< Waamuzi 21 >
1 Sasa watu wa Israeli walikuwa wameahidi huko Mispa, “Hakuna hata mmoja wetu atakayempa binti yake kuolewa na Mbenyamini.”
Les hommes d'Israël avaient juré à Mitspa, en disant: « Aucun de nous ne donnera sa fille pour femme à Benjamin. »
2 Ndipo watu wakaenda Betheli, wakakaa huko mbele ya Mungu hata jioni; wakalia kwa sauti kubwa.
Le peuple vint à Béthel et s'assit jusqu'au soir devant Dieu; il éleva la voix et pleura abondamment.
3 Walipiga kelele, “Kwa nini, Bwana, Mungu wa Israeli, amefanya jambo hili kwa Waisraeli, kwamba moja ya makabila yetu linapotea leo?”
Ils dirent: « Yahvé, le Dieu d'Israël, pourquoi cela est-il arrivé en Israël, qu'il manque aujourd'hui une tribu en Israël? »
4 Siku iliyofuata watu waliamka mapema na wakajenga madhabahu huko na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani.
Le lendemain, le peuple se leva de bonne heure, construisit un autel à cet endroit, et offrit des holocaustes et des sacrifices de prospérité.
5 Watu wa Israeli wakasema, “Ni nani kati ya kabila zote za Israeli hawakuja katika mkutano wa Bwana?” Kwa kuwa walikuwa wamefanya ahadi muhimu juu ya mtu yeyote ambaye hakuja kwa Bwana huko Mispa. Wakasema, “Hakika yeye atauawa.”
Les enfants d'Israël dirent: « Qui est, parmi toutes les tribus d'Israël, celui qui n'est pas monté à l'assemblée vers l'Éternel? » Car ils avaient fait un grand serment au sujet de celui qui n'était pas monté vers l'Éternel à Mitspa, en disant: « Il sera certainement mis à mort. »
6 Watu wa Israeli walikuwa na huruma kwa ndugu yao Benyamini. Wakasema, “Leo hii kabila moja limekatiliwa mbali kutoka Israeli.
Les enfants d'Israël s'affligèrent pour Benjamin, leur frère, et dirent: « Il y a aujourd'hui une tribu retranchée d'Israël.
7 Ni nani atakayewapa wale walioachwa wake, kwa kuwa tumeahidi kwa Bwana kwamba hatuwezi kuwaruhusu yeyote kati yao aoe binti zetu?”
Comment fournirons-nous des femmes à ceux qui restent, puisque nous avons juré par l'Éternel de ne pas leur donner de nos filles pour femmes? »
8 Wakasema, “Ni nani kati ya kabila za Israeli hawakuja kwa Bwana huko Mispa? Ilionekana kuwa hakuna mtu aliyekuja kwenye mkusanyiko kutoka Jabeshi-Gileadi.
Ils dirent: « Quel est celui des tribus d'Israël qui n'est pas monté vers l'Éternel à Mitspa? » Voici, personne n'est venu de Jabesh Galaad au camp, pour l'assemblée.
9 Kwa maana watu walipokuwa wamepangwa kwa utaratibu, tazama, hakuna hata mmoja wa wenyeji wa Yabeshi Gileadi.
Car lorsqu'on fit le compte du peuple, voici, il n'y avait là aucun des habitants de Jabesh Galaad.
10 Mkutano huo uliwatuma watu kumi na wawili wa watu wao wenye ujasiri kwa maagizo ya kwenda Jabeshi-gileadi na kuwaangamiza, na kuwaua, hata wanawake na watoto.
L'assemblée y envoya douze mille hommes parmi les plus vaillants, et leur donna cet ordre: « Allez frapper du tranchant de l'épée les habitants de Jabesh Galaad, les femmes et les petits enfants.
11 “Fanya hivi unapaswa kuua kila mume na kila mwanamke aliyelala na mwanaume.”
Voici ce que vous ferez: vous détruirez par interdit tout mâle et toute femme qui a couché avec un homme. »
12 Watu wale walikuta watu kati ya hao waliokaa Yabeshi-gileadi, wanawake mia nne ambao hawakulala na mwanaume, wakawapeleka kwenye kambi huko Shilo, huko Kanaani.
Ils trouvèrent parmi les habitants de Jabesh Galaad quatre cents jeunes vierges qui n'avaient pas connu l'homme en couchant avec lui, et ils les amenèrent au camp à Silo, qui est au pays de Canaan.
13 Mkutano wote ukatuma ujumbe na kuwaambia watu wa Benyamini waliokuwa kwenye mwamba wa Rimoni kwamba walikuwa wanawapa amani.
Toute l'assemblée envoya parler aux fils de Benjamin qui étaient au rocher de Rimmon, et leur annonça la paix.
