwa haadhibu kutoka moyoni mwake au kutesa watoto wa mwanadamu.
כי לא ענה מלבו ויגה בני איש׃
34 Kukanyaga chini ya mguu wafungwa wote wa dunia,
לדכא תחת רגליו כל אסירי ארץ׃
35 kumnyima haki mtu mbele ya uwepo wa Aliye Juu,
להטות משפט גבר נגד פני עליון׃
36 mkunyima haki mtu - Bwana hataidhinisha vitu kama hivyo!
לעות אדם בריבו אדני לא ראה׃
37 Ni nani aliye zungumza na ikatimia, kama sio Bwana kutamka?
מי זה אמר ותהי אדני לא צוה׃
38 Sio kutoka mdomoni mwa Aliye Juu majanga na mazuri yanakuja?
מפי עליון לא תצא הרעות והטוב׃
39 Mtu aliye hai anawezaje kulalamika? Mtu anawezaje kulalamika kwa adhabu ya dhambi zake?
מה יתאונן אדם חי גבר על חטאו׃
40 Natujichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Yahweh.
נחפשה דרכינו ונחקרה ונשובה עד יהוה׃
41 Na tunyanyue mioyo yetu na mikono yetu kwa Yahweh mbinguni:
נשא לבבנו אל כפים אל אל בשמים׃
42 “Tumekosea na kuasi, na haujasamehe.
נחנו פשענו ומרינו אתה לא סלחת׃
43 Umejifunika na hasira na kutukimbiza, umeua na haujanusuru.
סכתה באף ותרדפנו הרגת לא חמלת׃
44 Umejifunika na wingu ili kwamba kusiwe na ombi linaloweza kupita.
סכותה בענן לך מעבור תפלה׃
45 Umetufanya kama uchafu na taka miongoni mwa mataifa.
סחי ומאוס תשימנו בקרב העמים׃
46 Maadui wetu wote wametulaani,
פצו עלינו פיהם כל איבינו׃
47 wasiwasi na shimo limetujia, maafa na uharibifu.
פחד ופחת היה לנו השאת והשבר׃
48 Macho yangu yanatiririka na miferiji ya machozi kwasababu ya watu wangu.
פלגי מים תרד עיני על שבר בת עמי׃
49 Macho yangu yatatoa machozi pasipo kikomo; pasipo hauweni,
עיני נגרה ולא תדמה מאין הפגות׃
50 mpaka atakapo tazama chini na Yahweh ataona kutoka mbinguni.
עד ישקיף וירא יהוה משמים׃
51 Macho yangu yana ni sababishia uzuni kwasababu ya mabinti wa mji wangu.
עיני עוללה לנפשי מכל בנות עירי׃
52 Nimewindwa kama ndege hao walio kuwa maadui zangu; wameniwinda pasipo sababu.
צוד צדוני כצפור איבי חנם׃
53 Wamenitupa kwenye shimo na wakanitupia jiwe,
צמתו בבור חיי וידו אבן בי׃
54 na maji yaka mwagika juu ya kichwa changu. Nilisema, “Nimekatwa mbali!”
צפו מים על ראשי אמרתי נגזרתי׃
55 Nililiita jna lako, Yahweh, kutoka kina cha shimo.
קראתי שמך יהוה מבור תחתיות׃
56 Ulisikia sauti yangu. Ulisikia sauti yangu nilipo sema, “Usifunge sikio lako kwa kilio changu cha msaada.”
קולי שמעת אל תעלם אזנך לרוחתי לשועתי׃
57 Ulikuja karibu siku niliyo kuiita; ulisema, “Usiogope”
קרבת ביום אקראך אמרת אל תירא׃
58 Bwana, ulitetea kesi yangu, uliokoa maisha yangu!
רבת אדני ריבי נפשי גאלת חיי׃
59 Yahweh, umeona mabaya waliyo ni fanyia, hukumu kesi yangu.
ראיתה יהוה עותתי שפטה משפטי׃
60 Umeona matusi yao, mipango yao yote dhidi yangu -
ראיתה כל נקמתם כל מחשבתם לי׃
61 Umesikia dhihaka yao, Yahweh, na mipango yao kunihusu.
שמעת חרפתם יהוה כל מחשבתם עלי׃
62 Midomo ya hao wanao inuka kinyume changu, na mashtaka yao, inakuja dhidi yangu siku nzima.
שפתי קמי והגיונם עלי כל היום׃
63 Ngalia jinsi wanavyo keti na kuinuka; wana nidhihaki na nyimbo zao.
שבתם וקימתם הביטה אני מנגינתם׃
64 Walipize, Yahweh, kwa kadiri ya waliyo fanya.
תשיב להם גמול יהוה כמעשה ידיהם׃
65 Utaacha mioyo yao bila lawama! Hukumu yako iwe juu yao!
תתן להם מגנת לב תאלתך להם׃
66 Una wakimbiza kwa hasira na kuwaharibu nchini ya mbingu, Yahweh!
תרדף באף ותשמידם מתחת שמי יהוה׃

< Maombolezo 3 >