< Yoshua 7 >

1 Lakini watu wa Israeli hawakutenda katika uaminifu kuhusiana na vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu. Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka katika kabila la Yuda, alivitwaa baadhi ya vitu hivyo vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya uharibifu, na hasira ya Yahweh iliwaka juu yawatu wa Israeli.
Mais les enfants d'Israël se rendirent coupables au sujet de l'interdit: car Hacan fils de Carmi, fils de Zabdi, fils de Zara, de la Tribu de Juda, prit de l'interdit, et la colère de l'Eternel s'enflamma contre les enfants d'Israël.
2 Yoshua alituma watu kutoka Yeriko kwenda Ai, mji uliokuwa karibu na Bethi Aveni, mashariki mwa Betheli. Aliwaambia, “Nendeni na mkaipeleleza nchi.” Wale watu walikwea na kuipeleleza Ai.
Car Josué envoya de Jérico des hommes vers Haï, qui [était] près de Bethaven du côté de l'Orient de Béthel, et leur parla, en disant: Montez, et reconnaissez le pays. Ces hommes donc montèrent et reconnurent Haï.
3 Waliporudi kwa Yoshua, walimwambia, “Usitume watu wote kwenda Ai. Tuma tu watu elfu mbili au elfu tatu waende kuiteka Ai. Usiwafanye watu wateseke katika vita, kwani ni watu wachache.”
Et étant retournés vers Josué, ils lui dirent: Que tout le peuple n'y monte point [mais qu']environ deux mille ou trois mille hommes y montent, et ils battront Haï. Ne fatigue point tout le peuple [en l'envoyant] là; car ils sont peu de gens.
4 Hivyo ni watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi ndio walioenda, lakini watu hawa waliwakimbia watu wa Ai.
Ainsi environ trois mille hommes du peuple y montèrent, mais ils s'enfuirent de devant ceux de Haï.
5 Watu wa Ai waliwaua watu wapatao thelathini na sita, waliwafuata katika lango la mji hadi katika machimbo ya mawe, na waliwauwa walipokuwa wakishuka katika kilima. Na mioyo ya watu ilijawa hofu na ujasiri wao ukawatoka.
Et ceux de Haï en tuèrent environ trente-six hommes; car ils les poursuivirent depuis le devant de la porte jusqu'à Sébarim, et les battirent en une descente; et le cœur du peuple se fondit, et devint comme de l'eau.
6 Basi Yoshua alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh, na walibaki pale mpaka jioni.
Alors Josué déchira ses vêtements, et se jeta, le visage contre terre, devant l'Arche de l'Eternel, jusqu'au soir, lui et les Anciens d'Israël, et ils jetèrent de la poudre sur leur tête.
7 Kisha Yoshua akasema, “Oo, Yahweh Bwana, kwanini umewavusha watu hawa ng'ambo ya Yordani? Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza? ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti na tungekaa katika upande mwingine wa Yordani!
Et Josué dit: Hélas! Seigneur Eternel, pourquoi as-tu fait [si magnifiquement] passer le Jourdain à ce peuple, pour nous livrer entre les mains de l'Amorrhéen, [et] nous faire périr? Ô que n'avons-nous eu dans l'esprit [de demeurer], et que ne sommes-nous demeurés au delà du Jourdain!
8 Bwana, niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao?
Hélas! Seigneur, que dirai-je, puisque Israël a tourné le dos devant ses ennemis?
9 Kwa kuwa Wakaanani na wenyeji wote wa nchi watakaposikia, watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu. Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?
Les Cananéens et tous les habitants du pays l'entendront, et nous envelopperont, et ils retrancheront notre nom de dessus la terre; et que feras-tu à ton grand Nom?
10 Yahweh akamwambia Yoshua, “Inuka! kwanini umelala kifudifudi?
Alors l'Eternel dit à Josué: Lève-toi; pourquoi te jettes-tu ainsi le visage [contre terre]?
11 Israeli imetenda dhambi. Wamevunja agano langu nililowaagiza. Wameiba baadhi ya vitu vilivyokuwa vimetengwa. Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao kwa kuweka vitu vile walivyochukua miongoni mwa mali zao wenyewe.
Israël a péché; ils ont transgressé mon alliance que je leur avais commandée, même ils ont pris de l'interdit; même ils [en] ont dérobé; même ils ont menti, et même ils l'ont mis dans leurs hardes.
12 Na matokeo yake ni kwamba watu wa Israeli hawataweza kusimama mbele za maadui zao. Walitega migongo yao kwa maadui zao kwasababu wao wenyewe wametengwa kwa ajili ya uharibifu. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka pale mtakapoteketeza vitu vile vilivyotakiwa kuharibiwa, lakini sasa bado viko miongoni mwenu.
C'est pourquoi les enfants d'Israël ne pourront subsister devant leurs ennemis; ils tourneront le dos devant leurs ennemis; car ils sont devenus un interdit. Je ne serai plus avec vous si vous n'exterminez d'entre vous l'interdit.
13 Inuka! Waweke watu wakfu kwangu, na uwaambie, 'Jiwekeeni wakfu ninyi wenyewe kesho. Kwa kuwa, Yahweh, Mungu wa Israeli asema hivi, “Kuna vitu vilitengwa ili kuteketezwa ambavyo bado viko miongoni mwenu, Israeli. Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu mpaka pale mtakapoviondoa miongoni mwenu vitu vyote ambavyo vilitengwa kwa ajili ya kuteketezwa.”
