< Yoshua 8 >
1 Yahweh akamwambia Yoshua, “Usiogope; usivunjike moyo. Chukua pamoja nawe watu wa vita. Pandeni kwenda Ai. Tazama nimemtia mkononi mwako mfalme wa Ai, watu wake, mji wake na nchi yake.
Yahvé dit à Josué: « N'aie pas peur et ne t'effraie pas. Prends avec toi tous les guerriers, lève-toi et monte à Aï. Voici que je livre entre tes mains le roi d'Aï, son peuple, sa ville et son pays.
2 Mtafanya hivyo pia huko Ai na mfalme wake kama mlivyofanya kwa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mtachukua nyara na mifugo kwa ajili yenu. Pangeni mashambulizi ya uviziaji nyuma ya mji.”
Tu feras à Aï et à son roi ce que tu as fait à Jéricho et à son roi, sauf que tu prendras pour toi ses biens et son bétail. Mettez la ville en embuscade derrière elle. »
3 Basi Yoshua aliinuka na akawachukua kwenda Ai watu wote wa vita. Kisha Yoshua akachagua watu elfu thelathini - wenye nguvu na ujasiri - na aliwatuma waende wakati wa usiku.
Et Josué se leva, avec tous les guerriers, pour monter à Aï. Josué choisit trente mille hommes, les plus vaillants, et les envoya de nuit.
4 Aliwaamuru, “Tazama, mtalala katika hali ya mashambulizi ya uviziaji dhidi ya mji, kwa nyuma yake. Usiende mbali sana na mji, lakini ninyi nyote muwe tayari.
Il leur donna cet ordre: « Voici, vous vous mettrez en embuscade contre la ville, derrière la ville. Ne vous éloignez pas beaucoup de la ville, mais tenez-vous tous prêts.
5 Mimi pamoja na watu wote walio pamoja nami tutaukaribia mji. Na wakati watakapokuja kutushambulia sisi, tutawakimbia kama tulivyofanya hapo mwanzo.
Moi et tout le peuple qui est avec moi, nous nous approcherons de la ville. Lorsqu'ils sortiront contre nous, comme au début, nous fuirons devant eux.
6 Watatoka nje watukimbize mpaka hapo tutakapokuwa tumewavuta mbali sana na mji, watasema, “Wanatukimbia kama walivyofanya mara ya mwisho.' Hivyo tutawakimbia na kwenda mbali.
Ils sortiront après nous jusqu'à ce que nous les ayons éloignés de la ville, car ils diront: « Ils fuient devant nous, comme la première fois ». Nous fuirons donc devant eux,
7 Kisha mtapanda kutoka sehemu mliyojificha, na mtauteka mji. Yahweh Mungu wenu atawapa mkononi mwenu.
et vous vous lèverez de l'embuscade, et vous prendrez possession de la ville, car l'Éternel, votre Dieu, la livrera entre vos mains.
8 Tazama nimewaamuru, mtakapouteka mji, mtauchoma moto. Mtayafanya haya wakati mtakapotii agizo lililotolewa katika neno la Yahweh.”
Lorsque vous vous serez emparés de la ville, vous y mettrez le feu. Tu feras cela selon la parole de Yahvé. Voici, je te l'ai ordonné. »
9 Yoshua akawatuma, na wakaenda sehemu ya uviziajia, na wakajificha kati ya Betheli na Ai sehemu ya magharibi ya Ai. Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku ule.
Josué les envoya; ils allèrent préparer l'embuscade, et ils restèrent entre Béthel et Aï, à l'ouest d'Aï; mais Josué resta au milieu du peuple cette nuit-là.
10 Yoshua aliamka asubuhi na mapema na akawaandaa tayari wanajeshi wake, Yoshua na wazee wa Israeli walishambuliwa watu wa Ai.
Josué se leva de bon matin, rassembla le peuple, et monta, lui et les anciens d'Israël, devant le peuple, à Aï.
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda na kuukaribia mji. Walisogea karibu na mji na wakapiga kambi sehemu ya kasikazini mwa Ai. Kulikuwa na bonde kati yao na Ai.
Tout le peuple, même les hommes de guerre qui étaient avec lui, montèrent et s'approchèrent, arrivèrent devant la ville et campèrent au nord d'Aï. Or, il y avait une vallée entre lui et Aï.
12 Alichukua watu wapatao elfu tano hivi na akawaweka katika hali ya kuvizia katika upande wa magharibi mwa mji kati ya Betheli na Ai.
Il prit environ cinq mille hommes, et les mit en embuscade entre Béthel et Aï, à l'ouest de la ville.
13 Waliwapanga wanajeshi wote, jeshi kuu katika upande wa kasikazini mwa mji, na walinzi wa nyuma upande wa magharibi mwa mji. Yoshua alilala bondeni usiku ule.
