< Yoshua 6 >

1 Basi, milango yote ya Yeriko ilikuwa imefungwa kwasababu ya jeshi la Israeli. Hapakuwa na mtu wa kutoka nje au kuingia ndani.
Now, Jericho, was shut up and barred because of the sons of Israel, —none came out and none went in.
2 Yahweh akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeweka Yeriko katika mkono wako, mfalme wake pamoja na wanajeshi wake waliofunzwa.
Then said Yahweh unto Joshua, See, I have delivered, into thy hand, Jericho and her king, —the mighty men of valour.
3 Ni lazima kutembea kwa kuuzunguka mji, wanaume wote wa vita wauzunguke mji mara moja. Ni lazima mfanye hivi kwa siku sita.
So then ye shall compass the city all ye men of war, going round the city, once, —thus, shall thou do six days.
4 Makuhani saba lazima wabebe tarumbeta za pembe za kondoo waume mbele za sanduku. Na katika siku ya saba, ni lazima mtembee kwa kuuzunguka mji mara saba, na makuhani lazima wapulize tarumbeta.
And, seven priests, shall bear the seven rams’ horns before the ark, and, on the seventh day, shall ye compass the city seven times, —and, the priests, shall blow with the horns.
5 Kisha watapuliza pembe za kondoo waume kwa nguvu kuu, na mtakaposikia sauti za tarumbeta watu wote na wapige kelele kwa mshindo mkuu, na ukuta wa mji utaanguka chini pale pale. Wanajeshi ni lazime washambulie, kila mmoja eende mbele moja kwa moja.
And it shall come to pass, when the ram’s horn soundeth, when ye hear the sound of the horn, that all the people shall shout with a great shout, —and then shall the wall of the city fall down under it, and the people shall go up, every man straight before him.
6 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni, aliwaita makuhani na kuwaambia, “Lichukueni sanduku la agano, na waacheni makuhani saba wabebe tarumbeta za pembe za kondoo waume mbele ya sanduku la Yahweh.”
Then called Joshua son of Nun unto the priests, and said unto them, Bear ye the ark of the covenant, —and let, seven priest, bear seven rams horns, before the ark of Yahweh.
7 Yoshua aliwaambia watu, “Nendeni na mkatembee kuuzunguka mji, na watu wa vita wataenda mbele ya sanduku la Yahweh.”
Then said he unto the people, Pass on and compass the city, —and let, the armed host, pass on before the ark of Yahweh.
8 Makuhani saba walibeba tarumbeta saba za pembe za kondoo mbele ya Yahweh kama Yoshua alivyowaambia watu. Na walivyokuwa akiendelea mbele, walipuliza tarumbeta.
And it was so, when Joshua had spoken unto the people, that, the seven priests who were bearing the seven rams’ horns before Yahweh, passed on and blew with the horns, —the ark of the covenant of Yahweh also coming after them.
9 Sanduku la Yahweh liliwafuata kwa nyuma yao. Watu wa vita walitembea mbele ya makuhani, na walipuliza tarumbeta zao, lakini walinzi wa nyuma walilifuata sanduku kwa nyuma, na makuhani waliendelea kupuliza tarumbeta zao.
And, the armed host, went on before the priests who blew with the horns, —and, the rear-guard, came after the ark, going on and blowing with the horns.
10 Lakini Yoshua aliwaagiza watu, akisema, “Msipige kelele. Sauti yoyote isitoke vinywani mwenu mpaka siku nitakayowaambia kupiga kelele. Ndipo hapo mtakapopiga kelele.”
Now, unto the people, had Joshua given command, saying—Ye shall not shout nor let your voice be heard, neither shall there go out of your mouth, a word, —until the day when I say unto you Shout! then shall ye shout.
11 Hivyo, alisababisha sanduku la Yahweh kuuzunguka mji mara moja kwa siku hiyo. Kisha wakaingia katika kambi yao, wakakaa usiku ule katika kambi.
So he caused the ark of Yahweh to compass the city, going round once, —and they came into the camp, and lodged in the camp.
12 Basi Yoshua aliamka asubuhi na mapema, na makuhani wakalichukua sanduku la Yahweh.
And Joshua rose early in the morning, —and the priests bare the ark of Yahweh;
13 Makuhani saba waliobeba tarumbeta saba za pembe za kondoo waume walikuwa mbele ya sanduku la Yahweh, wakitembea kwa ushupavu, huku wakipuliza tarumbeta. Wanajeshi wenye silaha walikuwa wakitembea mbele yao, lakini walinzi wa nyuma walitembea nyuma ya sanduku la Yahweh, huku tarumbeta ziliendelea kupigwa.
and, the seven priests who bare the seven rams’ horns before the ark of Yahweh, went on and on, and blew with the horns, —with, the armed host going on before them, and, the rear-guard, coming after the ark of Yahweh, going on and blowing with the horns.
14 Walitembea kuuzunguka mji mara moja katika siku ya pili na kisha wakarudi kambini. Walifanya hivi kwa siku sita.
So they compassed the city on the second day once, and returned into the camp, —thus, did they, six days.