14 Wabenyamini walirudi wakati huo na walipewa wanawake wa Yabeshi Gileadi, lakini hapakuwa na wanawake wa kutosha kwa wote.
Benjamin revint à ce moment-là, et ils leur donnèrent les femmes qu'ils avaient sauvées vivantes parmi les femmes de Jabesh Galaad. Il n'y en avait toujours pas assez pour eux.
15 Watu waliomboleza kwa kile kilichotokea Benyamini, kwa kuwa Bwana alifanya mgawanyiko kati ya makabila ya Israeli.
Le peuple s'affligea pour Benjamin, car Yahvé avait fait une brèche dans les tribus d'Israël.
16 Kisha wakuu wa mkutano wakasema, “Tutafanyaje ili Wabenyamini wapate wake, kwa kuwa wanawake wa Benyamini wameuawa?”
Les anciens de l'assemblée dirent: « Comment pourrions-nous fournir des femmes à ceux qui restent, puisque les femmes sont détruites hors de Benjamin? »
17 Wakasema, 'Lazima kuwe na urithi kwa Wabenyamini waliosalia, ili kabila lisiharibiwe kutoka Israeli.
Ils dirent: « Il faut qu'il y ait un héritage pour ceux qui sont échappés de Benjamin, afin qu'une tribu ne soit pas effacée d'Israël.
18 Hatuwezi kuwapa wake kutoka kwa binti zetu, kwa kuwa wana wa Israeli walikuwa wametoa ahadi, 'Na alaaniwe mtu atakayempa Benyamini mke.'”
Mais nous ne pouvons pas leur donner des femmes de nos filles, car les enfants d'Israël ont juré en disant: « Maudit soit celui qui donne une femme à Benjamin. »
19 Wakasema, “Mnajua kuwa kuna sikukuu kwa Bwana kila mwaka huko Shilo ( ambayo ni kaskazini ya Betheli, mashariki ya barabara inayopanda kutoka Betheli hadi Shekemu, na kusini mwa Lebona).
Ils dirent: « Voici qu'il y a une fête de l'Éternel d'année en année à Silo, qui est au nord de Béthel, à l'est de la route qui monte de Béthel à Sichem, et au sud de Lebona. »
20 Wakawaagiza wana wa Benyamini, wakisema, “Nendeni, mjifiche kwa siri, na kusubiri katika mashamba ya mizabibu.
Ils donnèrent cet ordre aux fils de Benjamin: « Allez vous poster dans les vignes,
21 Tazama wakati ambapo wasichana kutoka Shilo watatoka kucheza, Tokeni nje ya mizabibu na kila mmoja wenu anapaswa kunyakua mke kutoka kwa wasichana wa Shilo, kisha kurudi kwenye nchi ya Benyamini.
et regardez, et voici, si les filles de Silo sortent pour danser dans les bals, sortez des vignes, prenez chacun sa femme parmi les filles de Silo, et allez au pays de Benjamin.
22 Wakati baba zao au ndugu zao watakapokuja kutupinga, tutawaambia, 'Tupeni neema! Waache wabaki kwa sababu hatukupata wake kwa kila mtu wakati wa vita. Na ninyi hamna hatia juu ya ahadi, kwa sababu hamkuwapa wao binti zenu.'”
Lorsque leurs pères ou leurs frères viendront se plaindre à nous, nous leur dirons: « Accordez-nous leur grâce, car nous n'avons pas pris pour chacun sa femme dans la bataille, et vous ne les leur avez pas données, sinon vous seriez maintenant coupables. »
23 Watu wa Benyamini walifanya hivyo. Walichukua idadi ya wake waliowahitaji kutoka kwa wasichana waliokuwa wakicheza, nao wakawachukua ili wawe wake zao. Wakaenda na kurudi mahali pa urithi wao; wakajenga tena miji, na wakaishi ndani yao.
Les fils de Benjamin firent de même et prirent des femmes selon leur nombre, de celles qui dansaient et qu'ils enlevèrent. Ils partirent et retournèrent dans leur héritage, bâtirent les villes et y habitèrent.
24 Kisha watu wa Israeli wakatoka mahali hapo na kwenda nyumbani, kila mmoja kwa kabila lake na ukoo, na kila mmoja kwa urithi wake mwenyewe.
En ce temps-là, les enfants d'Israël partirent de là, chacun dans sa tribu et dans sa famille, et ils s'en allèrent chacun dans son héritage.
25 Siku hizo hapakuwa na mfalme huko Israeli. Kila mtu alifanya yaliyo sawa machoni pake mwenyewe.
En ce temps-là, il n'y avait pas de roi en Israël. Chacun faisait ce qui était juste à ses propres yeux.