< Waamuzi 1 >
1 Baada ya kifo cha Yoshua, wana wa Israeli walimuuliza Yahweh wakisema, “Ni nani atawashambulia kwanza Wakanaani kwa ajili yetu, ili kupigana nao?
And it was after [the] death of Joshua and they enquired [the] people of Israel by Yahweh saying who? will he go up for us against the Canaanite[s] at the first to engage in battle against him.
2 Yahweh akasema, “Yuda atawashambulia. Tazama, nimewapa kumiliki nchi hii.
And he said Yahweh Judah he will go up here! I have given the land in hand his.
3 Watu wa Yuda wakawaambia wana wa Simeoni, ndugu zao, “Njoo pamoja nasi katika eneo letu ambalo tumepewa ili kwa pamoja tupigane na Wakanaani. Na sisi pia tutakwenda nanyi katika eneo mlilopewa.” Basi kabila la Simeoni wakaenda pamoja nao.
And he said Judah to Simeon brother his come up with me in lot my so let us fight against the Canaanite[s] and I will go also I with you in lot your and he went with him Simeon.
4 Watu wa Yuda wakashinda, na Bwana akawapa ushindi juu ya Wakanaani na Waperizi. Wakawaua watu elfu kumi huko Bezeki.
And he went up Judah and he gave Yahweh the Canaanite[s] and the Perizzite[s] in hand their and they defeated them at Bezek ten thousand man.
5 Wakamkuta Adoni Bezeki huko Bezeki, nao wakapigana naye na kuwashinda Wakanaani na Waperizi.
And they found Adoni-Bezek at Bezek and they fought against him and they defeated the Canaanite[s] and the Perizzite[s].
6 Lakini Adoni Bezeki akamkimbilia, wakamfuata na kumshika, nao wakavikata vidole gumba na vidole vyake vikubwa.
And he fled Adoni-Bezek and they pursued after him and they seized him and they cut off [the] thumbs of hands his and feet his.
7 Adoni Bezek akasema, “Wafalme sabini, ambao na vidole gumba vyako na vidole vikubwa vilivyokatwa, walikusanya chakula chao chini ya meza yangu. Kama nilivyofanya, hata hivyo Mungu amefanya kwangu.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
And he said Adoni-Bezek seventy - kings [the] thumbs of hands their and feet their cut off they were gathering up under table my just as I have done so he has repaid to me God and they brought him Jerusalem and he died there.
8 Watu wa Yuda wakapigana dhidi ya jiji la Yerusalemu na kulichukua. Walishambulia kwa makali ya upanga na wakauwasha mji kwa moto.
And they fought [the] descendants of Judah against Jerusalem and they captured it and they struck it to [the] mouth of [the] sword and the city they sent in fire.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda walikwenda kupigana na Wakanaani waliokaa mlimani, Negebu, na magharibi mwa milima.
And after they went down [the] descendants of Judah to fight against the Canaanite[s] [who] dwelt of the hill country and the Negev and the Shephelah.
10 Yuda akaenda dhidi ya Wakanaani waliokaa Hebroni (jina la Hebroni hapo awali ilikuwa Kiriath-arba), nao wakamshinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
And he went Judah against the Canaanite[s] who dwelt in Hebron and [the] name of Hebron before [was] Kiriath Arba and they defeated Sheshai and Ahiman and Talmai.
11 Kutoka huko watu wa Yuda walipigana na wenyeji wa Debiri (jina la Debiri hapo awali ilikuwa Kiriath-seferi).
And he went from there against [the] inhabitants of Debir and [the] name of Debir before [was] Kiriath Sepher.
12 Kalebu akasema, Yeyote atakayeivamia Kiriath-seferi na kuichukua, nitampa Aksa, binti yangu, awe mkewe.
And he said Caleb [the one] who he will strike Kiriath Sepher and he will capture it and I will give to him Achsah daughter my to a wife.
13 Otinieli, mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, akaiteka Debiri, naye Kalebu akampa Aksa, binti yake, awe mkewe.
And he captured it Othniel [the] son of Kenaz [the] brother of Caleb young more than him and he gave to him Achsah daughter his to a wife.
