< Waamuzi 5 >

1 Siku hiyo Debora na Baraka, mwana wa Abinoamu waliimba wimbo huu:
Then sang Deborah and Barak the son of Abinoam on that day, saying,
2 'Viongozi wanapoongoza mbele ya Israeli, watu wanapojitolea kupigana vita, tunamsifu Bwana!
For that the leaders took the lead in Israel, For that the people offered themselves willingly, Bless ye Jehovah.
3 Sikiliza, ninyi wafalme! Sikiliza kwa makini, ninyi viongozi! Mimi nitamwimbia Bwana; Nami nitamsifu Bwana, Mungu wa Israeli.
Hear, O ye kings; give ear, O ye princes; I, [even] I, will sing unto Jehovah; I will sing praise to Jehovah, the God of Israel.
4 Ee Bwana, wakati ulipotoka Seiri, ulipokwenda kutoka Edomu, nchi ilitetemeka, na mbingu pia ilitetemeka; pia mawingu yalitoa maji.
Jehovah, when thou wentest forth out of Seir, When thou marchedst out of the field of Edom, The earth trembled, the heavens also dropped, Yea, the clouds dropped water.
5 Milima ikatoka mbele ya uso wa Bwana; hata Mlima Sinai ukatetemeka mbele ya uso wa Bwana, Mungu wa Israeli.
The mountains quaked at the presence of Jehovah, Even yon Sinai at the presence of Jehovah, the God of Israel.
6 Katika siku za Shamgari (mwana wa Anathi), katika siku za Jael, barabara kuu ziliachwa, na wale ambao walitembea tu walitumia njia za upepo.
In the days of Shamgar the son of Anath, In the days of Jael, the highways were unoccupied, And the travellers walked through byways.
7 Kulikuwa na mashujaa wachache huko Israeli, mpaka mimi, Debora, nilipochukua amri- mama alichukua amri katika Israeli!
The rulers ceased in Israel, they ceased, Until that I Deborah arose, That I arose a mother in Israel.
8 Walichagua miungu mpya, kulikuwa na vita katika malango ya jiji lakini bado hapakuwa na ngao au mikuki iliyoonekana kati ya watu elfu arobaini nchini Israeli.
They chose new gods; Then was war in the gates: Was there a shield or spear seen Among forty thousand in Israel?
9 Moyo wangu unawaendea wakuu wa Israeli, pamoja na watu ambao walijitolea -tunambariki Bwana kwa ajili yao!
My heart is toward the governors of Israel, That offered themselves willingly among the people: Bless ye Jehovah.
10 Fikiria juu ya hili- ninyi ambao hupanda punda weupe mmeketi kwenye mazulia, nanyi mnaotembea njiani.
Tell [of it], ye that ride on white asses, Ye that sit on rich carpets, And ye that walk by the way.
11 Sikiliza sauti za wale wanaoimba kwenye maeneo ya kutekea maji. Huko wanasema tena juu ya matendo ya haki ya Bwana, na matendo ya haki ya wapiganaji wake katika Israeli. Ndipo watu wa Bwana wakashuka kwenye malango ya mji.
Far from the noise of archers, in the places of drawing water, There shall they rehearse the righteous acts of Jehovah, [Even] the righteous acts of his rule in Israel. Then the people of Jehovah went down to the gates.
12 Amka, amka, Debora! Amka, amka, imba wimbo! Simama, Baraka, na uwakamate wafungwa wako, wewe mwana wa Abinoamu.
Awake, awake, Deborah; Awake, awake, utter a song: Arise, Barak, and lead away thy captives, thou son of Abinoam.
13 Wale waliokoka wakaja chini kwa watu wenye nguvu; watu wa Bwana walikuja kwangu pamoja na mashujaa.
Then came down a remnant of the nobles [and] the people; Jehovah came down for me against the mighty.
14 Walikuja kutoka Efraimu, ambao mizizi yao iko katika Amaleki; watu wa Benyamini walikufuata. Wakuu wa Makiri walitoka, na kutoka Zebuloni wale wanaobeba fimbo ya afisa.
Out of Ephraim [came down] they whose root is in Amalek; After thee, Benjamin, among thy peoples; Out of Machir came down governors, And out of Zebulun they that handle the marshal’s staff.
15 Na wakuu wangu katika Isakari walikuwa pamoja na Debora; na Isakari alikuwa na Baraka waliingia bobdeni kwa kasi chini ya amri yake. Miongoni mwa jamaa za Reubeni kulikuwa na utafutaji mkubwa wa moyo.
And the princes of Issachar were with Deborah; As was Issachar, so was Barak; Into the valley they rushed forth at his feet. By the watercourses of Reuben There were great resolves of heart.
16 Kwa nini uliketi katikati ya moto, ukisikiliza wachungaji wakipiga filimbi yao kwa makundi yao? Na kwa jamaa za Reubeni kulikuwa na utafutaji mkubwa wa moyo.
