< Waamuzi 7 >

1 Ndipo Yerubaali (yaani Gideoni) akainuka mapema, na watu wote waliokuwa pamoja naye, wakaweka kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Midiani ilikuwa kaskazini mwao katika bonde karibu na kilima cha More.
Then Jerubbaal, who is Gideon, and all the people who were with him, rose up early, and encamped beside the spring of Harod. And the camp of Midian was on the north side of them, by the hill of Moreh, in the valley.
2 Bwana akamwambia Gideoni, Kuna askari wengi sana kwa mimi kukupa ushindi juu ya Wamidiani, ili Waisraeli wasijisifu juu yangu, wakisema, 'Nguvu zetu zimetuokoa'.
And Jehovah said to Gideon, The people who are with thee are too many for me to give the Midianites into their hand, lest Israel vaunt themselves against me, saying, My own hand has saved me.
3 Basi, tangaza masikioni mwa watu, ukisema, Yeyote anayeogopa, anayetetemeka, arudi na atoke katika mlima Gileadi. 'Basi, watu elfu ishirini na mbili wakaondoka, na elfu kumi wakabaki.
Now therefore proclaim in the ears of the people, saying, Whoever is fearful and trembling, let him return and depart from mount Gilead. And there returned of the people twenty-two thousand, and there remained ten thousand.
4 Bwana akamwambia Gideoni, 'Watu bado ni wengi sana. Wapeleke chini kwenye maji, na nitafanya idadi yao iwe ndogo kwa ajili yako. Kama nikisema, 'Huyu atakwenda pamoja nawe,' atakwenda pamoja nawe; lakini kama nikisema, 'Huyu hawezi kwenda pamoja nawe,' hatakwenda. '
And Jehovah said to Gideon, The people are yet too many. Bring them down to the water, and I will try them for thee there. And it shall be, that of whom I say to thee, This man shall go with thee, the same shall go with thee, and of whomever I say to thee, This man shall not go with thee, the same shall not go.
5 Gideoni akawapeleka watu kwenye maji; Bwana akamwambia, “Ondoa kila mtu atakayelamba maji, kama mbwa alambavyo, kutoka kwa wale wanaopiga magoti na kunywa.”
So he brought down the people to the water. And Jehovah said to Gideon, Everyone who laps of the water with his tongue, as a dog laps, him thou shall set by himself. Likewise everyone who bows down upon his knees to drink.
6 Wanaume mia tatu walilamba. Wengine wote walipiga magoti kunywa maji.
And the number of those who lapped, putting their hand to their mouth, was three hundred men, but all the rest of the people bowed down upon their knees to drink water.
7 Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa watu hawa mia tatu waliokwisha kulamba maji, nitakuokoa na kukupa ushindi juu ya Wamidiani. Acha kila mtu arudi mahali pake.”
And Jehovah said to Gideon, By the three hundred men who lapped I will save you, and deliver the Midianites into thy hand. And let all the people go every man to his place.
8 Kwa hiyo wale waliochaguliwa walichukua vifaa vyao na tarumbeta zao. Gideoni akawarudisha watu wote wa Israeli, kila mtu kwenda kwenye hema yake, lakini akawaweka watu mia tatu. Basi kambi ya Midiani ilikuwa chini yake katika bonde.
So the people took provision in their hand, and their trumpets. And he sent all the men of Israel every man to his tent, but retained the three hundred men. And the camp of Midian was beneath him in the valley.
9 Usiku huo huo Bwana akamwambia, “Simama! Kavamie kambi, kwa maana nitakupa ushindi juu yake.
And it came to pass the same night, that Jehovah said to him, Arise, get thee down into the camp, for I have delivered it into thy hand.
10 Lakini ikiwa unaogopa kushuka, shka kwenye kambi pamoja na Purh mtumishi wako,
But if thou fear to go down, go thou with Purah thy servant down to the camp.
11 na usikilize kile wanachosema, na ujasiri wako utaimarishwa kushambulia kambi.” Basi Gidioni akaenda pamoja na Pura mtumishi wake, mpaka chini kwa walinzi wa kambi.
And thou shall hear what they say, and afterward thy hands shall be strengthened to go down into the camp. Then he went down with Purah his servant to the outermost part of the armed men who were in the camp.
12 Wamidiani, Waamaleki, na watu wote wa mashariki walikaa karibu na bonde, wengi kama wingu la nzige. Ngamia zao walikuwa zaidi ya mawingu; walikuwa zaidi kuliko idadi ya mchanga katika bahari.
And the Midianites and the Amalekites and all the sons of the east lay along in the valley like locusts for multitude, and their camels were without number, as the sand which is upon the sea-shore for multitude.
13 Gideoni alipofika huko, mtu alikuwa akimwambia mwenzake ndoto. Mtu huyo akasema, “Angalia! Niliota ndoto, na nikaona mkate wa shayiri umeanguka ndani ya kambi ya Midiani. Ukaja hemani, na kuipiga kwa nguvu sana hata ikaanguka chini ikapinduka na kulala chini. '
And when Gideon came, behold, there was a man telling a dream to his fellow. And he said, Behold, I dreamed a dream. And, lo, a cake of barley bread tumbled into the camp of Midian, and came to the tent, and smote it so that it fell, and turned it upside down so that the tent lay flat.