14 Ndipo Aksa alifika kwa Othnieli, naye akamsihi amuombe baba yake ampe shamba. Alipokuwa akishuka katika punda wake, Kalebu akamwuliza, “Nikufanyie nini?”
And it was when came she and she incited him to ask from with father her the field and she went down from on the donkey and he said to her Caleb what? [is] to you.
15 Akamwambia, Nibariki. Kwa kuwa umenipa nchi ya Negebu, nipe pia chemchemi za maji. Kwa hiyo Kalebu akampa chemchemi za juu na chemchemi za chini.
And she said to him give! to me a blessing for [the] land of the Negev you have given to me and you will give to me springs of water and he gave to her Caleb springs upper and springs lower.
16 Kizazi cha Mkeeni shemeji yake na Musa, walikwenda kutoka mji wa Mitende pamoja na watu wa Yuda, mpaka jangwa la Yuda, ambalo liko Negevu, kuishi na watu wa Yuda karibu na Arad.
And [the] descendants of [the] Kenite [the] father-in-law of Moses they went up from [the] city of the palm trees with [the] descendants of Judah [the] wilderness of Judah which [is] in [the] Negev Arad and he went and he dwelt with the people.
17 Nao watu wa Yuda wakaenda pamoja na wana wa Simeoni ndugu zao, wakawaangamiza Wakanaani waliokaa Zefathi, wakaiharibu kabisa. Mji uliitwa Horma.
And he went Judah with Simeon brother his and they attacked the Canaanite[s] [who] dwelt of Zephath and they totally destroyed it and he called [the] name of the city Hormah.
18 Watu wa Yuda pia waliiteka Gaza na nchi iliyoizunguka, Ashkeloni na nchi iliyoizunguka, na Ekron na nchi iliyoizunguka.
And he captured Judah Gaza and territory its and Ashkelon and territory its and Ekron and territory its.
19 Yahweh alikuwa pamoja na watu wa Yuda na wakaimiliki nchi ya milima, lakini hawakuweza kuwatoa wenyeji wa kwenye bonde kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
And he was Yahweh (with *L(abh)*) Judah and it took possession of the hill country for not to dispossess [the] inhabitants of the valley for chariotry of iron [belonged] to them.
20 Hebroni alipewa Kalebu (kama Musa alivyosema), naye akawafukuza kutoka huko wana watatu wa Anaki.
And people gave to Caleb Hebron just as he had said Moses and he dispossessed from there three [the] sons of Anak.
21 Lakini wana wa Benyamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa Yerusalemu. Basi Wayebusi wakakaa na watu wa Benyamini huko Yerusalemu hata leo.
And the Jebusite[s] [who] dwelt of Jerusalem not they dispossessed [the] descendants of Benjamin and he has dwelt the Jebusite[s] with [the] descendants of Benjamin in Jerusalem until the day this.
22 Nyumba ya Yusufu ilijiandaa kuishambulia Betheli, na Yahweh alikuwa pamoja nao.
And they went up [the] house of Joseph also they Beth-el and Yahweh [was] with them.
23 Walipeleka watu kuipeleleza Betheli (jiji lililoitwa Luzu).
And they caused to spy out [the] house of Joseph at Beth-el and [the] name of the city before [was] Luz.
24 Wapelelezi waliona mtu akitoka nje ya jiji, wakamwambia, “Tafadhali tuonyeshe jinsi ya kuingia ndani ya jiji, na tutakutendea mema.”
And they saw those [who] watched a man coming out from the city and they said to him show us please [the] entrance of the city and we will do with you loyalty.
25 Aliwaonyesha njia ya kuingia kwenye mji. Waliuteka mji kwa makali ya upanga, lakini wakamuacha mtu huyo na ndugu zake wote waondoke.
And he showed them [the] entrance of the city and they struck the city to [the] mouth of [the] sword and the man and all family his they let go.
26 Na mtu huyo akaenda nchi ya Wahiti, akajenga mji, akauita Luzu, ambalo jina lake hata leo.
And he went the man [the] land of the Hittites and he built a city and he called name its Luz that [is] name its until the day this.
