< Waamuzi 7 >
1 Ndipo Yerubaali (yaani Gideoni) akainuka mapema, na watu wote waliokuwa pamoja naye, wakaweka kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Midiani ilikuwa kaskazini mwao katika bonde karibu na kilima cha More.
Et Jerubbaal, qui est Gédéon, et tout le peuple qui était avec lui, se levèrent de bonne heure et campèrent près de la source de Harod. Le camp de Madian était au nord, près de la colline de Moreh, dans la vallée.
2 Bwana akamwambia Gideoni, Kuna askari wengi sana kwa mimi kukupa ushindi juu ya Wamidiani, ili Waisraeli wasijisifu juu yangu, wakisema, 'Nguvu zetu zimetuokoa'.
Yahvé dit à Gédéon: « Le peuple qui est avec toi est trop nombreux pour que je livre les Madianites entre leurs mains, de peur qu'Israël ne se vante de moi en disant: « Ma propre main m'a sauvé ».
3 Basi, tangaza masikioni mwa watu, ukisema, Yeyote anayeogopa, anayetetemeka, arudi na atoke katika mlima Gileadi. 'Basi, watu elfu ishirini na mbili wakaondoka, na elfu kumi wakabaki.
Maintenant, proclame aux oreilles du peuple: « Que celui qui a peur et qui tremble s'en retourne et s'éloigne de la montagne de Galaad ». Ainsi, vingt-deux mille personnes du peuple s'en retournèrent, et dix mille restèrent.
4 Bwana akamwambia Gideoni, 'Watu bado ni wengi sana. Wapeleke chini kwenye maji, na nitafanya idadi yao iwe ndogo kwa ajili yako. Kama nikisema, 'Huyu atakwenda pamoja nawe,' atakwenda pamoja nawe; lakini kama nikisema, 'Huyu hawezi kwenda pamoja nawe,' hatakwenda. '
Yahvé dit à Gédéon: « Il y a encore trop de monde. Fais-les descendre jusqu'à l'eau, et là, je les mettrai à l'épreuve pour toi. Ceux à qui je dirai: « Ceci ira avec vous » iront avec vous, et ceux à qui je dirai: « Ceci n'ira pas avec vous » n'iront pas. »
5 Gideoni akawapeleka watu kwenye maji; Bwana akamwambia, “Ondoa kila mtu atakayelamba maji, kama mbwa alambavyo, kutoka kwa wale wanaopiga magoti na kunywa.”
Il fit donc descendre le peuple vers l'eau, et Yahvé dit à Gédéon: « Si quelqu'un lèche l'eau avec sa langue, comme un chien, tu le mettras à part, et si quelqu'un s'agenouille pour boire, tu le mettras à part. »
6 Wanaume mia tatu walilamba. Wengine wote walipiga magoti kunywa maji.
Le nombre de ceux qui laperont l'eau, en portant la main à la bouche, sera de trois cents hommes; mais tout le reste du peuple se prosternera à genoux pour boire l'eau.
7 Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa watu hawa mia tatu waliokwisha kulamba maji, nitakuokoa na kukupa ushindi juu ya Wamidiani. Acha kila mtu arudi mahali pake.”
Yahvé dit à Gédéon: « Je te sauverai par les trois cents hommes qui ont lapé, et je livrerai les Madianites entre tes mains. Laisse partir tout le reste du peuple, chacun à sa place. »
8 Kwa hiyo wale waliochaguliwa walichukua vifaa vyao na tarumbeta zao. Gideoni akawarudisha watu wote wa Israeli, kila mtu kwenda kwenye hema yake, lakini akawaweka watu mia tatu. Basi kambi ya Midiani ilikuwa chini yake katika bonde.
Et le peuple prit en main de la nourriture et ses trompettes; et il envoya tous les autres hommes d'Israël dans leurs tentes, mais il garda les trois cents hommes; et le camp de Madian était au-dessous de lui dans la vallée.
9 Usiku huo huo Bwana akamwambia, “Simama! Kavamie kambi, kwa maana nitakupa ushindi juu yake.
Cette même nuit, Yahvé lui dit: « Lève-toi, descends dans le camp, car je l'ai livré entre tes mains.
10 Lakini ikiwa unaogopa kushuka, shka kwenye kambi pamoja na Purh mtumishi wako,
Mais si tu as peur de descendre, descends au camp avec Purah, ton serviteur.
11 na usikilize kile wanachosema, na ujasiri wako utaimarishwa kushambulia kambi.” Basi Gidioni akaenda pamoja na Pura mtumishi wake, mpaka chini kwa walinzi wa kambi.
Tu entendras ce qu'ils diront, et tes mains seront fortifiées pour descendre au camp. » Et il descendit avec Purah, son serviteur, jusqu'à l'extrémité des hommes armés qui étaient dans le camp.
12 Wamidiani, Waamaleki, na watu wote wa mashariki walikaa karibu na bonde, wengi kama wingu la nzige. Ngamia zao walikuwa zaidi ya mawingu; walikuwa zaidi kuliko idadi ya mchanga katika bahari.
Les Madianites et les Amalécites, et tous les fils de l'Orient, étaient couchés dans la vallée comme des sauterelles, en grand nombre; et leurs chameaux étaient innombrables, comme le sable qui est au bord de la mer, en grand nombre.
