< Waamuzi 16 >
1 Samsoni alikwenda Gaza na akamwona kahaba huko, naye akalala pamoja naye.
И иде Сампсон в Газу, и виде тамо жену блудницу и вниде к ней.
2 Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja hapa.” Watu wa Gaza wakazunguka mahali hapo kwa siri, wakamngoja usiku wote katika lango la jiji. Walikaa kimya usiku wote. Wakisema, “Hebu tusubiri mpaka mchana, na kisha tumwuue.”
И поведаша Газяном, глаголюще: прииде Сампсон семо. И обыдоша и подседоша ему всю нощь у врат градных, и утаишася всю нощь, глаголюще: дондеже осветает утро, и убием его.
3 Samsoni akalala kitandani mpaka usiku wa manane. Usiku wa manane akaamka na akashika mlango wa jiji na miimo yake miwili. Akavivuta kutoka nje, komeo na vyote, akaviweka kwenye mabega yake, akavichukua hadi juu ya kilima, mbele ya Hebroni.
И спа Сампсон до полунощи: и воста в полунощи, и восхити двери у врат града со обеими вереями, и подя оныя с заворою, и возложи я на рамена своя, и вознесе я на верх горы, яже пред лицем Хеврона, и положи их тамо.
4 Baada ya hayo, Samsoni alimpenda mwanamke aliyeishi katika bonde la Soreki. Jina lake alikuwa Delila.
И бысть по сем, и возлюби жену от водотечи Сориховы: имя же ей Далида.
5 Wale wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, “mdanganye Samsoni ili uone mahali zilipo nguvu zake kuu, na kwa namna gani tunaweza kumshinda, ili tumfunge na kumtesa. Fanya hili, na kila mmoja wetu atakupa vipande 1, 100 vya fedha.”
И взыдоша к ней князи иноплеменничи и рекоша ей: прельсти его, и виждь, в чем есть крепость его великая, и чим преможем его, и свяжем его, яко смирити его: и мы тебе дадим кийждо тысящу и сто сребреников.
6 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Tafadhali, niambie ni kwa jinsi gani wewe ni mwenye nguvu sana, na kwa namna gani mtu anaweza kukufunga, ili aweze kukudhibiti?”
И рече Далида к Сампсону: повеждь ми ныне, в чем крепость твоя (тако) великая, и чим свяжешися и смиришися?
7 Samsoni akamwambia, “Ikiwa watanifunga na kamba saba safi ambazo hazijakauka, nitakuwa dhaifu na kuwa kama mtu mwingine yeyote.”
И рече ей Сампсон: аще свяжут мя седмию тятивами сырыми неистлевшими, и изнемогу, и буду яко един от человек.
8 Basi wakuu wa Wafilisti wakamletea Delila kamba saba ambazo hazijakauka, naye akamfunga Samsoni.
И принесоша ей князи от иноплеменник седмь тятив мокрых неистлевших, и связа его ими:
9 Sasa alikuwa na watu waliojificha kwa siri, walikaa katika chumba chake cha ndani. Akamwambia, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Lakini akazikata kamba kama uzi wakati unapogusa moto. Na hawakujifunza siri ya nguvu zake.
и подсада ему седяше в храмине. И рече ему: иноплеменницы на тя, Сампсоне. И расторже тятивы, аки бы кто расторгнул соскание изгребий, егда коснется ему огнь: и не уведася крепость его.
10 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Ndivyo ulivyonidanganya mimi na kuniambia uongo. Tafadhali, niambie kwa namna gani unaweza kufungwa.”
И рече Далида к Сампсону: се, прельстил еси мя, глаголя ко мне лжу: ныне убо повеждь ми, чим свяжешися?
11 Akamwambia, “Ikiwa watanifunga na kamba mpya ambayo haijawahi kutumika kwa kazi, nitakuwa dhaifu na kama mtu mwingine yeyote.”
И рече к ней: аще вяжуще свяжут мя ужы новыми, имиже не делано, и изнемогу, и буду яко един от человек.
12 Basi Delila alichukua kamba mpya akamfunga pamoja naye, akamwambia, “Wafilisti wako juu yako Samsoni!” Watu waliokuwa wakisubiri walikuwa ndani ya chumba cha ndani. Lakini Samsoni akaondoa kamba kutoka mikono yake kama kilikuwa kipande cha uzi.
