< Yoshua 24 >

1 Kisha Yoshua aliyakusanya pamoja makabila yote ya Israeli huko Shekemu na aliwaita wazee wa Israeli, viongozi, waamuzi na maafisa wao, nao wakajihudhurisha mbele za Mungu.
Josué réunit toutes les tribus d’Israël à Sichem; puis il appela les anciens d’Israël, ses chefs, ses juges et ses préposés, qui se placèrent en présence de Dieu.
2 Yoshua akawaambia watu wote, “Hiki ndicho Yahweh, Mungu wa Israeli anachokisema, 'Mababu zenu kwa miaka mingi iliyopita waliishi ng'ambo ya mto Frati - Tera, baba wa Ibrahimu na baba wa Nahori - nao waliabudu miungu mingine.
Et Josué dit à tout le peuple: "Ainsi a parlé l’Eternel, Dieu d’Israël: "Vos ancêtres habitaient jadis au-delà du Fleuve, jusqu’à Tharé, père d’Abraham et de Nahor, et ils servaient des dieux étrangers.
3 Lakini nilimchukua baba yenu kutoka ng'ambo ya Frati na nikamwongoza mpaka katika nchi ya Kanaani, na nilimpa watoto wengi kupitia kwa Isaka mwanaye.
Je pris votre père, Abraham, des bords du Fleuve, le fis voyager par tout le pays de Canaan, lui donnai une nombreuse postérité, et le rendis père d’Isaac.
4 Na Isaka nikampa Yakobo na Esau. Nilimpa Esau nchi ya milima ya Seiri ili aimiliki, lakini Yakobo na watoto wake walishuka kwenda Misri.
A Isaac je donnai Jacob et Esaü; j’attribuai à Esaü la montagne de Séïr pour sa possession, Jacob et ses enfants descendirent en Egypte.
5 Nilimtuma Musa na Haruni, na niliwapiga Wamisri kwa mapigo. Baada ya hapo, niliwatoa ninyi.
Je suscitai Moïse et Aaron, j’accablai l’Egypte par tout ce que je fis au milieu d’elle, après quoi je vous en fis sortir.
6 Niliwatoa baba zenu nje ya nchi ya Misri, nanyi mkafika hata katika bahari. Wamisri waliwafuata kwa magari na wapanda farasi hata katika bahari ya matete.
Quand j’eu fait sortir vos pères de l’Egypte et que vous fûtes parvenus jusqu’à la mer, les Egyptiens poursuivirent vos pères, avec chars et cavaliers, vers la mer des Joncs.
7 Na baba zenu walipomwita Yahweh, aliweka giza kati yenu na Wamisri. Aliileta bahari ije juu yao na kuwafunika. Mliona yale niliyoyakifanya huko Misri. Kisha mliishi jangwaani kwa muda mrefu.
Ceux-ci implorèrent l’Eternel, qui interposa un épais nuage entre vous et les Egyptiens, fit retomber sur eux la mer et les submergea vous avez vu de vos yeux ce que j’ai fait à l’Egypte puis vous demeurâtes de longs jours au désert.
8 Niliwaleta katika nchi wa Waamori, ambao waliishi katika upande mwingine mwa Yordani. Walipigana nanyi, nami niliwatia katika mkono wenu. Mliimiliki nchi yao, nami niliwaangamiza mbele yenu.
Je vous conduisis au pays des Amorréens, établis au bord du Jourdain, et qui vous combattirent; je les livrai en votre pouvoir, vous conquîtes leur pays, et je les exterminai devant vous.
9 Kisha Balaki mwana wa Zipori, mfalme wa Moabu, aliinuka na kuishambulia Israeli. Alimwita na kumtuma Baalamu mwana wa Beori, ili kuwalaani ninyi.
Puis se leva Balak, fis de Cippor, roi de Moab, qui entra en lutte avec Israël, et fit appeler Balaam, fils de Beor, pour vous maudire.
10 Lakini sikumsikiliza Balaamu. Kwa hakika, aliwabarikia ninyi. Basi, niliwaokoa na mkono wake.
Mais je ne voulus pas écouter Balaam, et il dut au contraire vous bénir, et je vous sauvai ainsi de sa main.
11 Mlivuka Yordani na mkafika Yeriko. Viongozi wa Yeriko waliinuka wapigane nanyi, pamoja na Waamori, Waperizi, Wakanaani, Wahiti, Wagirgashi, Wahivi na Wayebusi. Niliwapa ninyi ushindi dhidi yao na niliwaweka chini ya mamlaka yenu.
