< Waamuzi 2 >
1 Malaika wa Bwana akatoka Gilgali, akaenda Bokimu, akasema, “Nimekuleta kutoka Misri, na nimekuleta katika nchi niliyoapa kuwapa baba zako.
En ce temps-là, un ange du Seigneur vint de Galgala vers le Champ des Pleurs, vers Béthel et vers la maison de Joseph, à qui il dit: Voici ce que dit le Seigneur: Je vous ai fait sortir d'Egypte, je vous ai conduits en la terre que j'ai promise à vos pères, et j'ai dit: Je ne romprai pas l'alliance perpétuelle que j'ai faite avec vous.
2 Nikasema, 'Sitakuvunja kamwe agano langu na wewe. Usifanye agano na wale wanaoishi katika nchi hii. Ziangushe madhabahu zao. Lakini hukusikiliza sauti yangu. Je! ni nini hiki ulichokifanya?
Et vous, vous ne ferez point alliance avec les peuples de cette terre, vous n'adorerez point leurs dieux, mais vous en briserez les images, et vous démolirez leurs autels. Or, vous avez été indociles à ma voix: car vous avez fait ce qui vous était défendu.
3 Basi sasa nasema, “Sitawafukuza Wakanaani mbele yenu, nao watakuwa miiba kwenu, na miungu yao itakuwa mtego kwa ajili yenu.”
Et j'ai dit: Je n'exterminerai point ces peuples devant votre face, et ils seront pour vous un sujet d'angoisse, et leurs dieux vous seront un objet de scandale.
4 Malaika wa Bwana alipowaambia maneno hayo kwa watu wote wa Israeli, watu wakapiga kelele na kulia.
Lorsque l'ange du Seigneur eut dit ces paroles à tous les fils d'Israël, le peuple éleva la voix et pleura.
5 Waliita mahali hapo Bokimu. Hapo wakatoa dhabihu kwa Bwana.
Ils donnèrent à ce lieu le nom de Champ des Pleurs, et ils y sacrifièrent au Seigneur Dieu.
6 Yoshua alipowaruhusu watu waende zao, wana wa Israeli kila mmoja akaenda mahali alipopewa, wakiwa na umiliki wa ardhi yao.
Or, lorsque Josué avait congédié le peuple, chacun était allé prendre possession de son héritage.
7 Watu walimtumikia Bwana wakati wa maisha ya Yoshua na wazee walioendelea baada yake, ni wale waliokuwa wameona matendo yote makuu ya Bwana aliyoyafanya kwa Israeli.
Et le peuple avait servi le Seigneur durant tous les jours de Josué et durant tous les jours des anciens, dont la vie s'était prolongée avec la sienne, et qui avaient vu toutes les œuvres du Seigneur en faveur d'Israël
8 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, alikufa akiwa na umri wa miaka 110.
Et Josué, fils de Nau, serviteur de Dieu, était mort âgé de cent dix ans.
9 Wakamzika ndani ya mpaka wa nchi aliyopewa huko Timnath Heresi, katika mlima wa Efraimu, kaskazini mwa Mlima Gaash.
Et on l'avait enseveli sur les limites de son héritage en Thamnatharès, dans les montagnes d'Ephraïm au nord des montagnes de Gaas,
10 Kizazi hicho chote kilikusanyika kwa baba zao. Kizazi kingine kilichofuata baada yao ambao hakikumjua Bwana au kile alichokifanya kwa Israeli.
Toute cette génération s'était réunie à ses pères; et il s'éleva après elle une autre génération qui ne connaissait point le Seigneur, ni les œuvres du Seigneur en faveur d'Israël.
11 Watu wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.
Les fils d'Israël alors firent le mal devant le Seigneur, et ils servirent les Baal.
12 Wakaondoka kwa Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa kutoka Misri. Wakaifuata miungu mingine, miungu ya watu waliokuwa karibu nao, nao wakaisujudia. Wakamkasirisha BWANA kwa sababu
Ils abandonnèrent le Seigneur Dieu de leurs pères qui les avait fait sortir de l'Egypte, et ils suivirent d'autres dieux parmi les dieux des nations qui les entouraient; ils les adorèrent, et ils excitèrent le courroux du Seigneur.
