< Waamuzi 20 >
1 Ndipo watu wote wa Israeli wakatoka kama mtu mmoja, toka Dani mpaka Beer-sheba, pamoja na nchi ya Gileadi; nao wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
Et tous les fils d’Israël sortirent, depuis Dan jusqu’à Beër-Shéba, et le pays de Galaad; et l’assemblée se réunit comme un seul homme, vers l’Éternel, à Mitspa.
2 Viongozi wa watu wote, wa kabila zote za Israeli, wakachukua nafasi zao kwenye kusanyiko la watu wa Mungu-watu 400, 000 waendao kwa miguu, ambao walikuwa tayari kupigana na upanga.
Et les principaux de tout le peuple, toutes les tribus d’Israël, se présentèrent dans la congrégation du peuple de Dieu, 400 000 hommes de pied, tirant l’épée.
3 Basi wana wa Benyamini waliposikia kwamba watu wa Israeli walikuwa wamepanda Mispa. Wana wa Israeli wakasema, “Tuambieni ni kwa namna gani huu uovu umefanyika.”
Et les fils de Benjamin apprirent que les fils d’Israël étaient montés à Mitspa. Et les fils d’Israël dirent: Dites comment ce mal est arrivé.
4 Mlawi, mume wa mwanamke aliyeuawa, akajibu, Nilikuja Gibea katika nchi ya Benyamini, mimi na suria wangu, ili tulale.
Et le Lévite, le mari de la femme tuée, répondit et dit: J’étais venu à Guibha, qui est à Benjamin, moi et ma concubine, pour passer la nuit;
5 Wakati wa usiku, viongozi wa Gibea walinishambulia, wakizunguka nyumba na wakakusudia kuniua. Walimkamata na kumbaka suria wangu, naye akafa.
et les hommes de Guibha se levèrent contre moi, et entourèrent de nuit la maison, à cause de moi; ils avaient l’intention de me tuer, et ils ont humilié ma concubine, et elle est morte.
6 Nilimchukua suria wangu na kumkata mwili wake vipande vipande, na kuweka katika kila nchi ya urithi wa Israeli, kwa sababu wamefanya uovu huo na upumbavu katika Israeli.
Et j’ai saisi ma concubine et je l’ai coupée en morceaux, et je l’ai envoyée dans toutes les campagnes de l’héritage d’Israël; car ils ont commis une énormité et une infamie en Israël.
7 Sasa, ninyi Waisraeli wote, toeni maneno na ushauri wenu hapa.”
Voici, vous tous, fils d’Israël, délibérez, et donnez ici [votre] avis.
8 Watu wote wakaondoka pamoja kama mtu mmoja, wakasema, Hakuna hata mmoja wetu atakayeenda hemani kwake, wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
Et tout le peuple se leva comme un seul homme, disant: Aucun de nous n’ira à sa tente, et aucun de nous ne se retirera dans sa maison;
9 Lakini sasa hivi ndivyo tutakavyoifanyia Gibea tutaishambulia kama kura inavyotuongoza.
et maintenant, voici ce que nous ferons à Guibha: nous la traiterons selon ce que le sort décidera;
10 Tutachukua watu kumi katika mia moja katika makabila yote ya Israeli, na mia moja katika elfu, na elfu moja katika elfu kumi, kuwapa chakula kwa ajili ya watu hawa, ili waweze kufika Gibea katika Benyamini, watawaadhibu kwa uovu wao waliofanya katika Israeli.
et nous prendrons 10 hommes sur 100, de toutes les tribus d’Israël, et 100 sur 1 000, et 1 000 sur 10 000, qui prendront des provisions pour le peuple, afin que, à leur arrivée, on traite Guibha de Benjamin selon toute l’infamie qu’elle a commise en Israël.
11 Basi askari wote wa Israeli wakakusanyika juu ya mji, kama mtu mmoja.
Et tous les hommes d’Israël se rassemblèrent contre la ville, unis comme un seul homme.
12 Makabila ya Israeli waliwatuma watu kwa kabila lote la Benyamini, wakisema, “Uovu huu uliofanywa kati yenu ni nini?
Et les tribus d’Israël envoyèrent des hommes dans toutes les familles de Benjamin, disant: Quel est ce mal qui est arrivé au milieu de vous?
