< Waamuzi 10 >
1 Baada ya Abimeleki, Tola, mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, aliyekaa Shamiri, katika mlima wa Efraimu, akaondoka ili kuwaokoa Israeli.
And he arose after Abimelech to deliver Israel Tola [the] son of Puah [the] son of Dodo man of Issachar and he [was] dwelling in Shamir in [the] hill country of Ephraim.
2 Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na mitatu. Alikufa na kuzikwa Shamiri.
And he judged Israel twenty and three year[s] and he died and he was buried in Shamir.
3 Alifuatiwa na Yairi Mgileadi. Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na miwili.
And he arose after him Jair the Gileadite and he judged Israel twenty and two year[s].
4 Alikuwa na wana thelathini waliokuwa wakipanda kwenye punda thelathini, na walikuwa na miji thelathini, ambayo inaitwa Hawoth Yairi hata leo, iliyo katika nchi ya Gileadi.
And it belonged to him thirty sons [who] rode on thirty donkeys and thirty cities [belonged] to them them people call - Havvoth Jair until the day this which [are] in [the] land of Gilead.
5 Yairi alikufa na kuzikwa Kamoni.
And he died Jair and he was buried in Kamon.
6 Watu wa Israeli waliendelea kutenda maovu mbele za Bwana, wakaabudu Mabaali, Maashtoreti, miungu ya Aramu, miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu, miungu ya wana wa Amoni, na miungu ya Wafilisti. Wakamsahau Bwana na hawakamsujudia tena.
And they repeated - [the] people of Israel to do the evil in [the] eyes of Yahweh and they served the Baals and the Ashtaroth and [the] gods of Aram and [the] gods of Sidon and - [the] gods of Moab and [the] gods of [the] people of Ammon and [the] gods of [the] Philistines and they forsook Yahweh and not they served him.
7 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mikononi mwa Wafilisti na katika mikono ya wana wa Amoni.
And it burned [the] anger of Yahweh on Israel and he sold them in [the] hand of [the] Philistines and in [the] hand of [the] people of Ammon.
8 Wakawaangamiza na kuwadhulumu watu wa Israeli mwaka huo, na kwa muda wa miaka kumi na nane waliwafukuza watu wote wa Israeli waliokuwa ng'ambo ya Yordani katika nchi ya Waamori, iliyoko Gileadi.
And they shattered and they crushed [the] people of Israel in the year that eight-teen year[s] all [the] people of Israel who [were] on [the] other side of the Jordan in [the] land of the Amorite[s] which [is] in Gilead.
9 Nao wana wa Amoni wakavuka Yordani, wakapigana na Yuda, na Benyamini, na nyumba ya Efraimu; Israeli akasumbuliwa sana.
And they passed over [the] people of Ammon the Jordan to fight also against Judah and against Benjamin and against [the] house of Ephraim and it was distress to Israel exceedingly.
10 Ndipo wana wa Israeli wakamwita Bwana, wakisema, “Tumekukosea, kwa sababu tumemwacha Mungu wetu, tukaabudu Mabaali.”
And they cried out [the] people of Israel to Yahweh saying we have sinned to you and for we have forsaken God our and we have served the Baals.
11 Bwana akawaambia wana wa Israeli, “Je, sikuwatoa ninyi kutoka kwa Wamisri, na Waamori, na Waamoni, na Wafilisti,
And he said Yahweh to [the] people of Israel ¿ not from Egypt and from the Amorite[s] and from [the] people of Ammon and from [the] Philistines.
12 na pia kwa Wasidoni? Waamaleki na Wamaoni walipowakandamiza; mliniita, nami nikawaokoa kutoka katika nguvu zao.
And [the] Sidonians and Amalek and Maon they oppressed you and you cried out to me and I delivered! you from hand their.
13 Lakini ninyi mliniacha tena na kuabudu miungu mingine. Kwa hiyo, sitawaokoa tena.
And you you have forsaken me and you have served gods other therefore not I will repeat to deliver you.
14 Nendeni mkaiite miungu mnayoiabudu. Ili iwaokoe wakati wa shida.
Go and cry out to the gods which you have chosen them they let them deliver you at [the] time of distress your.
15 Wana wa Israeli wakamwambia Bwana, Tumefanya dhambi. Tufanyie chochote kinachoonekana kuwa kizuri kwako. Tafadhali, tuokoe leo.
And they said [the] people of Israel to Yahweh we have sinned do you to us according to all the good in view your only deliver us please the day this.
16 Wakaiacha miungu ya kigeni waliyokuwa nayo, nao wakamwabudu Bwana. Naye akawa na subira juu ya taabu ya Israeli.
And they removed [the] gods of foreignness from midst their and they served Yahweh and it was short self his at [the] trouble of Israel.
17 Ndipo Waamoni wakakusanyika, wakaweka kambi Gileadi. Waisraeli walikutana na kuweka kambi yao huko Mispa.
And they were summoned [the] people of Ammon and they encamped in Gilead and they gathered [the] people of Israel and they encamped at Mizpah.
18 Viongozi wa watu wa Gileadi wakaambiana, 'Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni? Yeye atakuwa kiongozi juu ya wote wanaoishi Gileadi.
And they said the people [the] leaders of Gilead each to neighbor his who? [is] the man who he will begin to fight against [the] people of Ammon he will become chief of all [the] inhabitants of Gilead.