< Waamuzi 18 >

1 Siku hizo hapakuwa na mfalme huko Israeli. Kabila la Wadani lilikuwa linatafuta makazi ya kuishi, kwa maana mpaka siku hiyo hawakupokea urithi wowote kutoka miongoni mwa makabila ya Israeli.
In those dayes there was no King in Israel, and at the same time the tribe of Dan sought them an inheritance to dwell in: for vnto that time all their inheritance had not fallen vnto them among the tribes of Israel.
2 Watu wa Dani walituma watu watano kutoka kwa idadi yote ya kabila lao, wanaume wenye ujasiri kutoka Sora na kutoka Eshtaoi, ili kukagua ardhi kwa miguu, na kuiangalia. Wakawaambia, “Nendeni mkaangalie nchi.' Wakafika nchi ya mlima wa Efraimu, kwa nyumba ya Mika wakalala huko.
Therefore the children of Dan sent of their familie, fiue men out of their coastes, euen men expert in warre, out of Zorah and Eshtaol, to viewe the lande and search it out, and saide vnto them, Goe, and search out the lande. Then they came to mount Ephraim to the house of Michah and lodged there.
3 Walipokuwa karibu na nyumba ya Mika, walitambua maneno ya Mlawi. Basi wakamsimama na kumwuliza, “Nani alikuleta hapa? Unafanya nini hapa? Kwa nini uko hapa?”
When they were in the house of Michah, they knewe the voyce of the yong man the Leuite: and being turned in thither, they saide vnto him, Who brought thee hither? or what makest thou in this place? and what hast thou to doe here?
4 Akawaambia, “Hivi ndivyo Mika amefanya kwa ajili yangu Yeye aliniajiri mimi kuwa kahani wake.”
And he answered them, Thus and thus dealeth Michah with me, and hath hired me, and I am his Priest.
5 Wakamwambia, “Tafadhali tafuta ushauri kwa Mungu, ili tuweze kujua kama safari tunayoendea itafanikiwa.”
Againe they said vnto him, Aske counsell nowe of God, that we may knowe whether the way which we goe, shalbe prosperous.
6 Kuhani huyo akawaambia, “Nenda kwa amani. Bwana atakuongoza katika njia unayoiendea.”
And the Priest sayde vnto them, Goe in peace: for the Lord guideth your way which ye goe.
7 Kisha wale watu watano wakaondoka na wakafika Laishia, na waliona watu waliokuwa pale waliishi salama- vivyo hivyo Wasidoni waliishi bila kusumbuliwa na kwa usalama. Hapakuwa na mtu aliyewashinda katika nchi hiyo, au aliyewasumbua kwa namna yoyote. Waliishi mbali na Wasidoni, na hawakuwa na ushirikiano na mtu yeyote.
Then the fiue men departed and came to Laish, and sawe the people that were therein, which dwelt carelesse, after the maner of the Zidonians, quiet and sure, because no man made any trouble in the lande, or vsurped any dominion: also they were farre from the Zidonians, and had no businesse with other men.
8 Walirudi kwa kabila lao huko Zora na Eshtaol. Ndugu zao waliwauliza, 'Mna habari gani?'
So they came againe vnto their brethren to Zorah and Eshtaol: and their brethren saide vnto them, What haue ye done?
9 Wakasema, “Njoo! Hebu tuwashambulie! Tumeona ardhi na ni nzuri sana. Je hamfanyi kitu? Msiwe wavivu kushambulia na kuchukua ardhi.
And they answered, Arise, that we may goe vp against them: for we haue seene the lande, and surely it is very good, and doe ye sit stil? be not slouthfull to goe and enter to possesse the lande:
10 Mnapoenda, mtakuta watu wanaofikiri wapo salama, na nchi ni pana! Mungu amewapa ninyi-mahali ambako hapajapungukiwa kitu chochote duniani. '
(If ye will goe, ye shall come vnto a carelesse people, and the countrey is large) for God hath giuen it into your hande. It is a place which doeth lacke nothing that is in the worlde.
11 Watu mia sita wa kabila la Dani, wenye silaha za vita, waliondoka kutoka Sora na Eshtaoli.
Then there departed thence of the familie of the Danites, from Zorah and from Eshtaol, sixe hundreth men appointed with instruments of warre.
12 Wakasafiri, wakapanga Kiriath-yearimu, huko Yuda. Ndio maana watu walipaita mahali pale Mahane Dani hata leo; ni magharibi ya Kiriath yearimu.
And they went vp, and pitched in Kiriath-iearim in Iudah: wherefore they called that place, Mahaneh-Dan vnto this day: and it is behinde Kiriath-iearim.
13 Wakaondoka huko na kwenda nchi ya mlima wa Efraimu, wakafika nyumbani kwa Mika.
And they went thence vnto mount Ephraim, and came to the house of Michah.
14 Kisha watu watano waliokuwa wamekwenda kutazama nchi ya Laisha waliwaambia jamaa zao, “Je, mnajua kwamba katika nyumba hizi kuna efodi, miungu ya kaya, sanamu zilizochongwa, na sanamu za chuma? Amua sasa utakachofanya.”
Then answered the fiue men, that went to spie out the countrey of Laish, and said vnto their brethren, Knowe ye not, that there is in these houses an Ephod, and Teraphim, and a grauen and a molten image? Nowe therefore consider what ye haue to doe.
15 Basi wakarudi huko, wakafika nyumbani mwa Mlawi, nyumbani mwa Mika; wakamsalimu.
And they turned thitherward and came to the house of the yong man the Leuite, euen vnto the house of Michah, and saluted him peaceably.
