< Waamuzi 8 >
1 Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
And the men of Ephraim said to him, “What is this, that you wanted to do, so that you would not call us when you went to fight against Midian?” And they rebuked him strongly, and came close to using violence.
2 Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
And he responded to them: “But what could I have done that would be so great as what you have done? Is not one bunch of grapes of Ephraim better than the vintages of Abiezer?
3 Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
The Lord has delivered into your hands the leaders of Midian, Oreb and Zeeb. What could I have done that would be so great as what you have done?” And when he had said this, their spirit, which was swelling up against him, was quieted.
4 Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
And when Gideon had arrived at the Jordan, he crossed over it with the three hundred men who were with him. And they were so weary that they were unable to pursue those who were fleeing.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
And he said to the men of Succoth, “I beg you, give bread to the people who are with me, for they are greatly weakened, so that we may be able to pursue Zebah and Zalmunna, the kings of Midian.”
6 Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
The leaders of Succoth answered, “Perhaps the palms of the hands of Zebah and Zalmunna are in your hand, and for this reason, you request that we give bread to your army.”
7 Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
And he said to them, “So then, when the Lord will have delivered Zebah and Zalmunna into my hands, I will thresh your flesh with the thorns and briers of the desert.”
8 Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
And going up from there, he arrived at Penuel. And he spoke to the men of that place similarly. And they also answered him, just as the men of Succoth had answered.
9 Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
And so he said to them also, “When I will have returned as a victor in peace, I will destroy this tower.”
10 Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
Now Zebah and Zalmunna were resting with their entire army. For fifteen thousand men were left out of all the troops of the eastern people. And one hundred twenty thousand warriors that drew the sword had been cut down.
11 Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
And Gideon ascended by the way of those who were dwelling in tents, to the eastern part of Nobah and Jogbehah. And he struck the camp of the enemies, who were confident and were suspecting nothing adverse.
12 Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
And Zebah and Zalmunna fled. And Gideon pursued and overtook them, sending their entire army into confusion.
13 Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
And returning from the war before sunrise,
14 Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
he took a boy from among the men of Succoth. And he asked him the names of the leaders and elders of Succoth. And he described seventy-seven men.
15 Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
And he went to Succoth, and he said to them: “Behold Zebah and Zalmunna, over whom you rebuked me, saying: ‘Perhaps the hands of Zebah and Zalmunna are in your hands, and for this reason, you request that we give bread to men who are languishing and weakened.’”
16 Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
Therefore, he took the elders of the city, and, using the thorns and briers of the desert, he threshed them with these, and he cut the men of Succoth to pieces.
17 Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
He also overturned the tower of Penuel, and he killed the men of the city.
18 Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
And he said to Zebah and Zalmunna, “What kind of men were those whom you killed at Tabor?” They responded, “They were like you, and one of them was like the son of a king.”
19 Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
He answered them: “They were my brothers, the sons of my mother. As the Lord lives, if you had preserved them, I would not kill you.”
20 Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
And he said to Jether, his firstborn son, “Rise up, and put them to death.” But he did not draw his sword. For he was afraid, being still a boy.
21 Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
And Zebah and Zalmunna said: “You should rise up and rush against us. For the strength of a man is in accord with his age.” Gideon rose up, and he killed Zebah and Zalmunna. And he took the ornaments and studs, with which the necks of the royal camels are usually adorned.
22 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
And all the men of Israel said to Gideon: “You should rule over us, and your son, and your son’s son. For you freed us from the hand of Midian.”
23 Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
And he said to them: “I will not rule over you. Neither shall my son rule over you. Instead, the Lord shall rule over you.”
24 Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
And he said to them: “I petition one request from you. Give me the earrings from your spoils.” For the Ishmaelites were accustomed to wear gold earrings.
25 Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
They responded, “We are very willing to give them.” And spreading a cloak on the ground, they cast upon it the earrings from the spoils.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
And the weight of the earrings that he requested was one thousand seven hundred shekels of gold, aside from the ornaments, and necklaces, and purple garments, which the kings of Midian were accustomed to use, and aside from the gold chains on the camels.
27 Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
And Gideon made an ephod from these, and he kept it in his city, Ophrah. And all of Israel committed fornication with it, and it became a ruin to Gideon and to all his house.
28 Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
But Midian was humbled before the sons of Israel. Neither were they able any longer to lift up their necks. But the land rested for forty years, while Gideon presided.
29 Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
And so Jerubbaal, the son of Joash, went and lived in his own house.
30 Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
And he had seventy sons, who went forth from his own thigh. For he had many wives.
31 Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
But his concubine, whom he had in Shechem, bore him a son named Abimelech.
32 Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
And Gideon, the son of Joash, died in a good old age, and he was buried in the sepulcher of his father, at Ophrah, of the family of Ezri.
33 Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
But after Gideon died, the sons of Israel turned away, and they committed fornication with the Baals. And they struck a covenant with Baal, so that he would be their god.
34 Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
And they did not remember the Lord their God, who rescued them from the hands of all their enemies on all sides.
35 Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.
Neither did they show mercy to the house of Jerubbaal Gideon, in accord with all the good that he had done for Israel.