< Waamuzi 6 >

1 Wana wa Israeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; naye akawatia mikononi mwa Midiani kwa miaka saba.
Les enfants d’Israël ayant de nouveau mécontenté l’Eternel, il les abandonna pendant sept ans au pouvoir des Madianites.
2 Uwezo wa Midiani uliwanyanyasa Israeli. Kwa sababu ya Midiani, watu wa Israeli walitengeneza makao wenyewe kutoka kwenye mabwawa katika milima, mapango, na ngome.
Accablés par la supériorité de Madian, les Israélites, pour y échapper, utilisèrent les creux des montagnes, les souterrains et les châteaux forts.
3 Kisha ikawa kwamba wakati wowote Waisraeli walipopanda mazao yao, Wamidiani na Waamaleki na watu kutoka mashariki waliwavamia Waisraeli.
Or, quand Israël avait fait les semailles, Madian accourait avec Amalec et les peuplades orientales, et venait l’attaquer.
4 Waliweza kutengenezajeshi lao juu ya ardhi na kuharibu mazao, mpaka njia ya Gaza. Hawakuacha chakula huko Israeli, wala kondoo wala ng'ombe wala punda.
Ils occupaient son pays, détruisaient les produits de la terre jusque vers Gaza, et ne laissaient en Israël aucune subsistance, non plus que brebis, bœufs ni ânes.
5 Kila wakati wao na mifugo yao na mahema walipokuja, walikuja kama kundi la nzige, na haikuwezekana kuhesabu watu au ngamia zao. Walivamia ardhi ili kuiharibu.
Car eux-mêmes venaient avec leurs troupeaux et leurs tentes, ils arrivaient en masse comme les sauterelles, eux et leurs chameaux étaient innombrables; et ils envahissaient le pays pour le ravager.
6 Midiani iliwadhoofisha Waisraeli sana mpaka watu wa Israeli wakamwita Bwana.
lsraël tomba ainsi dans une misère extrême par le fait de Madian, et il se plaignit à l’Eternel.
7 Watu wa Israeli walipomwomba Bwana kwa sababu ya Midiani,
Comme les enfants d’Israël se plaignaient à l’Eternel au sujet de Madian,
8 Bwana alimtuma nabii kwa wana wa Israeli. Nabii akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimekuleta kutoka Misri; Nilikutoa nje ya nyumba ya utumwa.
l’Eternel leur envoya un personnage inspiré, qui leur dit: "Ainsi a parlé l’Eternel, Dieu d’Israël: C’Est moi qui vous ai fait monter de l’Egypte, qui vous ai tirés de la maison de servitude;
9 Naliwaokoa kutoka kwenye mikono ya Wamisri, na kutoka kwenye mkono wa wote waliokuwa wakikunyanyasa. Niliwafukuza mbele yenu, na nimewapa nchi yao.
je vous ai sauvés de la main des Egyptiens et de la main de vos autres oppresseurs; j’ai chassé ces derniers devant vous et vous ai donné leur pays.
10 Niliwaambia, “Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu; Nimewaamuru msiabudu miungu ya Waamori, ambao mnaishi katika nchi yao. Lakini hamkuitii sauti yangu.”
Et je vous ai dit: "C’Est moi, I’Eternel, qui suis votre Dieu! ne révérez point les dieux des Amorréens dont vous habitez le pays!" Mais vous n’avez pas écouté ma voix…"
11 Basi malaika wa Bwana akaja na kukaa chini ya mwaloni huko Ofra, uliokuwa wa Yoashi (Mwabiyezeri), wakati Gidioni, mwana wa Yoashi, akitenganisha ngano katika sakafu, katika kikapu cha divai-kuificha toka kwa Wamidiani.
Or, un ange du Seigneur vint se placer sous un térébinthe près d’Ofra, appartenant à Joas l’Abiézrite, au moment où Gédéon, son fils, battait du froment dans le pressoir pour le mettre à l’abri des Madianites.
12 Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nanyi, mpiganaji mwenye nguvu!
L’Ange du Seigneur lui apparut et lui dit: "L’Eternel est avec toi, vaillant homme!"
13 Gideoni akamwambia, Oo, bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, kwa nini basi yote haya yanatupata? Je, yako wapi matendo yake yote mazuri ambayo baba zetu walituambia, waliposema, 'Je! si Bwana aliyetukomboa kutoka Misri?' Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia mikononi mwa Midiani. '
Et Gédéon lui répondit: "Hélas! Seigneur, si l’Eternel est avec nous, d’où vient tout ce qui nous arrive? Que sont devenus tous ses prodiges que nous ont contés nos pères, disant: N’Est-ce pas l’Eternel qui nous a fait sortir de l’Egypte? Maintenant l’Eternel nous délaisse et nous livre aux mains de Madian!"
14 Bwana akamtazama na kusema, “Nenda katika nguvu uliyo nayo tayari. Uiokoe Israeli kutoka mkononi wa Midiani. Je, sikukutuma?”
Alors l’Eternel s’adressa à lui, disant: "Va avec ce courage qui t’anime, et tu sauveras Israël de la main de Madian: c’est moi qui t’envoie."