Puis vous traversâtes le Jourdain et arrivâtes devant Jéricho; et vous eûtes contre vous les possesseurs de Jéricho, les Amorréens, les Phérézéens, les Cananéens, les Héthéens, le Ghirgachéens, les Hévéens et les Jébuséens; mais je les livrai en votre pouvoir.
12 Nilituma manyingu mbele yenu, ambayo yaliwafukuzia mbali na wafalme wawili wa Waamori watoke mbele yenu. Haikutokea kwa sababu ya upanga wenu wala kwa upinde wenu.
Je vous ai aussi fait précéder par les frelons, qui ont chassé de devant vous les deux rois des Amorréens, ce que tu ne dois ni à ton épée ni à ton arc.
13 Niliwapeni ninyi nchi ambayo hamkuifanyia kazi na miji ambayo hamkuijenga, na sasa mnaishi ndani yake. Mnakula matunda ya mizabibu na na mashamba ya mizeituni ambayo hamkuyapanda'.
Je vous ai ainsi donné un pays qui ne vous a coûté aucune peine; des villes où vous vous êtes installés sans les avoir bâties, des vignes et des oliviers dont vous jouissez sans les avoir plantés."
14 Basi sasa mcheni Yahweh na kumwabudu yeye kwa uadilifu na uaminifu wote; jitengeni na miungu ambayo baba zenu waliiabudu ng'ambo ya Frati na katika Misri, na mkamwabudu Yahweh.
A votre tour, révérez et servez l’Eternel avec droiture, avec sincérité; repoussez les dieux que vos pères ont adorés au-delà du Fleuve et en Egypte, et n’adorez que l’Eternel.
15 Na kama inaonekana kuwa ni vibaya machoni penu kumwabudu Yahweh, chagueni ninyi katika siku hii ya leo ni nani mtakayemtumikia, kama ni miungu ambayo baba zenu waliiabudu ng'ambo ya Frati, au miungu ya Waamori, ambao ninyi mnakaa ndani ya nchi yao. Lakini kwangu mimi na nyumba yangu, tutumwabudu Yahweh.”
Que s’il vous déplaît de servir l’Eternel, choisissez dès à présent qui vous voulez servir, soit les dieux qu’adoraient vos pères au-delà du Fleuve, soit les dieux des Amorréens dont vous occupez le pays: pour moi et ma famille, c’est l’Eternel que nous servons!"
16 Watu walijibu na kusema, “Hatutaweza kumwacha Yahweh na kuitumikia miungu mingine,
Le peuple répondit: "Loin de nous la pensée de renoncer à l’Eternel pour servir des dieux étrangers!
17 kwa kuwa ni Yahweh Mungu wetu ambaye alitutoa sisi na baba zetu kutoka katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa, na ambaye alifanya hizo ishara kubwa mbele yetu, na ambaye alituhifadhi sisi katika njia zote ambazo sisi tuliziendea, na miongoni mwa mataifa yote ambayo tulipita kati kati yake,
C’Est l’Eternel qui est notre Dieu, c’est lui qui nous a fait monter nous et nos pères, du pays d’Egypte, cette maison d’esclaves; qui a fait à nos yeux tant de grands miracles, qui nous a protégés constamment dans notre voie, parmi tous les peuples au milieu desquels nous avons passé.
18 Na Yahweh aliwaondoa mbele yetu watu wote, na Waamori walioishi katika nchi hii. Hivyo, tutamwabudu Yahweh pia, kwa kuwa ni Mungu wetu”
C’Est l’Eternel qui a repoussé devant nous l’Amorréen et les autres peuples habitant la contrée: nous aussi nous entendons servir l’Eternel, car c’est lui notre Dieu."
19 Lakini Yoshua akawaambia watu, “Hamwezi kumtumikia Yahweh, kwa kuwa ni Mungu mtakatifu; ni Mungu mwenye wivu; hatawasamehe makosa na dhambi zenu.
Et Josué dit au peuple: "Vous ne pourrez pas aisément servir l’Eternel; car c’est un Dieu saint, un Dieu jaloux, qui ne supporterait ni vos offenses ni vos péchés.
20 Kama mtamwacha Yahweh na kuabudu miungu ya kigeni, basi atageuka na kuwaharibu. Atawaangamizeni baada ya kuwa amewatendea mema.”
Si vous abandonnez l’Eternel pour servir les dieux de l’étranger, à son tour il vous maltraitera et consommera votre ruine, après avoir été votre bienfaiteur."
