< Waamuzi 10 >
1 Baada ya Abimeleki, Tola, mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, aliyekaa Shamiri, katika mlima wa Efraimu, akaondoka ili kuwaokoa Israeli.
After Abimelech, a leader rose up in Israel, Tola, the son of Puah, the paternal uncle of Abimelech, a man of Issachar, who lived in Shamir on mount Ephraim.
2 Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na mitatu. Alikufa na kuzikwa Shamiri.
And he judged Israel for twenty-three years, and he died and was buried at Shamir.
3 Alifuatiwa na Yairi Mgileadi. Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na miwili.
After him succeeded Jair, a Gileadite, who judged Israel for twenty-two years,
4 Alikuwa na wana thelathini waliokuwa wakipanda kwenye punda thelathini, na walikuwa na miji thelathini, ambayo inaitwa Hawoth Yairi hata leo, iliyo katika nchi ya Gileadi.
having thirty sons sitting upon thirty young donkeys, and who were leaders of thirty cities, which from his name were called Havvoth Jair, that is, the towns of Jair, even to the present day, in the land of Gilead.
5 Yairi alikufa na kuzikwa Kamoni.
And Jair died, and he was buried in the place which is called Kamon.
6 Watu wa Israeli waliendelea kutenda maovu mbele za Bwana, wakaabudu Mabaali, Maashtoreti, miungu ya Aramu, miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu, miungu ya wana wa Amoni, na miungu ya Wafilisti. Wakamsahau Bwana na hawakamsujudia tena.
But the sons of Israel did evil in the sight of the Lord, joining new sins to old, and they served idols, the Baals and Ashtaroth, and the gods of Syria and Sidon, and of Moab and the sons of Ammon, and the Philistines. And they abandoned the Lord, and they did not worship him.
7 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mikononi mwa Wafilisti na katika mikono ya wana wa Amoni.
And the Lord, becoming angry against them, delivered them into the hands of the Philistines and the sons of Ammon.
8 Wakawaangamiza na kuwadhulumu watu wa Israeli mwaka huo, na kwa muda wa miaka kumi na nane waliwafukuza watu wote wa Israeli waliokuwa ng'ambo ya Yordani katika nchi ya Waamori, iliyoko Gileadi.
And they were afflicted and vehemently oppressed for eighteen years, all who were living beyond the Jordan in the land of the Amorite, which is in Gilead,
9 Nao wana wa Amoni wakavuka Yordani, wakapigana na Yuda, na Benyamini, na nyumba ya Efraimu; Israeli akasumbuliwa sana.
to such a great extent that the sons of Ammon, crossing over the Jordan, laid waste to Judah and Benjamin and Ephraim. And Israel was exceedingly afflicted.
10 Ndipo wana wa Israeli wakamwita Bwana, wakisema, “Tumekukosea, kwa sababu tumemwacha Mungu wetu, tukaabudu Mabaali.”
And crying out to the Lord, they said: “We have sinned against you. For we have forsaken the Lord our God, and we have served the Baals.”
11 Bwana akawaambia wana wa Israeli, “Je, sikuwatoa ninyi kutoka kwa Wamisri, na Waamori, na Waamoni, na Wafilisti,
And the Lord said to them: “Did not the Egyptians, and the Amorites, and the sons of Ammon, and the Philistines,
12 na pia kwa Wasidoni? Waamaleki na Wamaoni walipowakandamiza; mliniita, nami nikawaokoa kutoka katika nguvu zao.
and also the Sidonians, and Amalek, and Canaan, oppress you, and so you cried out to me, and I rescued you from their hand?
13 Lakini ninyi mliniacha tena na kuabudu miungu mingine. Kwa hiyo, sitawaokoa tena.
And yet you have forsaken me, and you have worshipped foreign gods. For this reason, I will not continue to free you any more.
14 Nendeni mkaiite miungu mnayoiabudu. Ili iwaokoe wakati wa shida.
Go, and call upon the gods whom you have chosen. Let them free you in the time of anguish.”
15 Wana wa Israeli wakamwambia Bwana, Tumefanya dhambi. Tufanyie chochote kinachoonekana kuwa kizuri kwako. Tafadhali, tuokoe leo.
And the sons of Israel said to the Lord: “We have sinned. You may repay us in whatever way pleases you. Yet free us now.”
16 Wakaiacha miungu ya kigeni waliyokuwa nayo, nao wakamwabudu Bwana. Naye akawa na subira juu ya taabu ya Israeli.
And saying these things, they cast out all the idols of the foreign gods from their regions, and they served the Lord God. And he was touched by their miseries.
17 Ndipo Waamoni wakakusanyika, wakaweka kambi Gileadi. Waisraeli walikutana na kuweka kambi yao huko Mispa.
And then the sons of Ammon, shouting out together, pitched their tents in Gilead. And the sons of Israel gathered together against them, and they made camp at Mizpah.
18 Viongozi wa watu wa Gileadi wakaambiana, 'Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni? Yeye atakuwa kiongozi juu ya wote wanaoishi Gileadi.
And the leaders of Gilead said to one another, “Whoever among us will be the first to begin to contend against the sons of Ammon, he shall be the leader of the people of Gilead.”