< Yoshua 4 >

1 Watu wote walipokwisha kuvuka Yordani, Yahweh akamwambia Yoshua,
And when they had crossed over, the Lord said to Joshua:
2 “Chagueni wenyewe watu waume kumi na wawili, mmoja katika kila kabila.
“Choose twelve men, one from each tribe,
3 Wape agizo hilo: 'Chukueni mawe kumi na mbili kutoka katikati ya Yordani mahali wanaposimama makuhani katika nchi kavu, na wayalete na kuyaweka chini katika sehemu ambapo mtalala usiku wa leo.
and instruct them so that they may take from the midst of the channel of the Jordan, where the feet of the priests stood still, twelve very hard stones, which you shall station in the place of the camp, where you will pitch your tents this night.”
4 Kisha Yoshua akawaita wanaume kumi na wawili ambao aliwachagua kutoka katika makabila ya Israeli, mmoja kutoka kila kabila.
And Joshua called twelve men, whom he had chosen from the sons of Israel, one from each tribe,
5 Yoshua akawaambia, “Nendeni mbele za sanduku la Yahweh Mungu wenu katikati ya Yordani. Kila mmoja wenu achukue jiwe moja mabegani mwake, kulingana na hesabu ya makabila ya watu wa Israeli.
and he said to them: “Go before the ark of the Lord your God into the middle of the Jordan, and let each one carry from there one stone on your shoulders, according to the number of the sons of Israel,
6 Hii itakuwa ni ishara miongoni mwenu kwa ajili yenu wakati watoto wenu watakapowauliza katika siku zijazo, 'Nini maana ya mawe haya kwenu?'
so that it may be a sign among you. And when your sons will ask you, tomorrow, saying, ‘What do these stones mean to you?’
7 Ndipo mtakapowaambia, 'Maji ya Yordani yalitengwa mbele ya sanduku la Yahweh. Lililpopitishwa katika Yordani, maji ya Yordani yalisimamishwa. Hivyo, mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.'”
you shall respond to them: ‘The waters of the Jordan failed before the ark of the covenant of the Lord, when the ark crossed over it. For this reason, these stones were placed as a monument for the sons of Israel, even forever.’”
8 Watu waisraeli walifanya kama Yoshua alivyowaagiza, na walichukua mawe kumi na mbili kutoka katikati ya Yordani, kama Yahweh alivyomwambia Yoshua, walipangwa sawa sawa na hesabu ya makabila ya watu wa Israeli. Waliyachukua mawe mpaka mahali walipolala na wakayaweka chini huko.
Therefore, the sons of Israel did as Joshua instructed them, carrying twelve stones from the midst of the channel of the Jordan, just as the Lord had ordered him, according to the number of the sons of Israel, as far as the place where they made camp, and there they stationed them.
9 Kisha Yoshua akayapanga mawe kumi na mbili katikati ya Yordani, katika sehemu ambapo ilisimama miguu ya makuhani waliolichukua sanduku la agano. Na kumbukumbu hiyo ipo hadi leo.
Similarly, Joshua positioned another twelve stones in the middle of the channel of the Jordan, where the priests stood who were carrying the ark of the covenant; and they are there, even to the present day.
10 Makuhani waliolichukua sanduku walisimama katikati ya Yordani mpaka pale kila kitu ambacho Yahweh alimwamuru Yoshua kuwaambia watu kilipokamilika, sawa sawa na yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua. Watu walifanya haraka na wakavuka.
Now the priests who were carrying the ark stood in the midst of the Jordan, until everything was accomplished which the Lord had instructed Joshua to speak to the people and which Moses had said to him. And the people hurried, and they passed over.
11 Wakati watu wote walipokwisha kuvuka, sanduku la Yahweh pamoja na makuhani walivuka mbele za watu.
And when they had all crossed, the ark of the Lord also crossed, and the priests advanced before the people.
12 Kabila la Rubeni, kabila la Gadi, na nusu ya kabila la Manase walipita kama jeshi mbele ya watu wa Israeli, kama ambavyo Musa alivyowaambia.
Likewise, the sons of Reuben, and of Gad, and of the one half tribe of Manasseh advanced with weapons before the sons of Israel, just as Moses had instructed them.
13 Yapata watu watu elfu arobaini walioandaliwa kwa vita walipita mbele za Yahweh, kwa ajili ya vita katika uwanda wa Yeriko.
And forty thousand fighters, by companies and divisions, advanced through the plains and fields of the city of Jericho.
14 Katika siku hiyo Yahweh alimfanya Yoshua kuwa mkuu katika macho ya watu wote wa Israeli. Walimheshimu - kama walivyomheshimu Musa - siku zake zote.
In that day, the Lord magnified Joshua in the sight of all Israel, so that they would fear him, just as they had feared Moses while he lived.
15 Kisha Yahweh akamwambia Yoshua,
And he said to him,
16 “Waamuru makuhani wanaolibeba sanduku la ushuhuda watoke katika Yordani.”
“Command the priests who are carrying the ark of the covenant to ascend from the Jordan.”
17 Hivyo Yoshua akawaamuru makuhani, '' pandeni mtoke Yordani.”
And he commanded them, saying, “Ascend from the Jordan.”
18 Wakati makuhani wenye kulibeba sanduku la agano la Yahweh walitoka katikati ya Yordani, na nyayo za miguu yao ilikuwa imeinuliwa katika nchi kavu, kisha maji ya Yordani yalirudi katika sehemu zake na kujaa hadi katika kingo zake kama ilivyokuwa siku nne zilizopita.
And when those who were carrying the ark of the covenant of the Lord had ascended, and they began to step on dry soil, the waters returned to their channel, and they flowed as they usually did before.
19 Katika siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, watu walikwea kutoka Yordani. Wakakaa huko Gilgali, mashariki mwa Yeriko.
Now the people ascended from the Jordan on the tenth day of the first month, and they encamped at Gilgal, opposite the eastern portion of the city of Jericho.
20 Mawe kumi na mawili ambayo yalichukuliwa katika Yordani, Yoshuua aliyasimamisha hapo Gilgali.
Likewise, the twelve stones that they had taken up from the channel of the Jordan, Joshua stationed at Gilgal.
21 Aliwaambia watu wa Israeli, “wakati watoto wenu watakapowauliza baba zao katika wakai ujao, 'Mawe haya ni ya nini?'
And he said to the sons of Israel: “When your sons will question their fathers, tomorrow, and they will say to them, ‘What do these stones mean to you?’
22 Waambieni watoto wenu, 'Hapa ndipo Waisraeli walivuka Yordani katika nchi kavu.
you shall teach them, and you shall say: ‘Israel passed over this Jordan, through the dry channel.’
23 Yahweh Mungu wenu aliyakausha maji ya Yordani, mpaka hapo Yahweh Mungu wako aliyoyafanya katika bahari ya mianzi, ambayo aliikausha kwa ajili yetu ili tupite juu yakes,
For the Lord your God dried up its waters in your sight, until you crossed over, just as he had done before, at the Red Sea, which he dried up until we crossed over.
24 ili kwamba watu wote wa nchi wajue kwamba mkono wa Yahweh ni nguvu, na kwamba mtamweshimu Yahweh Mungu wenu milele.''
So may all the peoples of the earth learn of the very powerful hand of the Lord. So may you also fear the Lord your God for all time.”

< Yoshua 4 >