< Waamuzi 21 >
1 Sasa watu wa Israeli walikuwa wameahidi huko Mispa, “Hakuna hata mmoja wetu atakayempa binti yake kuolewa na Mbenyamini.”
And [the] man of Israel he had sworn at Mizpah saying anyone of us not he will give daughter his to Benjamin to a wife.
2 Ndipo watu wakaenda Betheli, wakakaa huko mbele ya Mungu hata jioni; wakalia kwa sauti kubwa.
And it came the people Beth-el and they sat there until the evening before God and they lifted up voice their and they wept weeping great.
3 Walipiga kelele, “Kwa nini, Bwana, Mungu wa Israeli, amefanya jambo hili kwa Waisraeli, kwamba moja ya makabila yetu linapotea leo?”
And they said why? O Yahweh [the] God of Israel has it happened (this [thing] *LA(bh)*) in Israel to be missing this day from Israel a tribe one.
4 Siku iliyofuata watu waliamka mapema na wakajenga madhabahu huko na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani.
And it was from [the] next day and they rose early the people and they built there an altar and they offered up burnt offerings and peace offerings.
5 Watu wa Israeli wakasema, “Ni nani kati ya kabila zote za Israeli hawakuja katika mkutano wa Bwana?” Kwa kuwa walikuwa wamefanya ahadi muhimu juu ya mtu yeyote ambaye hakuja kwa Bwana huko Mispa. Wakasema, “Hakika yeye atauawa.”
And they said [the] people of Israel who? [is [the] one] who not he went up in the assembly from all [the] tribes of Israel to Yahweh for the oath great it was to [the one] who not he went up to Yahweh Mizpah saying certainly he will be put to death.
6 Watu wa Israeli walikuwa na huruma kwa ndugu yao Benyamini. Wakasema, “Leo hii kabila moja limekatiliwa mbali kutoka Israeli.
And they had compassion [the] people of Israel to Benjamin brother its and they said it has been cut off this day a tribe one from Israel.
7 Ni nani atakayewapa wale walioachwa wake, kwa kuwa tumeahidi kwa Bwana kwamba hatuwezi kuwaruhusu yeyote kati yao aoe binti zetu?”
What? will we do for them for [those who] remain for wives and we we have sworn by Yahweh to not to give to them any of daughters our to wives.
8 Wakasema, “Ni nani kati ya kabila za Israeli hawakuja kwa Bwana huko Mispa? Ilionekana kuwa hakuna mtu aliyekuja kwenye mkusanyiko kutoka Jabeshi-Gileadi.
And they said who? [is the] one from [the] tribes of Israel which not it went up to Yahweh Mizpah and there! not he had come anyone to the camp from Jabesh Gilead to the assembly.
9 Kwa maana watu walipokuwa wamepangwa kwa utaratibu, tazama, hakuna hata mmoja wa wenyeji wa Yabeshi Gileadi.
And it was mustered the people and there! there not there [was] anyone from [the] inhabitants of Jabesh Gilead.
10 Mkutano huo uliwatuma watu kumi na wawili wa watu wao wenye ujasiri kwa maagizo ya kwenda Jabeshi-gileadi na kuwaangamiza, na kuwaua, hata wanawake na watoto.
And they sent there the congregation two [plus] ten thousand man from [the] sons of strength and they commanded them saying go and you will strike [the] inhabitants of Jabesh Gilead to [the] mouth of [the] sword and the women and the little one[s].
11 “Fanya hivi unapaswa kuua kila mume na kila mwanamke aliyelala na mwanaume.”
And this [is] the thing which you will do every male and every woman [who] has known lying of a male you will totally destroy.
12 Watu wale walikuta watu kati ya hao waliokaa Yabeshi-gileadi, wanawake mia nne ambao hawakulala na mwanaume, wakawapeleka kwenye kambi huko Shilo, huko Kanaani.
And they found of [the] inhabitants of - Jabesh Gilead four hundred young woman virgin[s] who not she had known a man to lying of a male and they brought them to the camp Shiloh which [is] in [the] land of Canaan.
13 Mkutano wote ukatuma ujumbe na kuwaambia watu wa Benyamini waliokuwa kwenye mwamba wa Rimoni kwamba walikuwa wanawapa amani.
And they sent all the congregation and they spoke to [the] descendants of Benjamin who [were] at [the] rock of Rimmon and they proclaimed to them peace.