21 Lakini watu walimwambia Yoshua, “Hapana, tutamwabudu Yahweh.”
Et le peuple répondit à Josué: "Non, nous voulons servir l’Eternel."
22 Kisha Yoshua akawaambia watu, “Ninyi ni mashahidi dhidi yenu wenyewe kuwa mmemchagua Yahweh ninyi wenyewe, ili mmwabudu yeye.” Watu walijibu, “Sisi ni mashahidi.”
Alors Josué dit au peuple: "Vous êtes témoins contre vous-mêmes, que c’est pour le culte de l’Eternel que vous avez opté!" Ils répondirent: "Nous le sommes."
23 “Sasa wekeni mbali miungu ya kigeni iliyoko kwenu, na geuzeni moyo wenu umwelekee Yahweh, Mungu wa Israeli.”
"Eh bien! Répudiez donc les dieux de l’étranger qui sont au milieu de vous, et tournez uniquement vos coeurs vers l’Eternel, Dieu d’Israël."
24 Watu wakamwambia Yoshua, “Tutamwabudu Yahweh Mungu wetu. Tutaisikiliza sauti yake.
Et le peuple dit à Josué: "C’Est l’Eternel, notre Dieu, que nous servirons, c’est à sa voix que nous voulons obéir."
25 Yoshua alifanya agano na watu siku hiyo. Aliziweka maagizo na sheria huko Shekemu.
En ce jour même, Josué établit un pacte avec le peuple, et lui imposa une loi et des statuts à Sichem.
26 Yoshua aliyaandika maneno haya katika kitabu cha sheria za Mungu. Alichukua jiwe kubwa na kulisimamisha hapo chini ya mti wa mwaloni uliokuwa karibu na mahali pa takatifu pa Yahweh.
Puis Josué consigna ces choses dans le livre de la loi divine; il prit aussi une grande pierre qu’il dressa en ce lieu, sous le chêne qui était dans le lieu consacré à l’Eternel.
27 Yoshua akawaambia watu, “Tazama, jiwe hili litakuwa ushuhuda dhidi yenu. Limeyasikia maneno yote ambayo Yahweh alitwambia. Hivyo, litakuwa ni shahidi dhidi yenu, hamtakiwi kumkana Mungu wenu.”
Et Josué dit à tout le peuple: "Cette pierre nous servira de témoin, car elle a entendu toutes les paroles que l’Eternel nous a adressées; elle serait un témoin contre vous, si vous veniez à renier votre Dieu."
28 Basi Yoshua aliwaacha watu waende zao, kila mmoja alienda kwenye urithi wake.
Et Josué congédia le peuple, chacun rentrant dans son territoire.
29 Baada ya mambo haya, Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Yahweh, alikufa akiwa na miaka 110.
Après ces événements, Josué, fils de Noun, serviteur de l’Eternel, mourut âgé de cent dix ans.
30 Walimzika katika mpaka wa urithi wake mwenyewe huko Timnathi Sera, ambayo iko kwenye nchi ya milima ya Efraimu, upande wa Mlima Gaashi.
On l’ensevelit dans les limites de sa possession, à Timnath-Sérah, dans la montagne d’Ephraïm, au nord du mont Gaach.
31 Israeli ilimwabudu Yahweh siku zote za maisha ya Yoshua, na siku zote za wazee ambao walidumu pamoja na Yoshua, wale ambao waliona kila kitu ambacho Yahweh alikuwa ameifanyia Israeli.
Israël resta attaché au Seigneur tant que vécut Josué, et tout le temps que continuèrent à vivre, après lui, les vieillards témoins de tout ce que le Seigneur avait fait pour Israël.
32 Mifupa ya Yusufu ambayo watu wa Israeli waliileta kutoka Misri, waliizika huko shekemu, katika sehemu ya nchi ambayo Yakobo alikuwa ameinunua kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu. Aliinunua kwa vipande mia moja vya fedha, na ulikuwa urithi kwa wazawa wa Yusufu.
Quant aux ossements de Joseph, que les enfants d’Israël avaient emportés d’Egypte, on les inhuma à Sichem, dans la pièce de terre que Jacob avait acquise, pour cent kecita, des fils de Hamor, père de Sichem, et qui devint la propriété des enfants de Joseph.
33 Eliazeri mwana wa Haruni alikufa pia. Walimzika huko Gibea, katika mji wa ambao alikuwa amepewa Finehasi mwanaye, na ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu.
Eléazar, fils d’Aaron, étant mort, on l’ensevelit sur la colline de Phinéas, son fils, qu’on lui avait donnée dans la montagne d’Ephraïm.

< Yoshua 24 >