< Waamuzi 21 >

1 Sasa watu wa Israeli walikuwa wameahidi huko Mispa, “Hakuna hata mmoja wetu atakayempa binti yake kuolewa na Mbenyamini.”
Or ceux d'Israël avaient juré en Mitspa, en disant: Nul de nous ne donnera sa fille pour femme aux Benjamites.
2 Ndipo watu wakaenda Betheli, wakakaa huko mbele ya Mungu hata jioni; wakalia kwa sauti kubwa.
Puis le peuple vint à la maison du [Dieu] Fort, et ils demeurèrent là jusqu'au soir en la présence de Dieu; et ils élevèrent leurs voix, et pleurèrent amèrement,
3 Walipiga kelele, “Kwa nini, Bwana, Mungu wa Israeli, amefanya jambo hili kwa Waisraeli, kwamba moja ya makabila yetu linapotea leo?”
Et dirent: Ô Eternel, Dieu d'Israël! pourquoi ceci est-il arrivé en Israël, qu'une Tribu d'Israël ait été aujourd'hui retranchée?
4 Siku iliyofuata watu waliamka mapema na wakajenga madhabahu huko na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani.
Et le lendemain le peuple se leva de bon matin, et bâtit là un autel, et ils offrirent des holocaustes, et des sacrifices de prospérités.
5 Watu wa Israeli wakasema, “Ni nani kati ya kabila zote za Israeli hawakuja katika mkutano wa Bwana?” Kwa kuwa walikuwa wamefanya ahadi muhimu juu ya mtu yeyote ambaye hakuja kwa Bwana huko Mispa. Wakasema, “Hakika yeye atauawa.”
Alors les enfants d'Israël dirent: Qui est celui d'entre toutes les Tribus d'Israël qui n'est point monté à l'assemblée vers l'Eternel? Car on avait fait un grand serment contre tout homme qui ne monterait point vers l'Eternel à Mitspa, en disant: Un tel sera puni de mort.
6 Watu wa Israeli walikuwa na huruma kwa ndugu yao Benyamini. Wakasema, “Leo hii kabila moja limekatiliwa mbali kutoka Israeli.
Car les enfants d'Israël se repentaient de ce qui était arrivé à Benjamin leur frère, et disaient aujourd'hui une Tribu a été retranchée d'Israël.
7 Ni nani atakayewapa wale walioachwa wake, kwa kuwa tumeahidi kwa Bwana kwamba hatuwezi kuwaruhusu yeyote kati yao aoe binti zetu?”
Comment ferons-nous pour donner des femmes à ceux qui sont demeurés de reste, puisque nous avons juré par l'Eternel que nous ne leur donnerions point de nos filles pour femmes?
8 Wakasema, “Ni nani kati ya kabila za Israeli hawakuja kwa Bwana huko Mispa? Ilionekana kuwa hakuna mtu aliyekuja kwenye mkusanyiko kutoka Jabeshi-Gileadi.
Ils dirent donc: Y a-t-il quelqu'un d'entre les Tribus d'Israël qui ne soit point monté vers l'Eternel à Mitspa? Or voici, aucun homme de Jabès de Galaad n'était venu au camp, à l'assemblée.
9 Kwa maana watu walipokuwa wamepangwa kwa utaratibu, tazama, hakuna hata mmoja wa wenyeji wa Yabeshi Gileadi.
Car quand on fit le dénombrement du peuple, voici, il ne s'était trouvé aucun des habitants de Jabès de Galaad.
10 Mkutano huo uliwatuma watu kumi na wawili wa watu wao wenye ujasiri kwa maagizo ya kwenda Jabeshi-gileadi na kuwaangamiza, na kuwaua, hata wanawake na watoto.
C'est pourquoi l'assemblée y envoya douze mille hommes des plus vaillants, et leur commanda en disant: Allez, et frappez les habitants de Jabès de Galaad au tranchant de l'épée, tant les femmes que les petits enfants.
11 “Fanya hivi unapaswa kuua kila mume na kila mwanamke aliyelala na mwanaume.”
Voici donc ce que vous ferez: Vous exterminerez à la façon de l'interdit tout mâle, et toute femme qui aura eu compagnie d'homme.
12 Watu wale walikuta watu kati ya hao waliokaa Yabeshi-gileadi, wanawake mia nne ambao hawakulala na mwanaume, wakawapeleka kwenye kambi huko Shilo, huko Kanaani.
Et ils trouvèrent entre les habitants de Jabès de Galaad quatre cents filles vierges, qui n'avaient point eu compagnie d'homme; et ils les amenèrent au camp à Silo, qui est au pays de Canaan.
13 Mkutano wote ukatuma ujumbe na kuwaambia watu wa Benyamini waliokuwa kwenye mwamba wa Rimoni kwamba walikuwa wanawapa amani.
Alors toute l'assemblée envoya pour parler aux enfants de Benjamin qui étaient au rocher de Rimmon, et pour leur offrir la paix.
