< Yoshua 7 >

1 Lakini watu wa Israeli hawakutenda katika uaminifu kuhusiana na vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu. Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka katika kabila la Yuda, alivitwaa baadhi ya vitu hivyo vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya uharibifu, na hasira ya Yahweh iliwaka juu yawatu wa Israeli.
And they acted unfaithfully [the] people of Israel unfaithfulness in the devoted thing[s] and he took Achan [the] son of Carmi [the] son of Zabdi [the] son of Zerah of [the] tribe of Judah some of the devoted thing[s] and it burned [the] anger of Yahweh on [the] people of Israel.
2 Yoshua alituma watu kutoka Yeriko kwenda Ai, mji uliokuwa karibu na Bethi Aveni, mashariki mwa Betheli. Aliwaambia, “Nendeni na mkaipeleleza nchi.” Wale watu walikwea na kuipeleleza Ai.
And he sent Joshua men from Jericho Ai which [is] beside Beth Aven from [the] east of Beth-el and he said to them saying go up and spy out the land and they went up the men and they spied out Ai.
3 Waliporudi kwa Yoshua, walimwambia, “Usitume watu wote kwenda Ai. Tuma tu watu elfu mbili au elfu tatu waende kuiteka Ai. Usiwafanye watu wateseke katika vita, kwani ni watu wachache.”
And they returned to Joshua and they said to him may not it go up all the people about two thousand man or about three thousand man let them go up and they may attack Ai may not you make go wearily there towards all the people for [are] few they.
4 Hivyo ni watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi ndio walioenda, lakini watu hawa waliwakimbia watu wa Ai.
And they went up some of the people there about three thousand man and they fled before [the] men of Ai.
5 Watu wa Ai waliwaua watu wapatao thelathini na sita, waliwafuata katika lango la mji hadi katika machimbo ya mawe, na waliwauwa walipokuwa wakishuka katika kilima. Na mioyo ya watu ilijawa hofu na ujasiri wao ukawatoka.
And they struck down of them [the] men of Ai about thirty and six man and they pursued them before the gate to Shebarim and they struck down them at the descent and it melted [the] heart of the people and it became water.
6 Basi Yoshua alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh, na walibaki pale mpaka jioni.
And he tore Joshua clothes his and he fell on face his [the] ground towards before [the] ark of Yahweh until the evening he and [the] elders of Israel and they made go up dust on head their.
7 Kisha Yoshua akasema, “Oo, Yahweh Bwana, kwanini umewavusha watu hawa ng'ambo ya Yordani? Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza? ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti na tungekaa katika upande mwingine wa Yordani!
And he said Joshua alas! - O Lord Yahweh why? have you brought over at all the people this the Jordan to give us in [the] hand of the Amorite[s] to destroy us and if we had been willing and we had remained on [the] other side of the Jordan.
8 Bwana, niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao?
Pardon me O Lord what? will I say after that it has turned Israel a neck before enemies its.
9 Kwa kuwa Wakaanani na wenyeji wote wa nchi watakaposikia, watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu. Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?
And they may hear the Canaanite[s] and all [the] inhabitants of the land and they will surround us and they will cut off name our from the earth and what? will you do for name your great.
10 Yahweh akamwambia Yoshua, “Inuka! kwanini umelala kifudifudi?
And he said Yahweh to Joshua stand up for yourself why? this [are] you falling on face your.
11 Israeli imetenda dhambi. Wamevunja agano langu nililowaagiza. Wameiba baadhi ya vitu vilivyokuwa vimetengwa. Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao kwa kuweka vitu vile walivyochukua miongoni mwa mali zao wenyewe.
It has sinned Israel and also they have transgressed covenant my which I commanded them and also they have taken some of the devoted thing[s] and also they have stolen and also they have deceived and also they have put [them] among things their.
12 Na matokeo yake ni kwamba watu wa Israeli hawataweza kusimama mbele za maadui zao. Walitega migongo yao kwa maadui zao kwasababu wao wenyewe wametengwa kwa ajili ya uharibifu. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka pale mtakapoteketeza vitu vile vilivyotakiwa kuharibiwa, lakini sasa bado viko miongoni mwenu.
And not they are able [the] people of Israel to stand before enemies their a neck they turn before enemies their for they have become a devoted thing not I will repeat to be with you if not you will destroy the devoted thing[s] from midst your.
13 Inuka! Waweke watu wakfu kwangu, na uwaambie, 'Jiwekeeni wakfu ninyi wenyewe kesho. Kwa kuwa, Yahweh, Mungu wa Israeli asema hivi, “Kuna vitu vilitengwa ili kuteketezwa ambavyo bado viko miongoni mwenu, Israeli. Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu mpaka pale mtakapoviondoa miongoni mwenu vitu vyote ambavyo vilitengwa kwa ajili ya kuteketezwa.”
