< Yoshua 7 >
1 Lakini watu wa Israeli hawakutenda katika uaminifu kuhusiana na vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu. Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka katika kabila la Yuda, alivitwaa baadhi ya vitu hivyo vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya uharibifu, na hasira ya Yahweh iliwaka juu yawatu wa Israeli.
But the sons of Israel transgressed the commandment, and they usurped what was anathema. For Achan, the son of Carmi, the son of Zabdi, the son of Zerah, from the tribe of Judah, took something from what was anathema. And the Lord became angry against the sons of Israel.
2 Yoshua alituma watu kutoka Yeriko kwenda Ai, mji uliokuwa karibu na Bethi Aveni, mashariki mwa Betheli. Aliwaambia, “Nendeni na mkaipeleleza nchi.” Wale watu walikwea na kuipeleleza Ai.
And when Joshua sent men from Jericho against Ai, which is beside Bethaven, toward the eastern region of the town of Bethel, he said to them, “Go up and explore the land.” And they fulfilled his instruction, and they explored Ai.
3 Waliporudi kwa Yoshua, walimwambia, “Usitume watu wote kwenda Ai. Tuma tu watu elfu mbili au elfu tatu waende kuiteka Ai. Usiwafanye watu wateseke katika vita, kwani ni watu wachache.”
And returning, they said to him: “Let not the entire people go up. Instead, let two or three thousand men go out and destroy the city. Why should all the people be troubled without cause against enemies that are so very few?”
4 Hivyo ni watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi ndio walioenda, lakini watu hawa waliwakimbia watu wa Ai.
Therefore, they went up with three thousand fighters. And they promptly turned their backs,
5 Watu wa Ai waliwaua watu wapatao thelathini na sita, waliwafuata katika lango la mji hadi katika machimbo ya mawe, na waliwauwa walipokuwa wakishuka katika kilima. Na mioyo ya watu ilijawa hofu na ujasiri wao ukawatoka.
and were struck down by the men of the city of Ai. And thirty-six men of them fell. And the adversaries pursued them from the gate, even as far as Shebarim. And they felled them as they were fleeing downward. And the heart of the people was struck with fear, and it melted like water.
6 Basi Yoshua alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh, na walibaki pale mpaka jioni.
And truly, Joshua tore his garments, and he fell prone on the ground before the ark of the Lord, even until evening, both he and all the elders of Israel. And they cast dust upon their heads.
7 Kisha Yoshua akasema, “Oo, Yahweh Bwana, kwanini umewavusha watu hawa ng'ambo ya Yordani? Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza? ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti na tungekaa katika upande mwingine wa Yordani!
And Joshua said: “Alas, O Lord God! Why would you want to lead this people over the river Jordan, so that you might deliver us into the hand of the Amorite and destroy us? I wish that we had remained beyond the Jordan, as when we began.
8 Bwana, niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao?
My Lord God, what shall I say, seeing Israel turning their backs to their enemies?
9 Kwa kuwa Wakaanani na wenyeji wote wa nchi watakaposikia, watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu. Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?
The Canaanites and all the inhabitants of the land will hear of it, and coming together as one, they will surround us, and they will wipe our name from the earth. And what will you do concerning your great name?”
10 Yahweh akamwambia Yoshua, “Inuka! kwanini umelala kifudifudi?
And the Lord said to Joshua: “Rise up. Why are you lying flat on the ground?
11 Israeli imetenda dhambi. Wamevunja agano langu nililowaagiza. Wameiba baadhi ya vitu vilivyokuwa vimetengwa. Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao kwa kuweka vitu vile walivyochukua miongoni mwa mali zao wenyewe.
Israel has sinned and transgressed my covenant. And they have taken from what is anathema. And they have stolen and lied, and they have hidden it among their goods.
12 Na matokeo yake ni kwamba watu wa Israeli hawataweza kusimama mbele za maadui zao. Walitega migongo yao kwa maadui zao kwasababu wao wenyewe wametengwa kwa ajili ya uharibifu. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka pale mtakapoteketeza vitu vile vilivyotakiwa kuharibiwa, lakini sasa bado viko miongoni mwenu.
Israel is not able to stand before his enemies, and he will flee from them. For he has been defiled by what is anathema. I will no longer be with you, until you destroy him who is guilty of this wickedness.
13 Inuka! Waweke watu wakfu kwangu, na uwaambie, 'Jiwekeeni wakfu ninyi wenyewe kesho. Kwa kuwa, Yahweh, Mungu wa Israeli asema hivi, “Kuna vitu vilitengwa ili kuteketezwa ambavyo bado viko miongoni mwenu, Israeli. Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu mpaka pale mtakapoviondoa miongoni mwenu vitu vyote ambavyo vilitengwa kwa ajili ya kuteketezwa.”