13 waliondoka kwa Bwana na kumwabudu Baal na Maashtoreti.
Ils l'abandonnèrent, et ils servirent Baal et les Astartés.
14 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawapa washambuliaji walioiba mali zao kutoka kwao. Aliwauza kama watumwa waliofanyika kwa nguvu za maadui zao waliowazunguka, hivyo hawakuweza kujikinga dhidi ya adui zao.
Alors le Seigneur fut courroucé contre Israël; il les livra aux mains de pillards qui les dépouillèrent; il les fit retomber entre les mains de leurs ennemis tout alentour, et ils ne purent résister devant leurs ennemis,
15 Israeli walipokwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi yao kuwashinda, kama alivyowaapia. Na walikuwa katika shida kali.
De quelque côté qu'ils marchassent. Et la main du Seigneur était sur eux pour leur mal, comme l'avait dit le Seigneur Dieu, comme il le leur avait jurés, et il les affligea beaucoup.
16 Ndipo Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa katika mikono ya wale waliokuwa wakiba mali zao.
Ensuite, le Seigneur suscita des juges, et le Seigneur sauva le peuple des mains de ceux qui en faisaient leur proie.
17 Hata hivyo hawakuwasikiliza waamuzi wao. Hawakuwa waaminifu kwa Bwana na wakajitoa wenyewe kama makahaba kwa miungu mingine na kuabudu. Waligeuka upesi na kuiacha njia waliyoishi baba zao-wale waliotii amri za Bwana-lakini wao wenyewe hawakufanya hivyo.
Et le peuple n'obéit pas aux juges, parce qu'il s'était prostituée à la suite des dieux étrangers, et qu'il les avait adorés; il dévia rapidement des voies ou avaient marché ses pères; il cessa d'écouter comme eux la parole du Seigneur.
18 Bwana aliinua waamuzi kwa ajili yao, Bwana akawasaidia waamuzi na kuwakomboa kutoka kwa mikono ya adui zao siku zote muamuzi aliishi. Bwana aliwahurumia walipougua kwa sababu ya wale waliowadhulumu na kuwasumbua.
Et lorsque le Seigneur avait suscité des juges pour les fils d'Israël, et que le Seigneur était avec le juge, il les sauvait des mains de leurs ennemis, durant tous les jours du juge, parce que le Seigneur était ému de leurs gémissements devant ceux qui les assiégeaient et les affligeaient.
19 Lakini mwamuzi alipokufa, waligeuka na kufanya mambo ambayo yalikuwa mabaya zaidi kuliko baba zao walivyofanya. Wakaenda kuifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao yote mabaya au njia zao za ukaidi.
Mais, lorsque le juge était mort, ils changeaient et retombaient dans une corruption plus grande que celle de leurs pères, en suivant d'autres dieux, en les servant et en les adorant. Ils ne pouvaient alors renoncer à leurs habitudes ni à leurs voies d'endurcissement.
20 Hasira ya Bwana iliwaka juu ya Israeli; akasema, Kwa sababu taifa hili limevunja masharti ya agano langu ambalo nililiweka kwa ajili ya baba zao-kwa sababu hawakuisikiliza sauti yangu.
Le Seigneur se courrouça donc contre Israël, et il dit: Pour punir ce peuple d'avoir abandonné l'alliance que j'avais faite avec ses pères, et de n'avoir pas écouté ma parole,
21 Tangu sasa sitaliondoa mbele yao taifa lolote aliloliacha Yoshua baada ya kufa.
Je ne ferai plus périr un seul homme de ceux qu'a laissés en cette terre Josué, fils de Nau, et qu'a laissés le Seigneur,
22 Nitafanya hivi ili kuwajaribu Israeli, ikiwa watafuata njia ya Bwana au sivyo, kama vile baba zao walivyoifuata.
Pour éprouver par eux Israël, et voir s'il persévèrerait ou non dans la voie du Seigneur qu'avaient suivie leurs pères.
23 Ndiyo sababu Bwana aliwaacha mataifa hayo, wala hakuwafukuza haraka na kuwatia mikononi mwa Yoshua.
Et le Seigneur permettra encore que les nations qu'il n'a pas livrées aux mains de Josué, ne soient point exterminées rapidement.