13 Kwa hiyo, tupeni watu hao waovu wa Gibea, tupate kuwaua, na hivyo tutaondoa kabisa uovu huu kutoka kwa Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakusikiliza sauti ya ndugu zao, watu wa Israeli,
Et maintenant, livrez-nous ces hommes, fils de Bélial, qui sont à Guibha, afin que nous les fassions mourir et que nous ôtions le mal du milieu d’Israël. Mais [les fils de] Benjamin ne voulurent pas écouter la voix de leurs frères, les fils d’Israël;
14 Ndipo wana wa Benyamini wakakusanyika kutoka mijini kwenda Gibea, wakajiandaa kupigana na wana wa Israeli.
et les fils de Benjamin se rassemblèrent de leurs villes à Guibha, pour sortir en guerre contre les fils d’Israël.
15 Watu wa Benyamini wakakusanya kutoka miji yao ili kupigana siku ile, askari elfu ishirini na sita waliopangwa kupigana na upanga. Walakini, kuna watu mia saba waliochaguliwa kutoka kwa wenyeji wa Gibea.
Et en ce jour-là furent dénombrés les fils de Benjamin qui vinrent de leurs villes: 26 000 hommes tirant l’épée, sans les habitants de Guibha, qui furent dénombrés: 700 hommes d’élite.
16 Miongoni mwa askari wote hawa walikuwa watu mia saba waliochaguliwa ambao walikuwa wenye shoto. Kila mmoja wao angeweza kupiga unywele kwa mawe na asikose.
De tout ce peuple, il y avait 700 hommes d’élite qui étaient gauchers; tous ceux-là lançaient avec la fronde une pierre contre un cheveu, et ne manquaient pas.
17 Watu wa Israeli, bila kuhesabu namba kutoka kwa Benyamini, walikuwa na watu 400, 000 waliokuwa wamejifunza kupigana na upanga. Wote hawa walikuwa watu wa vita.
Et les hommes d’Israël furent dénombrés, sauf Benjamin: 400 000 hommes tirant l’épée, tous gens de guerre.
18 Watu wa Israeli waliondoka, wakaenda Betheli, wakaomba ushauri kutoka kwa Mungu. Wakauliza, “Ni nani kwanza atakayewaangamiza watu wa Benyamini kwa ajili yetu?” Bwana akasema, “Yuda atashambulia kwanza.”
Et les fils d’Israël se levèrent, et montèrent à Béthel, et interrogèrent Dieu, et dirent: Qui de nous montera le premier pour livrer bataille aux fils de Benjamin? Et l’Éternel dit: Juda, le premier.
19 Watu wa Israeli waliamka asubuhi na wakahamisha kambi yao karibu na Gibea.
Et les fils d’Israël se levèrent le matin, et campèrent contre Guibha.
20 Watu wa Israeli walikwenda kupigana na Benyamini. Wakaweka nafasi zao za vita dhidi yao huko Gibea.
Et les hommes d’Israël sortirent en guerre contre Benjamin, et les hommes d’Israël se rangèrent en bataille contre eux devant Guibha.
21 Watu wa Benyamini wakatoka Gibea, nao wakawaua watu elfu ishirini na mbili wa jeshi la Israeli siku ile.
Et les fils de Benjamin sortirent de Guibha; et en ce jour-là ils étendirent morts par terre 22 000 hommes de ceux d’Israël.
22 Wana wa Israeli walijitia nguvu wenyewe, na wakaunda mstari wa vita mahali pale walipokwisha kuchukua nafasi siku ya kwanza.
Et le peuple, les hommes d’Israël, se fortifièrent, et se rangèrent de nouveau en bataille dans le lieu où ils s’étaient rangés le premier jour.
23 Na wana wa Israeli wakaenda, wakalia mbele za Bwana hata jioni. Walitaka mwongozo kutoka kwa Bwana “Je, tunapaswa kwenda tena kupigana na ndugu zetu, watu wa Benyamini?” Naye Bwana akasema, “Wapigeni!”
Et les fils d’Israël montèrent, et ils pleurèrent devant l’Éternel jusqu’au soir, et ils interrogèrent l’Éternel, disant: M’approcherai-je de nouveau pour livrer bataille aux fils de Benjamin, mon frère? Et l’Éternel dit: Montez contre lui.
24 Basi watu wa Israeli wakapigana na askari wa Benyamini siku ya pili.
Et les fils d’Israël s’avancèrent contre les fils de Benjamin, le second jour;
25 Siku ya pili, Benyamini alitoka kupigana nao kutoka Gibea, nao wakawaua watu wa Israeli elfu kumi na nane. Wote walikuwa watu ambao walijifunza kupigana na upanga.
et Benjamin sortit contre eux de Guibha, le second jour; et de nouveau ils étendirent morts par terre 18 000 hommes des fils d’Israël, tous tirant l’épée.
