< Yoshua 23 >
1 Na baada ya siku nyingi, kipindi ambacho Yahweh alikuwa ameipa Israeli pumziko kutoka maadui zao waliowazunguka,
And it was from days many after that he had given rest Yahweh to Israel from all enemies their from round about and Joshua he was old he had come in days.
2 Joshua alikuwa mzee sana. Yoshua aliwaita Waisraeli wote, na wazee wao, na viongozi, na waamuzi, na kwa maafisa, na kisha akawaambia, “Mimi nimezeeka sana.
And he summoned Joshua all Israel elders its and leaders its and judges its and officials its and he said to them I I am old I have come in days.
3 Mmeshaona kila kitu ambacho Yahweh Mungu wenu ameshafanya kwa mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa kuwa ni Yahweh Mungu wenu ambaye amewapigania ninyi.
And you you have seen all that he has done Yahweh God your to all the nations these from before you for Yahweh God your he [is] the [one who] has been fighting for you.
4 Tazama! Nimeshawakabidhi kwenu mataifa yaliyosalia ili kuyateka kwa ajili ya kupata urithi ya makabila yenu, sambasamba na mataifa yote ambayo tayari nimeshayaangamiza, tangu Yordani hadi Bahari kuu katika upande wa magharibi.
See I have made fall to you the nations which remain these an inheritance for tribes your from the Jordan and all the nations which I have cut off and the sea great [the] setting of the sun.
5 Yahweh Mungu wenu atayaondoa. Atayafukuzia mbali kutoka kwenu. Ataiteka nchi yao, nanyi mtaimiliki nchi yao, kama vile Yahweh Mungu wenu alivyowaahidi ninyi.
And Yahweh God your he he will drive out them from before you and he will dispossess them from to before you and you will take possession of land their just as he spoke Yahweh God your to you.
6 Hivyo, iweni jasiri, ili kwamba mtunze na kuyafanya yale yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa, msikengeuke upande wa kulia wala upande wa kushoto,
And you will be strong very to take care and to do every [thing] written in [the] book of [the] law of Moses to not to turn aside from it right [hand] and left [hand].
7 basi msichanganyikane na mataifa haya ambayo yamesalia miongoni mwenu, wala msiyataje majina ya miungu yao, wala msiape kwayo, wala msiiabudu, wala msiipigie magoti.
To not to go among the nations these which remain these with you and [the] name of gods their not you must bring to remembrance and not you must cause to swear and not you must serve them and not you must bow down to them.
8 Badala yake, mnatakiwa kumshika sana Yahweh Mungu wenu kama vile mlivyofanya siku hii ya leo.
That except to Yahweh God your you will cling just as you have done until the day this.
9 Kwa kuwa Yahweh ameyafukuzia mbali mbele yenu mataifa makubwa yenye nguvu. Hakuna hata mmoja aliyeweza kusimama mbele yenu hata siku hii ya leo.
And he has dispossessed Yahweh from before you nations great and mighty and you not he has stood anyone in faces your until the day this.
10 Mtu yeyote mmoja wa kwenu atawafanya watu elfu wakimbie mbali, kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ndiye anayepigania ninyi, kama vile alivyowaahidi.
A man one of you he puts to flight a thousand for - Yahweh God your he [is] the [one who] fights for you just as he spoke to you.
11 Zingatieni kwa uangalifu ili mmpende Yahweh Mungu wenu.
And you will take heed exceedingly to selves your to love Yahweh God your.
12 Lakini kama mkiegeuka na kushikamana na watu walioalia wa mataifa haya waliobaki miongoni mwenu, au kuoana nao, au kama mkishirikiana pamoja nao, na wao pamoja nanyi,
That - except ever you will turn back and you will cling to [the] remainder of the nations these which remain these with you and you will intermarry with them and you will go among them and they among you.
13 jueni kwa hakika kwamba Yahweh Mungu wenu hatayafukuzia mbali mataifa haya yatoke kati yenu. Badala yake, watakuwa kitanzi na mtego kwenu, viboko migongoni mwenu na miiba machoni mwenu, mpaka pale mtakapoangamia katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
Certainly you will know that not he will increase Yahweh God your to dispossess the nations these from to before you and they will become for you a trap and a snare and a scourge in sides your and thorns in view your until perish you from on the land good this which he has given to you Yahweh God your.
14 Na sasa ninaenda katika njia ya dunia yote, na mnajua kwa moyo na roho zenu zote kwamba hakuna hata neno moja ambalo halijatimia kati ya mambo yote mazuri ambayo Yahweh Mungu wenu aliyaahidi juu yenu. Vitu hivi vyote vimetokea kwa ajili yenu. Hakuna hata moja lililoshindikana.
And here! I [am] about to go this day in [the] way of all the earth and you know with all heart your and with all being your that not it has fallen a word one of all - the words good which he spoke Yahweh God your on you everything they have come to you not it has fallen of it a word one.
15 Lakini kama kila neno ambalo Yahweh Mungu wenu alilowaahidi limekwisha kutimia, hivyo Yahweh atawaletea juu yenu mabaya yote mpaka pale atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
And it will be just as it has come on you every word good which he spoke Yahweh God your to you so he will bring Yahweh on you every word bad until has destroyed he you from on the land good this which he has given to you Yahweh God your.
16 Atafanya hivi kama mtalivunja agano la Yahweh Mungu wenu, ambalo aliwaagizeni kulitunza. Kama mtaenda na kuiabudu miungu mingine na kuiinamia, ndipo hasira ya Yahweh itawaka kinyume nanyi, na ninyi mtaangamia upesi katika nchi nzuri ambayo amekwisha kuwapeni ninyi.”
When transgress you [the] covenant of Yahweh God your which he commanded you and you will go and you will serve gods other and you will bow down to them and it will burn [the] anger of Yahweh on you and you will perish quickly from on the land good which he has given to you.