Ils mirent donc le peuple, toute l'armée qui était au nord de la ville, et leur embuscade à l'ouest de la ville; et Josué alla cette nuit-là au milieu de la vallée.
14 Na ilikuwa alipoona hilo mfalme wa Ai, yeye pamoja na jeshi lake, waliamka asubuhi na mapema na walitoka kwa haraka kwenda kuwashambulia Israeli katika eneo linalokabili bonde la Mto Yordani. Hakujua kuwa kulikuwa na shambulizi la kuvizia lilikuwa linasubiria kushambulia kutokea kwa nyuma ya mji.
Lorsque le roi d'Aï vit cela, il se hâta et se leva de bonne heure, et les hommes de la ville sortirent contre Israël pour livrer bataille, lui et tout son peuple, au moment fixé, devant la plaine; mais il ne savait pas qu'il y avait une embuscade contre lui derrière la ville.
15 Yoshua na Waisraeli wote walikubali wenyewe kushindwa mbele yenu, na wakakimbia kuelekea nyikani.
Josué et tout Israël firent comme s'ils étaient battus devant eux, et s'enfuirent par le chemin du désert.
16 Watu wote waliokuwa kwenye mji waliitwa kwa pamoja waende mbele yao, na walienda mbele ya Yoshua na kwa jinsi hiyo walivutwa mbali na mji.
Tout le peuple qui était dans la ville se rassembla pour les poursuivre. Ils poursuivirent Josué, et furent entraînés loin de la ville.
17 Hapakuwa na mtu mme aliyesalia Ai na Betheli ambaye alikuwa hajaenda nje kuwafuatilia waisraeli. Na walipokuwa wanawafuatilia Waisraeli, Wakatoka na waliuacha mji wazi.
Il ne resta pas un homme à Aï ou à Béthel qui ne se soit mis à la poursuite d'Israël. Ils laissèrent la ville ouverte, et poursuivirent Israël.
18 Yahweh akamwambia Yoshua, “Nyosha mkuki huo ulio mkononi mwako kuelekea Ai, kwa kuwa nitaitia Ai mikononi mwako.” Yoshua akaunyosha mkuki uliokuwa mkononi mwake kuuelekea mji.
Yahvé dit à Josué: « Étends le javelot qui est dans ta main vers Aï, car je vais le livrer entre tes mains. » Josué étendit vers la ville le javelot qu'il avait à la main.
19 Wanajeshi waliojificha katika hali ya kuvizia walitoka upesi katika eneo lao mara tu alipounyosha mkono wake. Walikimbia mbio na kuuingia mji na kuuteka. Na kwa haraka wakauchoma moto mji.
L'embuscade se leva rapidement de sa place, et ils coururent dès qu'il eut tendu la main, entrèrent dans la ville et la prirent. Ils se précipitèrent et mirent le feu à la ville.
20 Watu wa Ai waligeuka na kuangalia nyuma. Waliona moshi kutoka katika mji ukipanda kwenda angani, na hawakuweza kutoroka kwa njia hii au ile. Kwa kuwa wanajeshi wa Israelei waliokuwa wamekimbia katika nyika, sasa walirudi kuwakabili wale waliokuwa wanawafuatilia.
Lorsque les hommes d'Aï regardèrent derrière eux, ils virent et voici que la fumée de la ville montait jusqu'au ciel, et ils n'eurent pas la force de fuir par ici ou par là. Le peuple qui s'était enfui dans le désert se retourna contre ses poursuivants.
21 Na wakati Yoshua na Israeli wote walipoona kuwa wale watu wa kuvizia wameuteka mji kwa ule moshi uliokuwa ukipanda, waligeuka nyuma na kuwaua watu wa Ai.
Lorsque Josué et tout Israël virent que l'embuscade avait pris la ville et que la fumée de la ville montait, ils firent demi-tour et tuèrent les hommes d'Aï.
22 Na wanajeshi wengine wa Israeli, wale waliokuwa wameingia ndani ya mji, walitoka nje ili kuwashambulia. Hivyo, watu wa Ai walikamatwa katikati ya majeshi ya Israeli, baadhi katika upande huu na wengine katika upande ule.
Les autres sortirent de la ville contre eux, de sorte qu'ils se trouvaient au milieu d'Israël, les uns de ce côté-ci, les autres de ce côté-là. Ils les frappèrent, de sorte qu'ils ne laissèrent aucun d'entre eux rester ou s'échapper.
23 Lakini walimhifadhi mfalme wa Ai, ambaye walimteka akiwa hai, na kisha wakamleta kwa Yoshua.
Ils capturèrent vivant le roi d'Aï et l'amenèrent à Josué.
24 Ilikuwa baada ya Israeli walipokuwa wamemaliza kuuwaua wenyeji wote wa Ai katika uwanda kariibu na nyika mahali walipowafuata, na baada ya wao wote, hata yule wa mwisho, walipokuwa wamekwisha kulala kwa ncha ya upanga, Waisraeli wote walirudi Ai. Waliuteka mji kwa ncha ya upanga.