26 Basi askari wote wa Israeli na watu wote wakaenda Betheli, wakalia, wakakaa mbele za Bwana; nao wakafunga siku hiyo hata jioni, wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
Et tous les fils d’Israël et tout le peuple montèrent et vinrent à Béthel, et pleurèrent et demeurèrent là devant l’Éternel, et jeûnèrent ce jour-là jusqu’au soir; et ils offrirent des holocaustes et des sacrifices de prospérités devant l’Éternel.
27 Wana wa Israeli wakamwomba Bwana, - kwa sababu ya sanduku la agano la Mungu lilikuwapo siku hizo;
Et les fils d’Israël interrogèrent l’Éternel (et l’arche de l’alliance de Dieu était là, en ces jours;
28 na Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni, aliyekuwa akihudumia mbele ya sanduku siku hizo. “Je twende vitani tena dhidi ya watu wa Benyamini, ndugu zetu, au tuache?” Bwana akasema, “Wapigeni, kwa maana kesho nitawasaidia kuwashinda.
et Phinées, fils d’Éléazar, fils d’Aaron, se tenait devant elle, en ces jours), et ils dirent: Sortirai-je encore de nouveau pour livrer bataille aux fils de Benjamin, mon frère, ou cesserai-je? Et l’Éternel dit: Montez; car demain je les livrerai en ta main.
29 Basi Israeli akaweka watu mahali pa siri karibu na Gibea.
Et Israël plaça des embuscades contre Guibha, tout autour.
30 Watu wa Israeli wakapigana na wana wa Benyamini kwa siku ya tatu, nao wakajenga vita vyao juu ya Gibea, kama walivyotangulia.
Et les fils d’Israël montèrent, le troisième jour, contre les fils de Benjamin; et ils se rangèrent contre Guibha, comme les autres fois.
31 Watu wa Benyamini wakaenda kupigana na watu, nao wakachukuliwa mbali na mji. Walianza kuua baadhi ya watu. Kulikuwa na watu thelathini wa Israeli ambao walikufa katika mashamba na barabara. Njia moja ilienda Betheli, na nyingine ikaenda Gibea.
Et les fils de Benjamin sortirent à la rencontre du peuple; ils furent attirés loin de la ville, et commencèrent à frapper quelques-uns du peuple, qui furent tués comme les autres fois, environ 30 hommes d’Israël, sur les routes, dont l’une monte à Béthel, et l’autre à Guibha, par la campagne.
32 Ndipo wana wa Benyamini wakasema, “Wameshindwa na wanatukimbia, kama hapo awali.” Lakini askari wa Israeli wakasema, “Hebu tukimbie na kuwavuta mbali na mji hadi barabarani.”
Et les fils de Benjamin dirent: Ils sont battus devant nous comme la première fois. Et les fils d’Israël dirent: Fuyons, et nous les attirerons loin de la ville, sur les routes.
33 Watu wote wa Israeli waliondoka kutoka mahali pao na wakajipanga kwa vita huko Baal-Tamari. Basi askari wa Israeli waliokuwa wakijificha mahali pa siri walikimbia kutoka Maare-Geba.
Et tous les hommes d’Israël se levèrent de leur lieu, et se rangèrent à Baal-Thamar; et l’embuscade d’Israël s’élança de son lieu, de la prairie de Guibha.
34 Wakatoka juu ya Gibea watu kumi elfu waliochaguliwa kutoka Israeli yote, na vita vilikuwa kali, lakini Wabenjamini hawakujua kwamba msiba ulikuwa karibu nao.
Et 10 000 hommes d’élite de tout Israël vinrent contre Guibha, et la bataille fut rude; et ceux [de Benjamin] ne savaient pas que le mal les atteignait.
35 Bwana akamshinda Benyamini mbele ya Israeli. Siku hiyo, askari wa Israeli waliwauawa watu wa Benyamini 25, 100. Wote hawa waliokufa walikuwa wale waliokuwa wamejifunza kupigana na upanga.
Et l’Éternel battit Benjamin devant Israël, et les fils d’Israël étendirent morts en ce jour-là 25 100 hommes de Benjamin, tous tirant l’épée.
36 Basi askari wa Benyamini waliona wameshindwa. Wana wa Israeli walikuwa wametoa ardhi kwa Benyamini, kwa kuwa walikuwa wakihesabu watu waliowaweka katika nafasi zilizofichwa nje ya Gibea.
Et les fils de Benjamin virent qu’ils étaient battus. – Or les hommes d’Israël firent place à ceux de Benjamin, car ils se confiaient en l’embuscade qu’ils avaient placée contre Guibha.