13 Gideoni alipofika huko, mtu alikuwa akimwambia mwenzake ndoto. Mtu huyo akasema, “Angalia! Niliota ndoto, na nikaona mkate wa shayiri umeanguka ndani ya kambi ya Midiani. Ukaja hemani, na kuipiga kwa nguvu sana hata ikaanguka chini ikapinduka na kulala chini. '
Lorsque Gédéon arriva, voici qu'un homme racontait un rêve à son compagnon. Il dit: « Voici, j'ai eu un songe; et voici, un gâteau de pain d'orge est tombé dans le camp de Madian, est venu jusqu'à la tente, l'a frappée de telle sorte qu'elle est tombée, et l'a retournée, de sorte que la tente est restée à plat. »
14 Mtu mwingine akasema, 'Hii si kitu kingine isipokuwa upanga wa Gideoni (mwana wa Yoashi), Mwisraeli. Mungu amempa ushindi juu ya Midiani na jeshi lake lote. '
Son compagnon répondit: « Ce n'est autre que l'épée de Gédéon, fils de Joas, homme d'Israël. Dieu a livré Madian entre ses mains, avec toute son armée. »
15 Gideoni aliposikia habari ya ile ndoto na tafsiri yake, akainama chini na kuabudu. Alirudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Simameni! Bwana ametupa ushindi juu ya jeshi la Midiani.”
Lorsque Gédéon entendit le récit du rêve et son interprétation, il se prosterna. Puis il revint dans le camp d'Israël et dit: « Levez-vous, car Yahvé a livré entre vos mains l'armée de Madian! »
16 Akawagawa watu mia tatu katika makundi matatu, na akawapa tarumbeta zote na mitungi tupu, na taa ndani ya kila mtungi.
Il divisa les trois cents hommes en trois compagnies, et il mit entre les mains de chacun d'eux des trompettes et des cruches vides, avec des torches dans les cruches.
17 Akawaambia, 'Niangalieni mimi na kufanya yale ninayoyafanya. Tazama! Ninapofika kwenye mwisho wa kambi, ni lazima mfanye kile ninachofanya.
Il leur dit: « Observez-moi, et faites de même. Voici, quand j'arriverai à l'extrémité du camp, vous ferez ce que je fais.
18 Nitakapopiga tarumbeta, mimi na wote Mlio pamoja nami, basi mtapiga tarumbeta zenu katika kila upande wa kambi nzima na kupiga kelele, “Kwa Bwana na Gideoni!”
Quand je sonnerai de la trompette, moi et tous ceux qui sont avec moi, vous sonnerez aussi des trompettes de tous les côtés de tout le camp, et vous crierez: « Pour l'Éternel et pour Gédéon ».
19 Basi Gideoni na watu mia moja waliokuwa pamoja naye walifika mwisho wa kambi, hapo mwanzoni mwa saa ya kati. Wakati Wamidiani walikuwa wakibadilisha walinzi, walipiga tarumbeta na kuvunja mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
Et Gédéon et les cent hommes qui étaient avec lui arrivèrent à l'extrémité du camp, au commencement de la veille du milieu, quand on venait de commencer la veille. Ils sonnèrent des trompettes et brisèrent les cruches qu'ils avaient à la main.
20 Vikosi vitatu vilipiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Walikuwa na taa katika mikono yao ya kushoto na tarumbeta katika mikono yao ya kulia ili kuwapiga. Walipiga kelele, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni.”
Les trois corps d'armée sonnèrent des trompettes, brisèrent les cruches, tinrent dans leur main gauche les torches et dans leur main droite les trompettes avec lesquelles ils sonnaient, et ils crièrent: « L'épée de Yahvé et de Gédéon ».
21 Kila mtu alisimama mahali pake kando ya kambi na jeshi la Midiani likakimbia. Walipiga kelele na kukimbia
Ils se tinrent chacun à sa place autour du camp, et toute l'armée accourut; ils crièrent et les mirent en fuite.
22 Walipopiga tarumbeta mia tatu, Bwana akaweka upanga wa kila mtu wa Midiani dhidi ya wenzake na dhidi ya jeshi lake lote. Jeshi likimbia mpaka Bethshita kuelekea Serera, mpaka mpaka wa Abel Mehola, karibu na Tabathi.
On sonna des trois cents trompettes, et l'Éternel mit l'épée de chacun contre son compagnon et contre toute l'armée; et l'armée s'enfuit jusqu'à Beth Shittah, vers Zérach, jusqu'à la frontière d'Abel Meholah, vers Tabbath.
23 Watu wa Israeli kutoka Naftali, Asheri, na Manase wote waliitwa nje, nao wakawafuata Midiani.
Les hommes d'Israël se rassemblèrent de Nephtali, d'Aser et de tout Manassé, et ils poursuivirent Madian.
24 Gideoni akatuma wajumbe katika nchi zote za mlima wa Efraimu, akisema, “Nenda chini dhidi ya Midiani na umiliki Mto Yordani mpaka Bethbara, ukawazuie.” Basi wanaume wote wa Efraimu walikusanyika pamoja na kuimiliki maji, mpaka Bethbara na Mto Yordani.
Gédéon envoya des messagers dans toute la montagne d'Éphraïm, en disant: « Descendez contre Madian, et prenez les eaux devant eux jusqu'à Beth Bara, jusqu'au Jourdain. » Tous les hommes d'Ephraïm se rassemblèrent donc et prirent les eaux jusqu'à Beth Bara, le Jourdain.
25 Wakawatwaa wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamwua Orebu kwenye mwamba wa Orebu, nao wakamwua Zeebu katika shinikizo la divai la Zeebu. Wakawafuata Wamidiani, wakamletea Gideoni vichwa vya Orebu na Zeebu, ng'ambo ya pili ya Yordani.
Ils prirent les deux princes de Madian, Oreb et Zeeb. Ils tuèrent Oreb au rocher d'Oreb, et ils tuèrent Zeeb au pressoir de Zeeb, pendant qu'ils poursuivaient Madian. Puis ils apportèrent les têtes d'Oreb et de Zeeb à Gédéon, de l'autre côté du Jourdain.