И взя Далида ужы новы и связа его ими, и рече ему: иноплеменницы на тя, Сампсоне. Подсада же седяше в храмине. И расторже я от руку своею аки нить.
13 Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa umenidanganya na kuniambia uongo. Niambie kwa namna gani unaweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, 'Ikiwa utavifuma vifungo saba vya nywele zangu na kuvifunga kwenye kitambaa, kisha kufunga kwenye msumari, nitakuwa kama mtu mwingine yeyote.”
И рече Далида к Сампсону: даже до ныне прельщал мя еси и глаголал ко мне лжу: повеждь ми убо, чим свяжешися? И рече ей: аще сплетеши седмь плениц влас главы моея спрядением и вбиеши колом в стену, и буду немощен яко един от человек.
14 Alipokuwa amelala, Dalila akavifuma vifungo saba vya nywele zake akavifunga ndani ya kitambaa na kuzifunga kwenye msumari, akamwambia, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Aliamka kutoka usingizini akang'oa kitambaa na pini zilizokuwa zimefungwa.
И успи Далида его на коленех своих, и бысть внегда уснути ему, взя Далида седмь плениц влас главы его и сплете спрядением и вонзе колом в стену, и рече: иноплеменницы на тя, Сампсоне. И возбну от сна своего и исторже кол сплетением из стены, и не уведася крепость его.
15 Akamwambia, “Wawezaje kusema,” Unanipenda, wakati hushiriki siri zako na mimi? Umenidhihaki mara tatu hizi na hukukuambia ni kwa jinsi gani unazo nguvu nyingi.”
И рече к нему Далида: како глаголеши, возлюбих тя, и сердце твое несть со мною? Се, третие прельстил еси мя, и не поведал еси мне, в чем крепость твоя великая.
16 Kila siku alisisitiza kwa bidii na maneno yake, naye akamkemea sana kiasi kwamba alitamani kufa.
И бысть егда стужи ему словесы своими по вся дни, и убеди его, и изнеможе даже до умертвия.
17 Basi Samsoni alimwambia kila kitu, akamwambia, “Wembe haujawahi kukata nywele juu ya kichwa changu, kwa maana nimekuwa Mnaziri kwa Mungu kutoka tumboni mwa mama yangu. Ikiwa kichwa changu kitanyolewa, basi nguvu zangu zitaniacha, nami nitakuwa dhaifu na kuwa kama kila mtu mwingine. '
И поведа ей все сердце свое, и рече к ней: железо не взыде на главу мою, яко назорей есмь аз Господу от утробы матере моея: аще убо обриюся, отступит от мене крепость моя, и изнемогу, и буду якоже вси человецы.
18 Delila alipoona kwamba amemwambia ukweli juu ya kila kitu, akawatuma na kuwaita watawala wa Wafilisti, akisema, “Njooni tena, kwa maana ameniambia kila kitu.” Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakaleta fedha mkononi mwao.
И виде Далида, яко поведа ей все сердце свое, посла и призва князи иноплеменничи, глаголющи: взыдите еще единою, яко поведа ми все сердце свое. И взыдоша к ней вси князи иноплеменничи, и принесоша сребро в руках своих.
19 Alimfanya alale katika magoti yake. Alimwita mtu avinyoe vifungo saba vya kichwa chake, naye akaanza kumshinda, kwa maana nguvu zake zilikuwa zimemwacha.
И успи Далида Сампсона на коленех своих: и призва стригача, и остриже седмь плениц влас главы его: и нача смирятися, и отступи крепость его от него.
20 Alisema, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Aliamka nje ya usingizi wake akasema, “Nitatoka nje kama nyakati nyingine na kujiweka huru.” Lakini hakujua kwamba Bwana amemwacha.
И рече Далида: иноплеменницы на тя, Сампсоне. И возбудися от сна своего и рече: изыду якоже и прежде, и отрясуся. И не разуме, яко Господь отступи от него.
21 Wafilisti walimkamata na kumng'oa macho. Wakampeleka Gaza na kumfunga kwa shaba. Alikuwa akisaga ngano katika gerezani.