Lorsqu'Israël eut achevé de tuer tous les habitants d'Aï dans les champs, dans le désert où ils les poursuivaient, et qu'ils furent tous tombés au fil de l'épée jusqu'à ce qu'ils eussent disparu, tout Israël revint vers Aï et la frappa du fil de l'épée.
25 Wale wote walikufa siku hiyo walikuwa watu elfu kumi na mbili elfu, wanaume na wanawake, wote ni watu wa Ai.
Tous ceux qui tombèrent ce jour-là, hommes et femmes, furent douze mille, tout le peuple d'Aï.
26 Yoshua hakuukunja mkono wake ambao alikuwa ameunyosha huku akishikilia mkuki wake, mpaka pale alipowateketeza kabisa watu wote wa Ai.
Car Josué ne retira pas sa main, avec laquelle il avait tendu le javelot, jusqu'à ce qu'il eût dévasté tous les habitants d'Aï.
27 Waisraeli walichukua tu wanyama na nyara kutoka katika mji kwa ajili yao wenyewe, kama Yahweh alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
Israël ne prit pour lui que le bétail et les biens de cette ville, selon la parole de Yahvé qu'il avait donnée à Josué.
28 Yoshua aliichoma Ai na kuigeuza kuwa kichuguu cha mapango. Ni mahali palipoachwa ukiwa hata leo.
Josué brûla Aï et en fit un monceau à jamais, une désolation, jusqu'à ce jour.
29 Alimtundika mfalme wa Ai juu ya mti mpaka jioni. Na jua lilipokuwa linaenda kuzama, Yoshua aliwaagiza na wakautoa mwili wa mfalme wakaushusha chini ya mti na kuutupa mbele ya malango ya mji. Huko wakaweka kichuguu kikubwa cha mawe juu yake. Kichuguu hicho kimebaki huko hata leo.
Il pendit le roi d'Aï à un arbre jusqu'au soir. Au coucher du soleil, Josué donna l'ordre de descendre son corps de l'arbre, de le jeter à l'entrée de la porte de la ville et d'élever sur lui un grand tas de pierres qui subsiste encore aujourd'hui.
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu kwa Yahweh, Mungu wa Israeli katika Mlima wa Ebali,
Josué bâtit un autel à Yahvé, le Dieu d'Israël, sur le mont Ebal,
31 kama vile Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza watu wa Israeli, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa: “Madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna mtu yeyote aliyetumia zana ya chuma.” Na allimtolea Yahweh sadaka ya kuteketezwa juu yake na wakatoa sadaka ya amani.
comme Moïse, serviteur de Yahvé, l'avait ordonné aux enfants d'Israël, selon ce qui est écrit dans le livre de la loi de Moïse: un autel de pierres brutes, sur lequel personne n'avait levé de fer. Ils y offraient des holocaustes à Yahvé et y sacrifiaient des sacrifices de prospérité.
32 Na huko aliandika juu ya mawe nakala ya sheria za Musa mbele ya watu wa Israeli.
Il écrivit là, sur les pierres, une copie de la loi de Moïse, qu'il avait écrite en présence des enfants d'Israël.
33 Waisraeli wote, wazee wao, maafisa, na waamuzi wao walisimama katika sehemu mbili za sanduku mbele ya makuhani na Walawi ambao hulibeba sanduku la Agano la Yahweh - wageni pamoja na wazalia, nusu yao walisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu walisimama mbele ya Mlima Ebali. Waliwabariki watu wa Israeli kama Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza hapo mwanzo.
Tout Israël, avec ses anciens, ses officiers et ses juges, se tenait des deux côtés de l'arche devant les prêtres lévitiques qui portaient l'arche de l'alliance de l'Éternel, l'étranger comme l'indigène, la moitié devant le mont Gerizim et l'autre moitié devant le mont Ebal, comme Moïse, serviteur de l'Éternel, l'avait ordonné dès le début, afin qu'ils bénissent le peuple d'Israël.
34 Baada ya hayo, Yoshua alisoma maneno yote ya sheria, baraka na laana, kama zilivyoandikwa katika kitabu cha sheria.
Ensuite, il lut toutes les paroles de la loi, les bénédictions et les malédictions, selon tout ce qui est écrit dans le livre de la loi.
35 Halikusalia hata neno moja katika yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua ambalo halikusomwa mbele ya kusanyiko la Waisraeli lilojumuisha wanawake, watoto wadogo na wageni walioishi miongoni mwao.
Il n'y eut pas un seul mot de tout ce que Moïse avait ordonné que Josué n'ait lu devant toute l'assemblée d'Israël, avec les femmes, les petits enfants et les étrangers qui étaient au milieu d'eux.