15 Ilikuwa ni katika siku ya saba ambayo waliamka mapema katika mapambazuko, na walitembea kuuzunguka mji kwa namna ile kama ilivyokuwa kawaida yao, katika siku hii walifanya mara saba.
And it came to pass, on the seventh day, that they rose early at the uprisings of the dawn, and compassed the city after this manner, seven times, —only on that day they compassed the city seven times.
16 Ilikuwa ni katika siku ya saba ambapo makuhani walipiga tarumbeta, na ya kwamba Yoshua aliwaagiza watu, “Pigeni kelele! Kwa kuwa Yahweh amewapa ninyi mji.
And it came to pass, at the seventh time—when the priests blew with the horns, then did Joshua say unto the people—Shout, for Yahweh hath delivered unto you the city.
17 Mji pamoja na vitu vyote ndani yake vitatengwa kwa Yahweh kwa ajili ya uharibifu. Ni Rahabu yule kahaba pekee ataishi - yeye pamoja wote waliokuwa pamoja naye katika nyumba - kwasababu aliwaficha watu tuliowatuma.
And it shall be, that, as for the city, devoted, shall it be and all that is therein unto Yahweh, —nevertheless, Rahab the harlot, shall live, she and all who are with her in the house, because she hid the messengers whom we sent.
18 Lakini kwenu, iweni waangalifu juu ya kuchukua vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu, ili baada ya kuvitia alama kwa ajili ya kuharibiwa, msichukue hata kimoja wapo. Na kama mtafanya hivi, mtaifanya kambi ya Waisraeli iharibiwe na mtaleta matatizo katika kambi.
But, in any wise, do, ye, beware of what is devoted, lest ye should covet, and then take of what is devoted, —and so cause the camp of Israel to be devoted, and bring trouble upon it.
19 Fedha zote, dhahabu na vitu vilivyotengenezwa kwa shaba na chuma vilitengwa kwa ajli ya Yahweh.”
But, as for all silver and gold and vessels of bronze and iron, hallowed, it is to Yahweh, —unto the treasury of Yahweh, shall it come.
20 Hivyo, watu wakapiga kelele, na wakatoa sauti kwa kupuliza tarumbeta. Ilikuwa watu waliposikia sauti za tarumbeta, walipiga kelele kwa sauti kuu, na ukuta ulianguka chini kabisa na kwamba watu waliungia mji, kila mmoja alisonga mbele moja kwa moja. Na waliuteka mji.
So the people shouted, when the horns were blown, —yea it came to pass, when the people heard the sound of the horn, that the people shouted with a great shout, and the wall fell down under it, and the people went up into the city every man straight before him, and so they captured the city.
21 Waliteketeza kabisa kila kitu kilichokuwa katika mji kwa makali ya upanga - wanaume kwa wanawake, wadogo kwa wakubwa, ng'ombe, kondoo na punda.
And they devoted all that were in the city, both man and woman, both young and old, —and ox and sheep and ass, with the edge of the sword.
22 Kisha Yoshua akawaambia wale watu wawili walioipeleleza nchi, “Nendeni katika nyumba ya kahaba, mtoeni mwanamke na wote walio pamoja naye, kama mlivyomwapia.”
But, unto the two men who spied out the land, Joshua said, Go into the house of the woman, the harlot, —and bring out thence the woman and all that she hath, as ye aware unto her.
23 Basi, vijana wale walioipeleleza nchi waliingia ndani na kumtoa Rahabu nje. Walimtoa nje baba yake, mama, kaka, na ndugu wote waliokuwa pamoja naye. waliwaleta katika sehemu ya nje ya kambi ya Waisraeli.
So the young men the spies went in and brought out Rahab and her father and her mother and her brethren and all that she had, yea, all her kindred, brought they out, —and set them outside the camp of Israel.
24 Na ndipo waliuteketeza mji na kila kitu ndani yake. Isipokuwa fedha, dhahabu na vyombo vya fedha na chuma viliwekwa kwa hazina ya nyumba ya Yahweh.
But, the city, burned they with fire, and all that was therein, —save only, the silver and the gold and the vessels of bronze and of iron, put they into the treasury of the house of Yahweh.
25 Bali Yoshua alimruhusu Rahabu kahaba, nyumba ya baba yake, na wote waliokuwa pamoja naye waishi. Mpaka leo hivi anaishi Israeli kwasababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko.
And, Rahab the harlot and the household of her father and all that she had, did Joshua save alive, so she hath dwelt in the midst of Israel until this day, —because she hid the messengers whom Joshua sent to spy out Jericho.
26 Kisha katika kipindi hicho, Yoshua aliwaamuru kwa kiapo na kusema, “Alaaniwe machoni pa Yahweh mtu yule anayeujenga mji huu, Yeriko. Ataujenga msingi kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza, na kwa gharama ya mzaliwa wake wa pili atapachika milango yake.”
And Joshua imposed an oath at that time, saying, —Cursed be the man before Yahweh who shall raise up and build this city—Jericho, At the price of his firstborn, shall he lay its foundation, and, at the price of his youngest, shall he set up its doors.
27 Basi Yahweh alikuwa pamoja na Yoshua, na umaarufu wake ulienea katika nchi yote.
And so it was that Yahweh was with Joshua, —and his fame was in all the land.

< Yoshua 6 >