27 Watu wa Manase hawakuwafukuza watu waliokuwa katika miji ya Bethsheani na vijiji vyake, au Taanaki na vijiji vyake, au wale waliokaa Dori na vijiji vyake, wala wale waliokaa Ibleamu na vijiji vyake, wala walioshi Megido na vijiji vyake, kwa sababu Wakanaani walikuwa wameamua kuishi katika nchi hiyo.
And not it took possession of Manasseh Beth Shean and daughters its and Taanach and daughters its and ([the] inhabitants of *Q(K)*) Dor and daughters its and [the] inhabitants of Ibleam and daughters its and [the] inhabitants of Megiddo and daughters its and it was determined the Canaanite[s] to dwell in the land this.
28 Israeli ipokuwa na nguvu, waliwalazimisha Wakanaani wawatumikie kwa kazi ngumu, lakini hawakuwafukuza kabisa.
And it was that it became strong Israel and it made the Canaanite[s] into forced labor and certainly not it dispossessed him.
29 Efraimu hakuwafukuza Wakanaani waliokaa Gezeri; kwa hiyo Wakanaani wakakaa kati yao.
And Ephraim not it dispossessed the Canaanite[s] who dwelt in Gezer and it dwelt the Canaanite[s] in midst its in Gezer.
30 Zebuloni hakuwafukuza watu wa Kitroni, wala watu waliokuwa Nahaloli; na Wakanaani wakaendelea kuishi pamoja nao; lakini Zabuloni akawalazimisha Wakanaani wawatumikie kwa kazi ngumu.
Zebulun not it dispossessed [the] inhabitants of Kitron and [the] inhabitants of Nahalol and it dwelt the Canaanite[s] in midst its and they became forced labor.
31 Asheri hakuwafukuza watu wanaoishi Aka, au watu wanaoishi Sidoni, au wale wanaoishi Alabu, Akzib, Helba, Afeka, au Rehobu.
Asher not it dispossessed [the] inhabitants of Acco and [the] inhabitants of Sidon and Ahlab and Aczib and Helbah and Aphek and Rehob.
32 Kwa hiyo kabila ya Asheri iliishi kati ya Wakanaani (waliokaa katika nchi hiyo), kwa sababu hawakuwafukuza.
And it dwelt the Asherite[s] in [the] midst of the Canaanite[s] [the] inhabitants of the land for not it dispossessed it.
33 Na kabila la Naftali halikuwafukuza watu waliokuwa wakiishi Bethshemeshi, wala waliokuwa wakiishi Bethanathi. Kwa hiyo kabila la Naftali liliishi kati ya Wakanaani (watu waliokuwa wakiishi katika nchi hiyo). Hata hivyo, wenyeji wa Bethshemeshi na Bethanathi walilazimishwa kufanya kazi ngumu kwa Naphthali.
Naphtali not it dispossessed [the] inhabitants of Beth Shemesh and [the] inhabitants of Beth Anath and it dwelt in [the] midst of the Canaanite[s] [the] inhabitants of the land and [the] inhabitants of Beth Shemesh and Beth Anath they became for them forced labor.
34 Waamori waliwalazimisha kabila la Dani kuishi katika nchi ya kilima, hawakuwaruhusu kuja bondeni.
And they pressed the Amorite[s] [the] descendants of Dan the hill country towards for not it permitted it to go down to the valley.
35 Basi Waamori waliishi katika mlima wa Heresi, huko Aiyaloni, na Shaalbimu, lakini nguvu za kijeshi za nyumba ya Yusufu ziliwashinda, nao wakalazimishwa kuwatumikia kwa kazi ngumu.
And it was determined the Amorite[s] to dwell in [the] mountain of Heres in Aijalon and in Shaalbim and it was heavy [the] hand of [the] house of Joseph and they became forced labor.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kutoka kilima cha Akrabimu huko Sela hadi nchi ya vilima.
And [the] border of the Amorite[s] [was] from [the] ascent of scorpions from Sela and up-wards.