Why sattest thou among the sheepfolds, To hear the pipings for the flocks? At the watercourses of Reuben There were great searchings of heart.
17 Gileadi alikaa upande wa pili wa Yordani; na Dani, kwa nini alizunguka juu ya meli? Asheri alibakia pwani na akaishi karibu na bandari zake.
Gilead abode beyond the Jordan: And Dan, why did he remain in ships? Asher sat still at the haven of the sea, And abode by his creeks.
18 Zabuloni lilikuwa kabila ambayo lingeweza kuhatarisha maisha yao mpaka kufikia kifo, Nafthali, pia, katika uwanja wa vita.
Zebulun was a people that jeoparded their lives unto the death, And Naphtali, upon the high places of the field.
19 Wafalme walikuja, wakapigana; wafalme wa Kanaani wakapigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido. Lakini hawakuondoa fedha kama nyara.
The kings came and fought; Then fought the kings of Canaan, In Taanach by the waters of Megiddo: They took no gain of money.
20 Nyota zilipigana kutoka mbinguni, kutoka katika njia zao za mbinguni zilipigana na Sisera
From heaven fought the stars, From their courses they fought against Sisera.
21 Mto Kishoni uliwaondoa, mto ule wa kale, Mto Kishoni. Endelea mbele nafsi yangu, jipe nguvu!
The river Kishon swept them away, That ancient river, the river Kishon. O my soul, march on with strength.
22 Kisha sauti za hofu za farasi-kupiga mbio, kupigana kwa watu wake wenye nguvu.
Then did the horsehoofs stamp By reason of the prancings, the prancings of their strong ones.
23 'Ilaani Meroz!' asema malaika wa Bwana. 'Hakika walaani wenyeji wake!' Kwa sababu hawakuja kumsaidia Bwana, kumsaidia Bwana katika vita dhidi ya mashujaa wenye nguvu.
Curse ye Meroz, said the angel of Jehovah. Curse ye bitterly the inhabitants thereof, Because they came not to the help of Jehovah, To the help of Jehovah against the mighty.
24 Yaeli amebarikiawa zaidi kuliko wanawake wengine wote, Yaeli (mke wa Heberi Mkeni), amebarikiwa zaidi kuliko wanawake wote wanaoishi katika hema.
Blessed above women shall Jael be, The wife of Heber the Kenite; Blessed shall she be above women in the tent.
25 Mtu yule aliomba maji, naye akampa maziwa; akamletea siagi katika sahani inayofaa kwa wakuu.
He asked water, [and] she gave him milk; She brought him butter in a lordly dish.
26 Aliweka mkono wake kwenye kigingi cha hema, na mkono wake wa kuia katika nyundo ya mfanyakazi; kwa nyundo akampiga Sisera, alimpiga kichwani kwake. Aliligawanya fuvu lake vipande vipande wakati alipompiga pembeni ya kichwa chake.
She put her hand to the tent-pin, And her right hand to the workmen’s hammer; And with the hammer she smote Sisera, she smote through his head; Yea, she pierced and struck through his temples.
27 Akaanguka katikati ya miguu yake, akaanguka akalala pale. Kati ya miguu yake akaanguka. Mahali alipoanguka ni pale ambapo aliuawa kwa ukatili.
At her feet he bowed, he fell, he lay; At her feet he bowed, he fell: Where he bowed, there he fell down dead.
28 Aliangalia dirishani - mama yake Sisera aliangalia kupitia kamba na akasema kwa huzuni, 'Kwa nini gari lakelimechelewa kuja? Kwa nini viboko vya farasi vinavyovuta magari yake vimechelewa? '
Through the window she looked forth, and cried, The mother of Sisera [cried] through the lattice, Why is his chariot so long in coming? Why tarry the wheels of his chariots?
29 Wafalme wake wenye hekima walijibu, na yeye mwenyewe akajibu jibu lile
Her wise ladies answered her, Yea, she returned answer to herself,
30 'Je, hawakupata na kugawanya nyara? Tumbo, matumbo mawili kwa kila mtu; nyara ya kitambaa kilichofunikwa kwa Sisera, nyara ya kitambaa kilichofunikwa, nguo mbili za rangi iliyofunikwa kwa misumari ya wale waliopora?
Have they not found, have they not divided the spoil? A damsel, two damsels to every man; To Sisera a spoil of dyed garments, A spoil of dyed garments embroidered, Of dyed garments embroidered on both sides, on the necks of the spoil?
31 Naam, adui zako wote wataangamia, Ee Bwana! Lakini marafiki zako watakuwa kama jua wakati linapoongezeka kwa uwezo wake. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.
So let all thine enemies perish, O Jehovah: But let them that love him be as the sun when he goeth forth in his might. And the land had rest forty years.

< Waamuzi 5 >