Arise consecrate the people and you will say consecrate yourselves for tomorrow for thus he says Yahweh [the] God of Israel devoted thing[s] [are] in midst your O Israel not you will be able to stand before enemies your until remove you the devoted thing[s] from midst your.
14 Asubuhi, mtajisogeza wenyewe kwa makabila. Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake. Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba. Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja.
And you will bring yourselves near in the morning to tribes your and it will be the tribe which he will take it Yahweh it will draw near to the families and the family which he will take it Yahweh it will draw near to the households and the household which he will take it Yahweh it will draw near to the men.
15 Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa na aliye navyo vitu hivyo vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, atachomwa moto, yeye na kila kitu alichonacho, kwasababu amelivunja agano la Yahweh na kwasababu amefanya jambo la aibu katika Israeli.'”
And it will be the [one who] is taken by lot with the devoted thing[s] he will be burned with fire him and all that [belongs] to him for he has transgressed covenant of Yahweh and for he has done disgraceful folly in Israel.
16 Basi, Yoshua aliamka asubuhi na mapema na aliwaleta Israeli karibu, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda lilichaguliwa.
And he rose early Joshua in the morning and he brought near Israel to tribes its and it was taken by lot [the] tribe of Judah.
17 Yoshua akazisogeza koo za Yuda karibu, na ukoo wa Zera ulichaguliwa. Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu, na Zabdi alichaguliwa.
And he brought near [the] family of Judah and he took [the] family of the Zerahite[s] and he brought near [the] family of the Zerahite[s] to the men and he was taken by lot Zabdi.
18 Akaisogeza karibu nyumba ya Zabdi mtu kwa mtu, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka kabila la Yuda, alichaguliwa.
And he brought near household his to the men and he was taken by lot Achan [the] son of Carmi [the] son of Zabdi [the] son of Zerah of [the] tribe of Judah.
19 Kisha Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, niambie ukweli mbele za Yahweh, Mungu wa Israel, na ufanye ukiri wako kwake. Tafadhali niambie kile ulichofanya. Usinifiche.”
And he said Joshua to Achan O son my put please glory to Yahweh [the] God of Israel and give to him confession and tell please to me what? have you done may not you hide [it] from me.
20 Akani akamjibu Yoshua, “Kwa kweli nimetenda dhambi mbele Yahweh, Mungu wa Israeli.
And he answered Achan Joshua and he said truly I I have sinned to Yahweh [the] God of Israel and like this and like this I have done.
21 Nilichofanya ni hiki: Nilipoona miongoni mwa nyara mkoti mzuri kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kipande cha dhahabu chenye uzito wa shekeli hamsini, nilivitamani na nikavichukua. Vimefichwa chini ardhini katikati ya hema langu, na fedha iko chini yake.”
(And I saw *Q(k)*) among the booty cloak of Shinar one good and two hundred shekels silver and a wedge of gold one [was] fifty shekels weight its and I desired them and I took them and there they [are] hidden in the ground in [the] midst of tent my and the silver [is] under it.
22 Yoshua akatuma wajumbe waliokimbia mpaka kwenye hema mahali palipokuwa na vile vitu. Walipoangalia, waliviona vimefichwa katika hema lake, na fedha chini yake.
And he sent Joshua messengers and they ran the tent towards and there! [it was] hidden in tent his and the silver [was] under it.
23 Walivichukua vitu hivyo kutoka katikati ya hema na kuvileta kwa Yoshua na watu wote wa Israeli. Walivimwaga mbele za Yahweh.
And they took them from [the] midst of the tent and they brought them to Joshua and to all [the] people of Israel and they poured out them before Yahweh.
24 Kisha Yoshua na Waisraeli wote pamoja naye, walimchukua Akani mwana wa Zera, na fedha, na koti, na kipande cha dhahabu, wana na binti zake, ng'ombe zake, punda zake, kondoo zake, hema lake, na kila kitu alichokuwa nacho, na wakavileta hata bonde la Akori.
And he took Joshua Achan [the] son of Zerah and the silver and the cloak and [the] wedge of gold and sons his and daughters his and ox[en] his and donkey[s] his and sheep his and tent his and all that [belonged] to him and all Israel with him and they brought up them [the] valley of Achor.
25 Kisha Yoshua akasema, “Kwanini umetusumbua? Leo Yahweh atakutesa na wewe.” Waisraeli wote wakampiga kwa mawe. Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe.
And he said Joshua why? have you brought trouble to us he will bring trouble to you Yahweh on the day this and they stoned him all Israel stone[s] and they burned them with fire and they stoned them with stones.
26 Kisha wakaweka juu yake kichuguu kikubwa cha mawe ambayo yapo hata leo. Yahweh akaachilia mbali hasira yake. Hivyo basi, jina la mahali hapo likawa Akori hata leo.
And they set up over him a heap of stones great until the day this and he turned back Yahweh from [the] burning of anger his there-fore someone called [the] name of the place that [the] valley of Achor until the day this.

< Yoshua 7 >