14 Mtu mwingine akasema, 'Hii si kitu kingine isipokuwa upanga wa Gideoni (mwana wa Yoashi), Mwisraeli. Mungu amempa ushindi juu ya Midiani na jeshi lake lote. '
And his fellow answered and said, This is nothing else except the sword of Gideon the son of Joash, a man of Israel. Into his hand God has delivered Midian, and all the army.
15 Gideoni aliposikia habari ya ile ndoto na tafsiri yake, akainama chini na kuabudu. Alirudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Simameni! Bwana ametupa ushindi juu ya jeshi la Midiani.”
And it was so, when Gideon heard the telling of the dream, and the interpretation of it, that he worshiped. And he returned into the camp of Israel, and said, Arise, for Jehovah has delivered the army of Midian into your hand.
16 Akawagawa watu mia tatu katika makundi matatu, na akawapa tarumbeta zote na mitungi tupu, na taa ndani ya kila mtungi.
And he divided the three hundred men into three companies, and he put trumpets into the hands of all of them, and empty pitchers, with torches inside the pitchers.
17 Akawaambia, 'Niangalieni mimi na kufanya yale ninayoyafanya. Tazama! Ninapofika kwenye mwisho wa kambi, ni lazima mfanye kile ninachofanya.
And he said to them, Look on me, and do likewise, and, behold, when I come to the outermost part of the camp, it shall be that, as I do, so ye shall do.
18 Nitakapopiga tarumbeta, mimi na wote Mlio pamoja nami, basi mtapiga tarumbeta zenu katika kila upande wa kambi nzima na kupiga kelele, “Kwa Bwana na Gideoni!”
When I blow the trumpet, I and all who are with me, then blow ye the trumpets also on every side of all the camp, and say, For Jehovah and for Gideon.
19 Basi Gideoni na watu mia moja waliokuwa pamoja naye walifika mwisho wa kambi, hapo mwanzoni mwa saa ya kati. Wakati Wamidiani walikuwa wakibadilisha walinzi, walipiga tarumbeta na kuvunja mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
So Gideon, and the hundred men who were with him, came to the outermost part of the camp in the beginning of the middle watch when they had but newly set the watch. And they blew the trumpets, and broke in pieces the pitchers that were in their hands.
20 Vikosi vitatu vilipiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Walikuwa na taa katika mikono yao ya kushoto na tarumbeta katika mikono yao ya kulia ili kuwapiga. Walipiga kelele, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni.”
And the three companies blew the trumpets, and broke the pitchers, and held the torches in their left hands, and the trumpets in their right hands with which to blow. And they cried out, The sword of Jehovah and of Gideon.
21 Kila mtu alisimama mahali pake kando ya kambi na jeshi la Midiani likakimbia. Walipiga kelele na kukimbia
And they stood every man in his place round about the camp. And all the army ran, and they shouted, and put them to flight.
22 Walipopiga tarumbeta mia tatu, Bwana akaweka upanga wa kila mtu wa Midiani dhidi ya wenzake na dhidi ya jeshi lake lote. Jeshi likimbia mpaka Bethshita kuelekea Serera, mpaka mpaka wa Abel Mehola, karibu na Tabathi.
And they blew the three hundred trumpets, and Jehovah set every man's sword against his fellow, and against all the army. And the army fled as far as Beth-shittah toward Zererah, as far as the border of Abel-meholah, by Tabbath.
23 Watu wa Israeli kutoka Naftali, Asheri, na Manase wote waliitwa nje, nao wakawafuata Midiani.
And the men of Israel were gathered together out of Naphtali, and out of Asher, and out of all Manasseh, and pursued after Midian.
24 Gideoni akatuma wajumbe katika nchi zote za mlima wa Efraimu, akisema, “Nenda chini dhidi ya Midiani na umiliki Mto Yordani mpaka Bethbara, ukawazuie.” Basi wanaume wote wa Efraimu walikusanyika pamoja na kuimiliki maji, mpaka Bethbara na Mto Yordani.
And Gideon sent messengers throughout all the hill-country of Ephraim, saying, Come down against Midian, and take before them the waters, as far as Beth-barah, even the Jordan. So all the men of Ephraim were gathered together, and took the waters as far as Beth-barah, even the Jordan.
25 Wakawatwaa wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamwua Orebu kwenye mwamba wa Orebu, nao wakamwua Zeebu katika shinikizo la divai la Zeebu. Wakawafuata Wamidiani, wakamletea Gideoni vichwa vya Orebu na Zeebu, ng'ambo ya pili ya Yordani.
And they took the two princes of Midian, Oreb and Zeeb. And they killed Oreb at the rock of Oreb, and Zeeb they killed at the winepress of Zeeb, and pursued Midian. And they brought the heads of Oreb and Zeeb to Gideon beyond the Jordan.

< Waamuzi 7 >