< Waamuzi 2 >

1 Malaika wa Bwana akatoka Gilgali, akaenda Bokimu, akasema, “Nimekuleta kutoka Misri, na nimekuleta katika nchi niliyoapa kuwapa baba zako.
And the Messenger of YHWH goes up from Gilgal to Bochim,
2 Nikasema, 'Sitakuvunja kamwe agano langu na wewe. Usifanye agano na wale wanaoishi katika nchi hii. Ziangushe madhabahu zao. Lakini hukusikiliza sauti yangu. Je! ni nini hiki ulichokifanya?
and says, “I cause you to come up out of Egypt, and bring you into the land which I have sworn to your fathers, and say, I do not break My covenant with you for all time; and you make no covenant with the inhabitants of this land—you break down their altars; and you have not listened to My voice—what [is] this you have done?
3 Basi sasa nasema, “Sitawafukuza Wakanaani mbele yenu, nao watakuwa miiba kwenu, na miungu yao itakuwa mtego kwa ajili yenu.”
And I have also said, I do not cast them out from your presence, and they have been for adversaries to you, and their gods are for a snare to you.”
4 Malaika wa Bwana alipowaambia maneno hayo kwa watu wote wa Israeli, watu wakapiga kelele na kulia.
And it comes to pass, when the Messenger of YHWH speaks these words to all the sons of Israel, that the people lift up their voice and weep,
5 Waliita mahali hapo Bokimu. Hapo wakatoa dhabihu kwa Bwana.
and they call the name of that place Bochim, and sacrifice to YHWH there.
6 Yoshua alipowaruhusu watu waende zao, wana wa Israeli kila mmoja akaenda mahali alipopewa, wakiwa na umiliki wa ardhi yao.
And Joshua sends the people away, and the sons of Israel go, each to his inheritance, to possess the land;
7 Watu walimtumikia Bwana wakati wa maisha ya Yoshua na wazee walioendelea baada yake, ni wale waliokuwa wameona matendo yote makuu ya Bwana aliyoyafanya kwa Israeli.
and the people serve YHWH all [the] days of Joshua, and all [the] days of [the] elderly who prolonged days after Joshua, who saw all the great work of YHWH which He did to Israel.
8 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, alikufa akiwa na umri wa miaka 110.
And Joshua son of Nun, servant of YHWH, dies, a son of one hundred and ten years,
9 Wakamzika ndani ya mpaka wa nchi aliyopewa huko Timnath Heresi, katika mlima wa Efraimu, kaskazini mwa Mlima Gaash.
and they bury him in the border of his inheritance, in Timnath-Heres, in the hill-country of Ephraim, on the north of Mount Gaash;
10 Kizazi hicho chote kilikusanyika kwa baba zao. Kizazi kingine kilichofuata baada yao ambao hakikumjua Bwana au kile alichokifanya kwa Israeli.
and all that generation have also been gathered to their fathers, and another generation rises after them who have not known YHWH, and even the work which He has done to Israel.
11 Watu wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.
And the sons of Israel do evil in the eyes of YHWH, and serve the Ba‘alim,
12 Wakaondoka kwa Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa kutoka Misri. Wakaifuata miungu mingine, miungu ya watu waliokuwa karibu nao, nao wakaisujudia. Wakamkasirisha BWANA kwa sababu
and forsake YHWH, God of their fathers, who brings them out from the land of Egypt, and go after other gods (of the gods of the peoples who [are] around them), and bow themselves to them, and provoke YHWH,
13 waliondoka kwa Bwana na kumwabudu Baal na Maashtoreti.
indeed, they forsake YHWH, and do service to Ba‘al and to Ashtaroth.
14 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawapa washambuliaji walioiba mali zao kutoka kwao. Aliwauza kama watumwa waliofanyika kwa nguvu za maadui zao waliowazunguka, hivyo hawakuweza kujikinga dhidi ya adui zao.
And the anger of YHWH burns against Israel, and He gives them into the hand of spoilers, and they spoil them, and He sells them into the hand of their surrounding enemies, and they have not been able to stand before their enemies anymore;
15 Israeli walipokwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi yao kuwashinda, kama alivyowaapia. Na walikuwa katika shida kali.
in every [place] where they have gone out, the hand of YHWH has been against them for calamity, as YHWH has spoken, and as YHWH has sworn to them, and they are greatly distressed.
16 Ndipo Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa katika mikono ya wale waliokuwa wakiba mali zao.
And YHWH raises up judges, and they save them from the hand of their spoilers;
17 Hata hivyo hawakuwasikiliza waamuzi wao. Hawakuwa waaminifu kwa Bwana na wakajitoa wenyewe kama makahaba kwa miungu mingine na kuabudu. Waligeuka upesi na kuiacha njia waliyoishi baba zao-wale waliotii amri za Bwana-lakini wao wenyewe hawakufanya hivyo.
and they have also not listened to their judges, but have gone whoring after other gods, and bow themselves to them; they have turned aside [with] haste out of the way [in] which their fathers walked to obey the commands of YHWH—they have not done so.
18 Bwana aliinua waamuzi kwa ajili yao, Bwana akawasaidia waamuzi na kuwakomboa kutoka kwa mikono ya adui zao siku zote muamuzi aliishi. Bwana aliwahurumia walipougua kwa sababu ya wale waliowadhulumu na kuwasumbua.
And when YHWH raised up judges for them—then YHWH was with the judge, and saved them out of the hand of their enemies all [the] days of the judge; for YHWH sighs, because of their groaning from the presence of their oppressors, and of those thrusting them away.
19 Lakini mwamuzi alipokufa, waligeuka na kufanya mambo ambayo yalikuwa mabaya zaidi kuliko baba zao walivyofanya. Wakaenda kuifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao yote mabaya au njia zao za ukaidi.
And it has come to pass, when the judge dies—they turn back and have done corruptly above their fathers, to go after other gods, to serve them, and to bow themselves to them; they have not fallen from their doings, and from their stiff way.
20 Hasira ya Bwana iliwaka juu ya Israeli; akasema, Kwa sababu taifa hili limevunja masharti ya agano langu ambalo nililiweka kwa ajili ya baba zao-kwa sababu hawakuisikiliza sauti yangu.
And the anger of YHWH burns against Israel, and He says, “Because that this nation has transgressed My covenant which I commanded their fathers, and have not listened to My voice—
21 Tangu sasa sitaliondoa mbele yao taifa lolote aliloliacha Yoshua baada ya kufa.
I also do not continue to dispossess any from before them of the nations which Joshua has left when he dies,
22 Nitafanya hivi ili kuwajaribu Israeli, ikiwa watafuata njia ya Bwana au sivyo, kama vile baba zao walivyoifuata.
in order to try Israel by them, whether they are keeping the way of YHWH, to go in it, as their fathers kept [it], or not.”
23 Ndiyo sababu Bwana aliwaacha mataifa hayo, wala hakuwafukuza haraka na kuwatia mikononi mwa Yoshua.
And YHWH leaves these nations, so as not to dispossess them quickly, and did not give them into the hand of Joshua.

< Waamuzi 2 >