< Yoshua 23 >

1 Na baada ya siku nyingi, kipindi ambacho Yahweh alikuwa ameipa Israeli pumziko kutoka maadui zao waliowazunguka,
And it came to pass, after many days, when Yahweh had given rest unto Israel, from all their enemies round about, —and, Joshua, had become old, advanced in days,
2 Joshua alikuwa mzee sana. Yoshua aliwaita Waisraeli wote, na wazee wao, na viongozi, na waamuzi, na kwa maafisa, na kisha akawaambia, “Mimi nimezeeka sana.
that Joshua called for all Israel, for their elders, and for their heads, and for their judges, and for their officers, —and said unto them, I, am old, advanced in days;
3 Mmeshaona kila kitu ambacho Yahweh Mungu wenu ameshafanya kwa mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa kuwa ni Yahweh Mungu wenu ambaye amewapigania ninyi.
but, ye, have seen—all that Yahweh your God hath done unto all those nations, because of you, —for, Yahweh your God, is he that hath fought for you.
4 Tazama! Nimeshawakabidhi kwenu mataifa yaliyosalia ili kuyateka kwa ajili ya kupata urithi ya makabila yenu, sambasamba na mataifa yote ambayo tayari nimeshayaangamiza, tangu Yordani hadi Bahari kuu katika upande wa magharibi.
Behold, I have allotted to you these nations which remain, as an inheritance, for your tribes, —from the Jordan, and all the nations which I have cut off, even unto the great sea, at the going in of the sun.
5 Yahweh Mungu wenu atayaondoa. Atayafukuzia mbali kutoka kwenu. Ataiteka nchi yao, nanyi mtaimiliki nchi yao, kama vile Yahweh Mungu wenu alivyowaahidi ninyi.
But, Yahweh your God—he, will thrust them out from before you, and drive them away out of your sight, —so shall ye possess their land, as Yahweh your God spoke unto you.
6 Hivyo, iweni jasiri, ili kwamba mtunze na kuyafanya yale yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa, msikengeuke upande wa kulia wala upande wa kushoto,
Therefore must ye be very firm to observe and to do all that is written in the scroll of the law of Moses, —so as not to turn aside therefrom, to the right hand or to the left;
7 basi msichanganyikane na mataifa haya ambayo yamesalia miongoni mwenu, wala msiyataje majina ya miungu yao, wala msiape kwayo, wala msiiabudu, wala msiipigie magoti.
so as not to go in among these nations, these which remain with you, —and, with the name of their gods, shall ye neither make memorial nor put on oath, and neither serve them, —nor bow down to them.
8 Badala yake, mnatakiwa kumshika sana Yahweh Mungu wenu kama vile mlivyofanya siku hii ya leo.
But, unto Yahweh your God, must ye cleave, —as, ye have done until this day;
9 Kwa kuwa Yahweh ameyafukuzia mbali mbele yenu mataifa makubwa yenye nguvu. Hakuna hata mmoja aliyeweza kusimama mbele yenu hata siku hii ya leo.
therefore hath Yahweh dispossessed, from before you, nations great and strong, —but, as for you, not a man hath stood before you, until this day.
10 Mtu yeyote mmoja wa kwenu atawafanya watu elfu wakimbie mbali, kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ndiye anayepigania ninyi, kama vile alivyowaahidi.
One man of you, can chase a thousand, —for, Yahweh your God, is he that fighteth for you, as he spake to you.
11 Zingatieni kwa uangalifu ili mmpende Yahweh Mungu wenu.
Take diligent heed, therefore, unto your souls, —to love Yahweh your God.
12 Lakini kama mkiegeuka na kushikamana na watu walioalia wa mataifa haya waliobaki miongoni mwenu, au kuoana nao, au kama mkishirikiana pamoja nao, na wao pamoja nanyi,
But, if ye, do in any wise turn back, and cleave unto the remnant of these nations, these which remain with you, —and intermarry with them, and go in with them, and, they, with you;
13 jueni kwa hakika kwamba Yahweh Mungu wenu hatayafukuzia mbali mataifa haya yatoke kati yenu. Badala yake, watakuwa kitanzi na mtego kwenu, viboko migongoni mwenu na miiba machoni mwenu, mpaka pale mtakapoangamia katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
know, that Yahweh your God will no further drive out these nations from before you, —but they will become unto you a snare and a hook, and a goad in your sides, and thorns in your eyes, until ye have perished from off this goodly soil, which Yahweh your God hath given unto you.
14 Na sasa ninaenda katika njia ya dunia yote, na mnajua kwa moyo na roho zenu zote kwamba hakuna hata neno moja ambalo halijatimia kati ya mambo yote mazuri ambayo Yahweh Mungu wenu aliyaahidi juu yenu. Vitu hivi vyote vimetokea kwa ajili yenu. Hakuna hata moja lililoshindikana.
But lo! I am going to-day, in the way of all the earth, —ye must acknowledge, therefore, with all your heart and with all your soul, that there hath not failed a single thing, out of all the good things which Yahweh your God spake concerning you, the whole, hath come to pass to you, there hath not failed thereof, a single thing.
15 Lakini kama kila neno ambalo Yahweh Mungu wenu alilowaahidi limekwisha kutimia, hivyo Yahweh atawaletea juu yenu mabaya yote mpaka pale atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
But it shall be that, as all the good things have come unto you, which Yahweh your God spake unto you, so, will Yahweh bring upon you all the evil things, until he hath destroyed you from off this goodly soil, which Yahweh your God hath given unto you.
16 Atafanya hivi kama mtalivunja agano la Yahweh Mungu wenu, ambalo aliwaagizeni kulitunza. Kama mtaenda na kuiabudu miungu mingine na kuiinamia, ndipo hasira ya Yahweh itawaka kinyume nanyi, na ninyi mtaangamia upesi katika nchi nzuri ambayo amekwisha kuwapeni ninyi.”
When ye transgress the covenant of Yahweh your God which he hath commanded you, and go and serve other gods, and bow yourselves down unto them, then will the anger of Yahweh kindle upon you, and ye will perish quickly, from off the good land which he hath given unto you.

< Yoshua 23 >