Lève-toi; sanctifie le peuple, et dis: Sanctifiez-vous pour demain; car ainsi a dit l'Eternel le Dieu d'Israël; il y a de l'interdit parmi toi, ô Israël! tu ne pourras subsister devant tes ennemis jusqu'à ce que vous ayez ôté l'interdit d'entre vous.
14 Asubuhi, mtajisogeza wenyewe kwa makabila. Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake. Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba. Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja.
Vous vous approcherez donc le matin selon vos Tribus; et la Tribu que l'Eternel aura saisie s'approchera selon les familles; et la famille que l'Eternel aura saisie s'approchera selon les maisons; et la maison que l'Eternel aura saisie, s'approchera selon les têtes.
15 Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa na aliye navyo vitu hivyo vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, atachomwa moto, yeye na kila kitu alichonacho, kwasababu amelivunja agano la Yahweh na kwasababu amefanya jambo la aibu katika Israeli.'”
Alors celui qui aura été saisi en l'interdit, sera brûlé au feu, lui et tout ce qui [est] à lui; à cause qu'il a transgressé l'alliance de l'Eternel, et qu'il a commis une infamie en Israël.
16 Basi, Yoshua aliamka asubuhi na mapema na aliwaleta Israeli karibu, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda lilichaguliwa.
Josué donc se leva de bon matin, et fit approcher Israël selon ses Tribus; et la Tribu de Juda fut saisie.
17 Yoshua akazisogeza koo za Yuda karibu, na ukoo wa Zera ulichaguliwa. Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu, na Zabdi alichaguliwa.
Puis il fit approcher les familles de Juda, et il saisit la famille de ceux qui étaient descendus de Zara. Puis il fit approcher par têtes la famille de ceux qui étaient descendus de Zara, et Zabdi fut saisi.
18 Akaisogeza karibu nyumba ya Zabdi mtu kwa mtu, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka kabila la Yuda, alichaguliwa.
Et quand il eut fait approcher sa maison par têtes, Hacan fils de Carmi, fils de Zabdi, fils de Zara, de la Tribu de Juda, fut saisi.
19 Kisha Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, niambie ukweli mbele za Yahweh, Mungu wa Israel, na ufanye ukiri wako kwake. Tafadhali niambie kile ulichofanya. Usinifiche.”
Alors Josué dit à Hacan: Mon fils, donne, je te prie, gloire à l'Eternel le Dieu d'Israël, et fais-lui confession; et déclare-moi, je te prie, ce que tu as fait; ne me le cache point.
20 Akani akamjibu Yoshua, “Kwa kweli nimetenda dhambi mbele Yahweh, Mungu wa Israeli.
Et Hacan répondit à Josué, et dit: J'ai péché, il est vrai, contre l'Eternel le Dieu d'Israël, et j'ai fait telle et telle chose.
21 Nilichofanya ni hiki: Nilipoona miongoni mwa nyara mkoti mzuri kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kipande cha dhahabu chenye uzito wa shekeli hamsini, nilivitamani na nikavichukua. Vimefichwa chini ardhini katikati ya hema langu, na fedha iko chini yake.”
J'ai vu parmi le butin un beau manteau de Sinhar, deux cents sicles d'argent, et un lingot d'or du poids de cinquante sicles; je les ai convoités, [je les ai] pris; et voilà ces choses [sont] cachées en terre au milieu de ma tente, et l'argent est sous le manteau.
22 Yoshua akatuma wajumbe waliokimbia mpaka kwenye hema mahali palipokuwa na vile vitu. Walipoangalia, waliviona vimefichwa katika hema lake, na fedha chini yake.
Alors Josué envoya des messagers qui coururent à cette tente; et voici le manteau était caché dans la tente d'Hacan, et l'argent sous le manteau.
23 Walivichukua vitu hivyo kutoka katikati ya hema na kuvileta kwa Yoshua na watu wote wa Israeli. Walivimwaga mbele za Yahweh.
Ils les prirent donc du milieu de la tente, et les apportèrent à Josué, et à tous les enfants d'Israël, et ils les déployèrent devant l'Eternel.
24 Kisha Yoshua na Waisraeli wote pamoja naye, walimchukua Akani mwana wa Zera, na fedha, na koti, na kipande cha dhahabu, wana na binti zake, ng'ombe zake, punda zake, kondoo zake, hema lake, na kila kitu alichokuwa nacho, na wakavileta hata bonde la Akori.
Alors Josué et tout Israël avec lui, prenant Hacan fils de Zara, et l'argent, et le manteau, et le lingot d'or, et ses fils, et ses filles, et ses bœufs, et ses ânes, et ses brebis, et sa tente, et tout ce qui [était] à lui, les firent venir en la vallée de Hacor.
25 Kisha Yoshua akasema, “Kwanini umetusumbua? Leo Yahweh atakutesa na wewe.” Waisraeli wote wakampiga kwa mawe. Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe.
Et Josué dit: Pourquoi nous as-tu troublés? l'Eternel te troublera aujourd'hui. Et tous les Israélites l'assommèrent de pierres, et les brûlèrent au feu, après les avoir assommés de pierres.
26 Kisha wakaweka juu yake kichuguu kikubwa cha mawe ambayo yapo hata leo. Yahweh akaachilia mbali hasira yake. Hivyo basi, jina la mahali hapo likawa Akori hata leo.
Et ils dressèrent sur lui un grand monceau de pierres, [qui dure] jusqu'à ce jour. Et l'Eternel apaisa l'ardeur de sa colère; c'est pourquoi ce lieu-là a été appelé jusqu'à aujourd'hui, la vallée de Hacor.

< Yoshua 7 >