14 Wabenyamini walirudi wakati huo na walipewa wanawake wa Yabeshi Gileadi, lakini hapakuwa na wanawake wa kutosha kwa wote.
And it returned Benjamin at the time that and they gave to them the women whom they had preserved alive from [the] women of Jabesh Gilead and not they found for them so.
15 Watu waliomboleza kwa kile kilichotokea Benyamini, kwa kuwa Bwana alifanya mgawanyiko kati ya makabila ya Israeli.
And the people it had compassion to Benjamin for he had made Yahweh a breach in [the] tribes of Israel.
16 Kisha wakuu wa mkutano wakasema, “Tutafanyaje ili Wabenyamini wapate wake, kwa kuwa wanawake wa Benyamini wameuawa?”
And they said [the] elders of the congregation what? will we do for [those who] remain for wives for she is destroyed from Benjamin woman.
17 Wakasema, 'Lazima kuwe na urithi kwa Wabenyamini waliosalia, ili kabila lisiharibiwe kutoka Israeli.
And they said a possession of [the] escaped remnant [belongs] to Benjamin and not it will be wiped out a tribe from Israel.
18 Hatuwezi kuwapa wake kutoka kwa binti zetu, kwa kuwa wana wa Israeli walikuwa wametoa ahadi, 'Na alaaniwe mtu atakayempa Benyamini mke.'”
And we not we are able to give to them wives any of daughters our for they had sworn [the] people of Israel saying [be] cursed [one who] gives a wife to Benjamin.
19 Wakasema, “Mnajua kuwa kuna sikukuu kwa Bwana kila mwaka huko Shilo ( ambayo ni kaskazini ya Betheli, mashariki ya barabara inayopanda kutoka Betheli hadi Shekemu, na kusini mwa Lebona).
And they said here! [the] festival of Yahweh [is] in Shiloh from days - days towards which [is] from north-ward of Beth-el [the] rising of towards the sun of [the] highway which goes up from Beth-el Shechem towards and from [the] south to Lebonah.
20 Wakawaagiza wana wa Benyamini, wakisema, “Nendeni, mjifiche kwa siri, na kusubiri katika mashamba ya mizabibu.
(And they commanded *Q(K)*) [the] descendants of Benjamin saying go and you will lie in wait in the vineyards.
21 Tazama wakati ambapo wasichana kutoka Shilo watatoka kucheza, Tokeni nje ya mizabibu na kila mmoja wenu anapaswa kunyakua mke kutoka kwa wasichana wa Shilo, kisha kurudi kwenye nchi ya Benyamini.
And you will see and there! if they will come out [the] daughters of Shiloh to dance in dances and you will go out from the vineyards and you will seize for yourselves each man wife his from [the] daughters of Shiloh and you will go [the] land of Benjamin.
22 Wakati baba zao au ndugu zao watakapokuja kutupinga, tutawaambia, 'Tupeni neema! Waache wabaki kwa sababu hatukupata wake kwa kila mtu wakati wa vita. Na ninyi hamna hatia juu ya ahadi, kwa sababu hamkuwapa wao binti zenu.'”
And it will be that they will come fathers their or brothers their (to make a complaint *Q(k)*) to us and we will say to them show favor for to us them for not we took each man wife his in the battle for not you you gave [them] to them about this time you will be guilty.
23 Watu wa Benyamini walifanya hivyo. Walichukua idadi ya wake waliowahitaji kutoka kwa wasichana waliokuwa wakicheza, nao wakawachukua ili wawe wake zao. Wakaenda na kurudi mahali pa urithi wao; wakajenga tena miji, na wakaishi ndani yao.
And they did thus [the] descendants of Benjamin and they carried off wives to number their from the dancers whom they seized and they went and they returned to inheritance their and they rebuilt the cities and they dwelt in them.
24 Kisha watu wa Israeli wakatoka mahali hapo na kwenda nyumbani, kila mmoja kwa kabila lake na ukoo, na kila mmoja kwa urithi wake mwenyewe.
And they dispersed from there [the] people of Israel at the time that each man to tribe his and to clan his and they went out from there each man to inheritance his.
25 Siku hizo hapakuwa na mfalme huko Israeli. Kila mtu alifanya yaliyo sawa machoni pake mwenyewe.
In the days those there not [was] a king in Israel each man the right in own eyes his he will do.