37 Ndipo watu waliokuwa wameficha wakainuka na haraka na wakamkimbia Gibea. Nao wakauawa kila mtu aliyeishi mjini kwa upanga wao.
Et l’embuscade se hâta, et se jeta sur Guibha; et l’embuscade se porta en avant, et frappa toute la ville par le tranchant de l’épée.
38 Ishara iliyopangwa kati ya askari wa Israeli na watu waliojificha kwa siri itakuwa wingu kubwa la moshi litatokea nje ya mji.
Et le signal convenu entre les hommes d’Israël et l’embuscade était qu’ils fassent monter de la ville une épaisse colonne de fumée.
39 Ishara ilipokuja askari wa Israeli wakageuka kutoka kwenye vita. Basi Benyamini wakaanza kushambulia na wakawaua watu wa Israeli thelathini, wakasema, “Hakika wanapigwa mbele yetu, kama katika vita vya kwanza.”
Et les hommes d’Israël avaient tourné visage dans la bataille, et Benjamin avait commencé de frapper à mort une trentaine d’hommes parmi les hommes d’Israël, car ils disaient: Certainement il est complètement battu devant nous comme dans la première bataille.
40 Lakini wakati nguzo ya moshi ilipoanza kuinuka nje ya mji, Wabenjamini waligeuka na kuona moshi ukitanda mbinguni kutoka mji mzima.
Et quand l’incendie commença à monter de la ville comme une colonne de fumée, Benjamin se tourna en arrière, et voici, toute la ville montait [en fumée] vers les cieux.
41 Ndipo watu wa Israeli wakawageuka. Wana wa Benyamini waliogopa, kwa sababu waliona kwamba maafa yaliwajia.
Et les hommes d’Israël tournèrent visage: et les hommes de Benjamin furent épouvantés; car ils virent que le mal les avait atteints.
42 Basi wakakimbia kutoka kwa wana wa Israeli, kuelekea njia ya jangwani. Lakini vita viliwapata. Askari wa Israeli walitoka mijini na wakawaua pale waliposimama.
Et ils tournèrent le dos devant les hommes d’Israël, vers le chemin du désert, et la bataille les serra de près. Et ceux qui sortirent des villes les détruisirent au milieu d’eux.
43 Waliwalzungukia wana wa Benjamini na wakawafuata. Nao wakawakanyaga huko Noha, wakawaua mpaka upande wa mashariki wa Gibea.
Ils environnèrent Benjamin, le poursuivirent, le foulèrent aux pieds là où il voulait se reposer, jusque vis-à-vis de Guibha, vers le soleil levant.
44 Kutoka kabila la Benyamini, watu kumi na nane elfu walikufa, wote walikuwa wanaume waliojulikana katika vita.
Et il tomba de Benjamin 18 000 hommes, tous hommes vaillants.
45 Wakageuka na kukimbia kuelekea jangwani hadi mwamba wa Rimoni. Waisraeli waliuawa zaidi ya elfu tano kati yao barabarani. Waliendelea kuwafuata, wakifuata kwa njia kuu kwenda Gidomu, na huko waliuawa elfu mbili zaidi.
Et ils tournèrent le dos, et s’enfuirent au désert, vers le rocher de Rimmon; et [les Israélites] en grappillèrent sur les routes 5 000 hommes, et ils les serrèrent de près en les poursuivant jusqu’à Guidhom, et en frappèrent 2 000 hommes.
46 Askari wote wa Benyamini walioshuka siku hiyo walikuwa watu ishirini na tano waliokuwa wamejifunza kupigana kwa upanga; wote walikuwa wanajulikana katika vita.
Et tous ceux de Benjamin qui tombèrent en ce jour-là, furent 25 000 hommes tirant l’épée, tous hommes vaillants.
47 Lakini watu mia sita wakageuka na kukimbilia jangwani, kuelekea mwamba wa Rimoni. Wakakaa katika mwamba wa Rimoni kwa muda wa miezi minne.
Et 600 hommes tournèrent le dos et s’enfuirent au désert, vers le rocher de Rimmon, et ils demeurèrent au rocher de Rimmon quatre mois.
48 Askari wa Israeli waliwarudia watu wa Benyamini na wakawashinda na kuwaua-mji mzima, ng'ombe, na kila kitu walichopata. Pia walichoma moto kila mji katika njia yao.
Et les hommes d’Israël retournèrent vers les fils de Benjamin et les frappèrent par le tranchant de l’épée, et les hommes de chaque ville, et les bêtes, et tout ce qui fut trouvé; même toutes les villes qu’ils rencontrèrent, ils les livrèrent au feu.