< Yoshua 5 >

1 Mara tu waliposikia wafalme wa Waamori walio upande wa magharibi wa Yordani, na wafalme wote wa Wakanaani waliokuwa katika pwani ya Ziwa kuu, waliposikia ya kwamba Yahweh alikuwa ameyakausha maji ya Yordani mpaka pale waisraeli wote walipomaliza kuvuka, mioyo yao ikayeyuka, na hapakuwa na moyo wowote ndani yao kwa sababu ya watu wa Israeli.
Nowe when all the Kings of the Amorites, which were beyond Iorden Westward, and all the Kinges of the Canaanites which were by the Sea, heard that the Lord had dried vp the waters of Iorden before the children of Israel vntill they were gone ouer, their heart fainted: and there was no courage in them any more because of the children of Israel.
2 Kwa wakati huo Yahweh alimwambia Yoshua, “Tengenezeni visu vya mawe na mara moja mwatahiri wanaume wote wa Israeli.”
That same time the Lord said vnto Ioshua, Make thee sharpe kniues, and returne, and circumcise the sonnes of Israel the second time.
3 Kisha Yoshua alijifanyia visu vya mawe na akawatahiri wanaume wote wa Gibea Haaraloti.
Then Ioshua made him sharpe kniues and circumcised the sonnes of Israel in the hill of the foreskinnes.
4 Na hii ndo sababu ya Yoshua kuwatahiri; wanaume wote waliotoka Misri, pamoja na wanaume wa vita walikuwa wamekwisha kufa njiani katika nyikani, baada ya kukwea kutoka Misri.
And this is the cause why Ioshua circumcised all the people, euen the males that came out of Egypt, because all the men of warre were dead in the wildernesse by the way after they came out of Egypt.
5 Ingawa wanaume wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, bado hapakuwa na kijana yeyote aliyekuwa ametahiriwa kati ya vijana wote waliozaliwa nyikani katika njia ya kutoka Misri.
For all the people that came out were circumcised: but all the people that were borne in the wildernes by the way after they came out of Egypt, were not circumcised.
6 Kwasababu watu wa Israeli walitembea nyikani miaka arobaini, mpaka watu wa vita, yaani wanaume wote waliotoka Misri walikufa, kwasababu hawakuitii sauti ya Yahweh. Yahweh aliwaapia kwamba hawataruhusu kuiona nchi ambayo aliwaapia mababa zao kwamba angetupatia sisi, nchi inayotiririka maziwa na asali.
For the children of Israel walked fourtie yeres in the wildernes, till all the people of the men of warre that came out of Egypt were consumed, because they obeyed not the voyce of the Lord: vnto whome the Lord sware, that he would not shewe them the lande, which the Lord had sworne vnto their fathers, that he would giue vs, euen a land that floweth with milke and hony.
7 Na badala yao, Yahweh aliwainua watoto wao kuchukua nafasi zao ambao Yoshua aliwatahiri, kwasababu walikuwa bado hajatahiriwa njiani.
So their sonnes whome he raysed vp in their steade, Ioshua circumcised: for they were vncircumcised, because they circumcised them not by the way.
8 Walipokwisha kutahiriwa wote, walibaki mahali walipokuwa katika kambi mpaka walipopona.
And when they had made an ende of circumcising al the people, they abode in the places in the campe till they were whole.
9 Na Yahweh akasema na Yoshua, “Siku hii nimeiondoa kwenu aibu ya Misri.” Hivyo, mahali pale paliitwa Gilgali hadi leo.
After, the Lord said vnto Ioshua, This day I haue taken away the shame of Egypt from you: wherefore he called the name of that place Gilgal, vnto this day.
10 Watu wa Israeli walipiga kambi hapo Gilgali. Waliitunza Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, katika uwanda wa Yeriko.
So the children of Israel abode in Gilgal, and kept ye feast of the Passeouer the fourteenth day of the moneth at euen in ye plaine of Iericho.
11 Na siku iliyofuata baada ya Pasaka, walikula sehemu ya mazao ya nchi, mikate isiyotiwa chachu na nafaka iliyokaangwa katika siku hiyo iyo.
And they did eat of the corne of the land, on the morow after the Passeouer, vnleauened breade, and parched corne in the same day.
12 Mana zilikoma siku ile walipokula mazao ya nchi. Hapakuwa tena na mana kwa watu wa Israeli, bali walikula mazao ya nchi ya Kanaani mwaka huo.
And the MAN ceased on the morowe after they had eaten of the corne of the land, neither had the children of Israel MAN any more, but did eate of the fruite of the land of Canaan that yeere.
13 Wakati Yoshua alipokaribia Yeriko, aliinua macho na kuangalia, na tazama, mtu alikuwa amesimama mbele yake, alikuwa amechomoa upanga wake na ulikuwa mkononi mwake. Yoshua alimwendea na kumwambia, “Je uko kwa ajili yetu au kwa ajli ya maadui zetu?”
And when Ioshua was by Iericho, he lift vp his eyes and looked: and behold, there stood a man against him, hauing a sword drawen in his hand: and Ioshua went vnto him, and said vnto him, Art thou on our side, or on our aduersaries?
14 Akajibu, la hasha. Maana mimi ni amiri wa jeshi la Yahweh. Sasa nimekuja. Kisha Yoshua akainamisha uso wake juu ya nchi akaabudu na akamwambia, “Bwana wangu anasema nini kwa mtumwa wake?”
And he said, Nay, but as a captaine of the host of the Lord am I nowe come: then Ioshua fel on his face to the earth, and did worship, and saide vnto him, What sayth my Lord vnto his seruant?
15 Amiri wa jeshi la Yahweh akamwambia Musa, “Vua viatu vyako miguuni mwako, kwasababu sehemu uliyosimama ni takatifu.” Na Yoshua akafanya hivyo.
And the captaine of ye Lords host said vnto Ioshua, Loose thy shoe of thy foote: for ye place wheron thou standest, is holy: and Ioshua did so.

< Yoshua 5 >