15 Gideoni akamwambia, “Tafadhali, Bwana, nawezeje kuwaokoa Israeli? Angalia, familia yangu ni dhaifu zaidi katika Manase, na mimi si muhimu katika nyumba ya baba yangu.”
Gédéon répliqua: "De grâce, mon Dieu, par quel moyen sauverais-je Israël? Ma famille est la moindre en Manassé, et moi je suis le plus jeune dans la maison de mon père!"
16 Bwana akamwambia, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utalishinda jeshi lote la Midiani kama mtu mmoja.”
"C’Est que je serai avec toi, répondit l’Eternel, et tu battras les Madianites comme un seul homme."
17 Gideoni akamwambia, “Ikiwa unapendezwa na mimi, nipe basi ishara kwamba wewe ndio unenena nami.
"Eh bien! dit-il, si j’ai trouvé faveur à tes yeux, tu me prouveras par un signe que c’est toi-même qui me parles.
18 Tafadhali, usiondoke hapa, mpaka nitakapokuja kwako na kuleta zawadi yangu na kuiweka mbele yako.” Bwana akasema, “Nitasubiri mpaka utakaporudi.”
Ne t’éloigne pas d’ici, je te prie, que je ne sois revenu près de toi: je vais quérir mon offrande et la déposer devant toi." Il répondit: "J’Attendrai ton retour."
19 Gideoni akaenda, akaandaa mwana mbuzi, na efa moja ya unga akafanya mikate isiyotiwa chachu. Akaiweka nyama hiyo katika kikapu, na akaweka mchuzi ndani ya sufuria na kuviletea chini ya mti wa mwaloni, akavitowa.
Et Gédéon rentra, apprêta un jeune chevreau et des pains azymes d’un êpha de farine, mit la viande dans une corbeille et le bouillon dans un pot, porta le tout sous le térébinthe et le lui offrit.
20 Malaika wa Mungu akamwambia, “Chukua nyama na mikate isiyotiwa chachu, ukaweke juu ya mwamba huu, ukamwage mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
L’Ange de Dieu lui dit: "Prends la viande avec les azymes, pose-les sur ce rocher, et répands le bouillon"; ce qu’il fit.
21 Kisha malaika wa Bwana akashika ncha ya fimbo mkononi mwake. Kwa hiyo akagusa nyama na mikate isiyotiwa chachu; moto ukatoka nje ya mwamba, ukateketeza nyama na mikate isiyotiwa chachu. Kisha malaika wa Bwana akaenda, na Gideoni hakuweza kumwona tena.
Et l’ange de l’Eternel, de l’extrémité du bâton qu’il tenait à la main, toucha la viande et les azymes: soudain un feu sortit du rocher, consuma viande et azymes, et l’ange de l’Eternel disparut à ses yeux.
22 Gideoni alielewa kuwa yule alikuwa malaika wa Bwana. Gideoni akasema, “Ewe Bwana MUNGU! Kwa maana nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
Gédéon vit alors que c’était un ange, et il s’écria: "Malheur à moi, Seigneur Dieu! car c’est un ange de l’Eternel que j’ai vu face à face."
23 Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope, huwezi kufa.”
"Rassure-toi, lui dit le Seigneur, ne crains rien: tu ne mourras pas."
24 Basi Gideoni akamjengea Bwana madhabahu huko. Aliiita, “Bwana ni Amani.” Hadi leo bado iko katika Ofra ya jamaa ya Waabiezeri.
Gédéon bâtit là au Seigneur un autel, qu’il appela Adonaï Chalôm; aujourd’hui encore il subsiste dans Ofra, qui est aux Abiézrites.
25 Usiku huo, Bwana akamwambia, “Twaa ng'ombe wa baba yako, na ng'ombe wa pili wa umri wa miaka saba, ukaondoe madhabahu ya Baali, ambayo ni ya baba yako, na kukata Ashera iliyo karibu nayo.
Cette même nuit, l’Eternel lui dit: "Prends l’un des taureaux qui sont à ton père, le deuxième taureau, âgé de sept ans. Tu démoliras l’autel consacré à Baal par ton père, et tu abattras le bocage qui est auprès.
26 Jenga madhabahu kwa Bwana, Mungu wako juu ya mahali pa kukimbilia, na kuijenga njia sahihi. Toa ng'ombe ya pili kama sadaka ya kuteketezwa, ukitumia kuni kutoka Ashera uliyoikata. '
Puis tu bâtiras un autel à l’Eternel, ton Dieu, au sommet de ce rocher, sur le plateau; tu prendras le deuxième taureau, et le brûleras en holocauste, sur le bois du bocage que tu auras abattu."
27 Gideoni akachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa sababu aliogopa sana watu wa nyumba ya baba yake na watu wa mji hakufanya hivyo wakati wa mchana, alifanya hivyo usiku.
Gédéon, aidé de dix de ses serviteurs, fit ce que l’Eternel lui avait ordonné; mais comme il n’osait, à cause de sa famille et des gens de la ville, agir en plein jour, il le fit nuitamment.