И яша его иноплеменницы, и избодоша ему очи, и введоша его в Газу, и оковаша его путы медяны: и бяше меля в храмине темничней.
22 Lakini nywele juu ya kichwa chake zilianza kukua tena baada ya kunyolewa.
И начаша власы главы его расти по острижении.
23 Watawala wa Wafilisti walikusanyika ili kutoa dhabihu kubwa kwa Dagoni mungu wao, na kufurahi. Walisema, “mungu wetu amemshinda Samsoni, adui yetu, na kumtia katika ufahamu wetu.”
И князи иноплеменничи собрашася пожрети жертву велику Дагону богу своему и возвеселитися, и рекоша: предаде бог наш в руки нашя Сампсона врага нашего.
24 Watu walipomwona, walimsifu mungu wao, kwa sababu walisema, “mungu wetu ameshinda adui yetu na kutupa sisi - mharibifu wa nchi yetu, ambaye aliwaua wengi wetu.”
И видеша его людие, и похвалиша бога своего, яко реша: предаде бог наш в руки нашя врага нашего, опустошившаго землю нашу, и иже умножи язвенных наших.
25 Walipokuwa wakisherehekea, wakasema, 'Mwite Samsoni, aje kutufurahisha.' Walimwita Samsoni nje ya jela na akawafanya wacheke. Walimsimamisha katikati ya nguzo.
И бысть егда возблажа сердце их, и рекоша: призовите Сампсона из дому темничнаго, и да играет пред нами. И призваша Сампсона из дому темничнаго, и играша пред ними: и заушаху его, и поставиша его между столпы.
26 Samsoni akamwambia yule kijana ambaye alikuwa ameshika mkono wake, 'Niruhusu nishike nguzo zilizoshikilia nyumba hii, ili nipate kuegemea.”
И рече Сампсон ко юноши держащему его за руку: остави мене, да осяжу столпы, на нихже дом сей утвержден есть, и опруся на них. Юноша же сотвори тако.
27 Sasa nyumba ilikuwa imejaa wanaume na wanawake. Watawala wote wa Wafilisti walikuwa huko. Juu ya paa kulikuwa na wanaume na wanawake elfu tatu, ambao walikuwa wakiangalia wakati Samsoni alipokuwa akiwafurahisha.
Дом же бяше полн мужей и жен, и тамо вси князи иноплеменничи: на крове же том до трех тысящ мужей и жен, зряще ругаемаго Сампсона.
28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, “Bwana MUNGU, nipe nia! Tafadhali niimarishe mara moja tu, Mungu, ili nipate kulipiza kisasi kwa Wafilisti kwa kuchukua macho yangu mawili.
И воззва Сампсон ко Господу и рече: Адонаи Господи, Господи Сил, помяни мя ныне, и укрепи мя еще единою, Боже, да воздам мщение едино за два ока моя Филистимом.
29 Samsoni aliweka nguzo mbili katikati ambzo zinashikilia nyumba hiyo, naye akaegemea juu yake, nguzo moja kwa mkono wake wa kuume, na mwingine kwa kushoto kwake.
И объя Сампсон оба столпа средния, на нихже храмина бяше утверждена, и опреся на них, держя един рукою десною, а другий левою.
30 Samsoni akasema, “Na nife pamoja na Wafilisti!” Alipanda kwa nguvu zake na jengo likaanguka juu ya watawala na juu ya watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo waliouawa wakati alikufa walikuwa zaidi ya wale waliouawa wakati wa maisha yake.
И рече Сампсон: да умрет душа моя со иноплеменники. И преклонися крепостию, и паде храмина на князи и на вся люди иже в ней: и бысть мертвых, ихже умертви Сампсон при смерти своей, множае неже ихже умертви в животе своем.
31 Kisha ndugu zake na nyumba yote ya baba yake wakashuka. Wakamchukua, wakamrudisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli katika mahali pa kuzikwa Manoa, baba yake. Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.
И снидоша братия его и весь дом отца его, и взяша его: и взыдоша, и погребоша его между Сараи и между Есфаолом во гробе Маноя отца его. И сей суди Израилю лет двадесять. (и воста по Сампсоне Емегар сын Енань, и уби от иноплеменников шесть сот мужей кроме скота, и спасе и он Израиля.)