Rise up. Sanctify the people. And you shall say to them: ‘Be sanctified tomorrow. For thus says the Lord, the God of Israel: That which is anathema is in your midst, O Israel! You are not able to stand before your enemies, until he who has been contaminated by this wickedness is taken away from you.’
14 Asubuhi, mtajisogeza wenyewe kwa makabila. Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake. Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba. Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja.
And you shall draw near in the morning, each one by your tribes. And whichever tribe will be found by lot shall come forward by its families, and the families by houses, and the house by the men.
15 Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa na aliye navyo vitu hivyo vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, atachomwa moto, yeye na kila kitu alichonacho, kwasababu amelivunja agano la Yahweh na kwasababu amefanya jambo la aibu katika Israeli.'”
And whoever he may be that will be found guilty of this deed, he shall be burnt with fire with all his substance. For he transgressed the covenant of the Lord, and he committed a wicked act in Israel.”
16 Basi, Yoshua aliamka asubuhi na mapema na aliwaleta Israeli karibu, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda lilichaguliwa.
And so Joshua, rising in the morning, brought forth Israel by their tribes, and the tribe of Judah was found.
17 Yoshua akazisogeza koo za Yuda karibu, na ukoo wa Zera ulichaguliwa. Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu, na Zabdi alichaguliwa.
And when its families had been presented, the family of Zerah was found. Likewise, bringing that one forward by the houses, he discovered Zabdi.
18 Akaisogeza karibu nyumba ya Zabdi mtu kwa mtu, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka kabila la Yuda, alichaguliwa.
And dividing his house by each man, he found Achan, the son of Carmi, the son of Zabdi, the son of Zerah, from the tribe of Judah.
19 Kisha Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, niambie ukweli mbele za Yahweh, Mungu wa Israel, na ufanye ukiri wako kwake. Tafadhali niambie kile ulichofanya. Usinifiche.”
And Joshua said to Achan: “My son, give glory to the Lord, the God of Israel, and confess, and reveal to me what you have done. You may not conceal it.”
20 Akani akamjibu Yoshua, “Kwa kweli nimetenda dhambi mbele Yahweh, Mungu wa Israeli.
And Achan responded to Joshua, and he said to him: “Truly, I have sinned against the Lord, the God of Israel, and I have done one thing and another.
21 Nilichofanya ni hiki: Nilipoona miongoni mwa nyara mkoti mzuri kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kipande cha dhahabu chenye uzito wa shekeli hamsini, nilivitamani na nikavichukua. Vimefichwa chini ardhini katikati ya hema langu, na fedha iko chini yake.”
For I saw among the spoils a very fine scarlet cloak, and two hundred shekels of silver, and a gold bar of fifty shekels. And coveting these, I took and hid them in the ground near the middle of my tent, and I covered the silver with the soil that I had dug.”
22 Yoshua akatuma wajumbe waliokimbia mpaka kwenye hema mahali palipokuwa na vile vitu. Walipoangalia, waliviona vimefichwa katika hema lake, na fedha chini yake.
Therefore, Joshua sent ministers, who, running to his tent, discovered everything hidden in the same place, together with the silver.
23 Walivichukua vitu hivyo kutoka katikati ya hema na kuvileta kwa Yoshua na watu wote wa Israeli. Walivimwaga mbele za Yahweh.
And taking these from the tent, they brought them to Joshua, and to all the sons of Israel, and they cast them down before the Lord.
24 Kisha Yoshua na Waisraeli wote pamoja naye, walimchukua Akani mwana wa Zera, na fedha, na koti, na kipande cha dhahabu, wana na binti zake, ng'ombe zake, punda zake, kondoo zake, hema lake, na kila kitu alichokuwa nacho, na wakavileta hata bonde la Akori.
And so Joshua took Achan, the son of Zerah, and the silver, and the cloak, and the gold bar, also his sons and daughters, the oxen and donkeys and sheep, and even the tent and all his goods, (and all of Israel went with him, ) and he brought these to the valley of Achor.
25 Kisha Yoshua akasema, “Kwanini umetusumbua? Leo Yahweh atakutesa na wewe.” Waisraeli wote wakampiga kwa mawe. Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe.
There, Joshua said: “Because you have troubled us, the Lord troubles you, on this day.” And all of Israel stoned him. And all the things that were his were consumed by fire.
26 Kisha wakaweka juu yake kichuguu kikubwa cha mawe ambayo yapo hata leo. Yahweh akaachilia mbali hasira yake. Hivyo basi, jina la mahali hapo likawa Akori hata leo.
And they gathered upon him a great pile of stones, which remains even to the present day. And the fury of the Lord was averted from them. And the name of that place was called the Valley of Achor, even to this day.