28 Asubuhi wakati watu wa mji walipoamka, madhabahu ya Baali imebomolewa, na Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na ng'ombe wa pili ametolewa sadaka kwenye madhabahu iliyojengwa.
Au matin, quand les gens de la ville se levèrent, ils virent l’autel de Baal renversé, son bocage abattu, le deuxième taureau offert en holocauste sur l’autel nouveau,
29 Watu wa mji wakaambiana, “Ni nani aliyefanya jambo hili?” Walipokuwa wakiongea na wengine na kutafuta majibu, wakasema, 'Gidioni mwana wa Yoashi amefanya jambo hili.”
et ils se dirent l’un à l’autre: "Qui a fait cela?…" Ils s’informèrent, firent des recherches et on leur dit: "C’Est Gédéon, fils de Joas, qui en est l’auteur."
30 Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mtoe mtoto wako ili afe, kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali, na kwa sababu ameikata Ashera karibu nayo.”
Alors les gens de la ville dirent à Joas: "Livre ton fils pour qu’il meure, parce qu’il a démoli l’autel de Baal et abattu le bocage attenant."
31 Yoashi akawaambia wote waliompinga, “Je, ninyi mtamsihi Baali? Je, mtamuokoa? Mtu yeyote atakayemtetea, basi atauawa asubuhi hii. Ikiwa Baali ni mungu, basi atajitetea mwenyewe wakati mtu anaibomoa madhabahu yake.”
Mais Joas dit à la foule qui l’assaillait: "Est-ce à vous de venger Baal, à vous de lui venir en aide? Qui prétend le faire mérite la mort, avant même qu’il soit jour! Si Baal est Dieu, qu’il venge lui-même son injure, son autel renversé!"
32 Kwa hiyo siku hiyo wakamwita Gideoni “Yerubaali,” kwa sababu alisema, “Baali ajijitetee dhidi yake,” kwa sababu Gidioni alivunja madhabahu ya Baali.
Gédéon fut à cette occasion, surnommé Jérubbaal, c’est-à-dire que Baal s’en prenne à lui, pour avoir démoli son autel.
33 Basi Wamidiani wote, Waamaleki, na watu wa mashariki walikusanyika pamoja. Wakavuka Yordani na wakapanga katika bonde la Yezreeli.
Or, tout Madian s’était réuni avec Amalec et les peuplades orientales; ils avaient pénétré à l’intérieur et campaient dans la vallée de Jezreêl.
34 Lakini Roho wa Bwana akaja juu ya Gideoni. Gideoni akapiga tarumbeta, akawaita jamaa ya Abiezeri, ili wapate kumfuata.
Soudain une inspiration divine enveloppa Gédéon; il fit sonner du cor, et les Abiézrites se groupèrent derrière lui.
35 Aliwatuma wajumbe wote katika Manase, na wao pia, waliitwa nje kumfuata. Naye akatuma wajumbe kwa Asheri, na Zabuloni, na Naftali; nao wakaenda kumlaki.
Il envoya aussi des messagers dans tout Manassé, qui se joignit également à lui; pareillement en Aser, Zabulon, Nephtali, qui montèrent au-devant d’eux.
36 Gideoni akamwambia Mungu, “Ikiwa ungependa kunitumia kuokoa Israeli, kama ulivyosema,
Et Gédéon dit au Seigneur: "Si tu veux, par ma main, secourir Israël comme tu l’as dit,
37 tazameni, ninaweka ngozi ya samazi kwenye sakafu. Ikiwa kuna umande tu juu ya ngozi, na ni kavu duniani, basi nitajua kwamba utanitumia kuokoa Israeli, kama ulivyosema.”
eh bien! je mets cette toison sur le sol de l’aire: s’il vient de la rosée sur la toison seule et que tout le sol reste sec, je saurai que tu veux secourir par ma main Israël, comme tu l’as promis."
38 Hivi ndivyo ilivyotokea-Gideoni aliamka mapama asubuhi, akaikamua ngozi hiyo, na akatoa umande kwenye ngozi, wa kutosha kujaza bakuli kwa maji.
Et il en fut ainsi. En se levant le lendemain, Gédéon pressa la toison et, de la rosée qu’il en exprima, il eut une pleine écuelle d’eau.
39 Gideoni akamwambia Mungu, 'Usinikasirikie, nitasema tena kwa mara nyingine. Tafadhali niruhusu nijaribu tena kwa kutumia ngozi. Wakati huu uifanye kavu, na iwe na umande juu ya ardhi yote kuzunguka.
Gédéon dit au Seigneur: "Ne te mets pas en colère contre moi si je t’adresse encore une prière. Permets-moi seulement une nouvelle épreuve par cette toison: que la toison seule reste sèche, tandis que tout le sol sera couvert de rosée!"
40 Mungu alifanya kile alichoomba usiku huo. Ngozi ilikuwa kavu, na kulikuwa na umande katika ardhi yote iliyozunguka.
Dieu déféra à sa demande cette nuit même: la toison seule resta sèche, le sol d’alentour fut couvert de rosée.

< Waamuzi 6 >