16 Wana Daniani mia sita, wenye silaha za vita, walisimama kwenye maingilio ya lango.
And the six hundreth men appointed with their weapons of warre, which were of the children of Dan, stoode by the entring of the gate.
17 Wale watu watano waliokuwa wamekwenda kutembelea nchi walikwenda huko na wakachukua sanamu zilizochongwa, efodi, na miungu ya nyumba, na sanamu ya chuma, wakati kuhani alipokuwa amesimama kwenye maingilio ya lango na wanaume mia sita wenye silaha za vita.
Then the fiue men that went to spie out the land, went in thither, and tooke the grauen image and the Ephod, and the Teraphim, and the molten image: and the Priest stoode in the entring of the gate with the sixe hundreth men, that were appointed with weapons of warre,
18 Walipokuwa wakiingia nyumbani kwa Mika na kuchukua sanamu zilizochongwa, efodi, miungu ya nyumba, na sanamu za chuma, kuhani akasema, “mnafanya nini?”
And the other went into Michahs house and fet the grauen image, the Ephod, and the Teraphim, and the molten image. Then saide the Priest vnto them, What doe ye?
19 Wakamwambia, “Tulia! Weka mkono wako kwenye kinywa chako na uje nasi, na uwe kwetu baba na kuhani. Je, ni bora kuwa wewe kuhani kwa ajili ya nyumba ya mtu mmoja, au kuhani kwa kabila na jamaa katika Israeli?”
And they answered him, Holde thy peace: lay thine hande vpon thy mouth, and come with vs to be our father and Priest. Whether is it better that thou shouldest be a Priest vnto ye house of one man, or that thou shouldest be a Priest vnto a tribe and to a familie in Israel?
20 Moyo wa kuhani ulifurahi. Akachukua efodi, miungu ya nyumba, na sanamu ya kuchongwa, akaenda pamoja na hao watu.
And the Priestes heart was glad, and hee tooke the Ephod and the Teraphim, and the grauen image, and went among the people.
21 Basi wakageuka wakaenda. Wameweka watoto wadogo mbele yao wenyewe, pamoja na ng'ombe na mali zao.
And they turned and departed, and put the children, and the cattell, and the substance before them.
22 Walipokuwa umbali mzuri kutoka kwa nyumba ya Mika, watu waliokuwa ndani ya nyumba iliyo karibu na nyumba ya Mika waliitwa, nao wakawafikia Wadani.
When they were farre off from the house of Michah, the men that were in the houses neere to Michahs house, gathered together, and pursued after the children of Dan,
23 Waliwapigia kelele Wadani, nao wakageuka, wakamwambia Mika, “Kwa nini mmekuja pamoja?
And cryed vnto the children of Dan: who turned their faces, and said vnto Michah, What ayleth thee, that thou makest an outcrie?
24 Akasema, “ninyi mmeiba miungu niliyoifanya, mmemchukua kuhani wangu, na mnaondoka. Je, nina nini tena? Unawezaje kuniuliza, 'Ni nini kinachokusumbua?'”
And hee saide, Yee haue taken away my gods, which I made, and the Priest, and go your wayes: and what haue I more? howe then say ye vnto me, what ayleth thee?
25 'Watu wa Dani wakamwambia,” Usiruhusu tusikie chochote unachosema, au baadhi ya watu wenye hasira sana watawapiga, wewe na familia yako mtauawa.”
And the children of Dan sayde vnto him, Let not thy voyce be heard among vs, least angrie fellowes runne vpon thee, and thou lose thy life with the liues of thine housholde.
26 Ndipo watu wa Dani wakaenda zao. Mika alipoona kwamba walikuwa na nguvu sana juu yake, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
So the children of Dan went their wayes: and when Michah saw that they were too strong for him, hee turned, and went backe vnto his house.
27 Watu wa Dani walichukua kile alichokifanya Mika, pamoja na kuhani wake, na wakafika Laisha, kwa watu waliokuwa hawasumbuliwi na wenye usalama na salama wakawaua kwa upanga na kuuchoma mji huo.
And they tooke the things which Michah had made, and the Priest which he had, and came vnto Laish, vnto a quiet people and without mistrust, and smote them with the edge of the sworde, and burnt the citie with fire:
28 Hapakuwa na mtu wa kuwaokoa kwa sababu palikuwa na umbali mrefu kutoka Sidoni, na hawakuwa na uhusiano na mtu yeyote. Palikuwa katika bonde lililo karibu na Beth Rehobu. Wadani wakaujenga mji na kuishi huko.
And there was none to helpe, because Laish was farre from Zidon, and they had no businesse with other men: also it was in the valley that lyeth by Beth-rehob. After, they built the citie, and dwelt therein,
29 Wakauita jina lake Dani, jina la baba zao Dani, ambaye alikuwa mmoja wa wana wa Israeli. Lakini jina la mji hapo mwanzo ulikuwa Laisha.
And called the name of the citie Dan, after the name of Dan their father which was borne vnto Israel: howbeit the name of the city was Laish at the beginning.
30 Watu wa Dani walijenga sanamu za kuchonga wenyewe. Naye Yonathani, mwana wa Gershomu, mwana wa Musa, yeye na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka siku ya uhamisho wa nchi.
Then the children of Dan set them vp the grauen image: and Ionathan the sonne of Gershom, the sonne of Manasseh and his sonnes were the Priestes in the tribe of the Danites vntil the day of the captiuitie of the lande.
31 Basi wakaiabudu sanamu ya kuchonga ya Mika aliyoifanya wakati wa nyumba ya Mungu huko Shilo.
So they set them vp the grauen image, which Michah had made, all the while the house of God was in Shiloh.

< Waamuzi 18 >