14 Wabenyamini walirudi wakati huo na walipewa wanawake wa Yabeshi Gileadi, lakini hapakuwa na wanawake wa kutosha kwa wote.
En ce temps-là donc les Benjamites retournèrent, et on leur donna pour femmes celles qui avaient été conservées en vie d'entre les femmes de Jabès de Galaad; mais il ne s'en trouva pas [assez pour eux].
15 Watu waliomboleza kwa kile kilichotokea Benyamini, kwa kuwa Bwana alifanya mgawanyiko kati ya makabila ya Israeli.
Et le peuple se repentit de ce qui avait été fait à Benjamin; car l'Eternel avait fait une brèche aux Tribus d'Israël.
16 Kisha wakuu wa mkutano wakasema, “Tutafanyaje ili Wabenyamini wapate wake, kwa kuwa wanawake wa Benyamini wameuawa?”
Et les Anciens de l'assemblée dirent: Comment ferons-nous pour donner des femmes à ceux qui sont demeurés de reste; car les femmes ont été exterminées d'entre les Benjamites.
17 Wakasema, 'Lazima kuwe na urithi kwa Wabenyamini waliosalia, ili kabila lisiharibiwe kutoka Israeli.
Puis ils dirent: Ceux qui sont réchappés posséderont ce qui appartenait à Benjamin, afin qu'une Tribu d'Israël ne soit point effacée.
18 Hatuwezi kuwapa wake kutoka kwa binti zetu, kwa kuwa wana wa Israeli walikuwa wametoa ahadi, 'Na alaaniwe mtu atakayempa Benyamini mke.'”
Cependant nous ne leur pourrons point donner des femmes d'entre nos filles; car les enfants d'Israël ont juré, en disant: Maudit soit celui qui donnera une femme à ceux de Benjamin.
19 Wakasema, “Mnajua kuwa kuna sikukuu kwa Bwana kila mwaka huko Shilo ( ambayo ni kaskazini ya Betheli, mashariki ya barabara inayopanda kutoka Betheli hadi Shekemu, na kusini mwa Lebona).
Et ils dirent: Voici la solennité ordinaire de l'Eternel est à Silo, qui est vers l'Aquilon de Bethel, et au soleil levant du chemin qui monte de Bethel à Sichem, et au midi de Lebona.
20 Wakawaagiza wana wa Benyamini, wakisema, “Nendeni, mjifiche kwa siri, na kusubiri katika mashamba ya mizabibu.
Et ils commandèrent aux enfants de Benjamin, en disant: Allez, et mettez des gens en embuscade aux vignes.
21 Tazama wakati ambapo wasichana kutoka Shilo watatoka kucheza, Tokeni nje ya mizabibu na kila mmoja wenu anapaswa kunyakua mke kutoka kwa wasichana wa Shilo, kisha kurudi kwenye nchi ya Benyamini.
Et quand vous verrez que les filles de Silo sortiront pour danser avec des flûtes, alors vous sortirez des vignes, et vous ravirez pour vous chacun sa femme d'entre les filles de Silo, et vous en irez au pays de Benjamin.
22 Wakati baba zao au ndugu zao watakapokuja kutupinga, tutawaambia, 'Tupeni neema! Waache wabaki kwa sababu hatukupata wake kwa kila mtu wakati wa vita. Na ninyi hamna hatia juu ya ahadi, kwa sababu hamkuwapa wao binti zenu.'”
Et quand leurs pères, ou leurs frères viendront vers nous pour plaider, nous leur dirons: Ayez pitié d'eux pour l'amour de nous, puisque nous n'avons point pris femme pour [chacun d'eux] en cette guerre, et vous serez coupables si vous ne leur en donnez point en un temps comme celui-ci.
23 Watu wa Benyamini walifanya hivyo. Walichukua idadi ya wake waliowahitaji kutoka kwa wasichana waliokuwa wakicheza, nao wakawachukua ili wawe wake zao. Wakaenda na kurudi mahali pa urithi wao; wakajenga tena miji, na wakaishi ndani yao.
Les enfants de Benjamin firent ainsi, et enlevèrent des femmes selon leur nombre, d'entre celles qui dansaient, lesquelles ils ravirent; puis s'en allant ils retournèrent à leur héritage, et rebâtirent des villes, et y habitèrent.
24 Kisha watu wa Israeli wakatoka mahali hapo na kwenda nyumbani, kila mmoja kwa kabila lake na ukoo, na kila mmoja kwa urithi wake mwenyewe.
Ainsi en ce temps-là chacun des enfants d'Israël s'en alla de là en sa Tribu, et dans sa famille, et ils se retirèrent de là chacun dans son héritage.
25 Siku hizo hapakuwa na mfalme huko Israeli. Kila mtu alifanya yaliyo sawa machoni pake mwenyewe.
En ces jours-là il n'y avait point de Roi en Israël; mais chacun faisait ce qui lui semblait être droit.

< Waamuzi 21 >