< Yoshua 23 >
1 Na baada ya siku nyingi, kipindi ambacho Yahweh alikuwa ameipa Israeli pumziko kutoka maadui zao waliowazunguka,
A long time later, after the Lord had given peace to the Israelites from conflict with their enemies around them, Joshua, by now really old,
2 Joshua alikuwa mzee sana. Yoshua aliwaita Waisraeli wote, na wazee wao, na viongozi, na waamuzi, na kwa maafisa, na kisha akawaambia, “Mimi nimezeeka sana.
summoned all the Israelites—the elders, leaders, judges, and officials—and told them, “I'm old, getting on in years.
3 Mmeshaona kila kitu ambacho Yahweh Mungu wenu ameshafanya kwa mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa kuwa ni Yahweh Mungu wenu ambaye amewapigania ninyi.
You've seen everything the Lord your God has done to all the nations on your behalf—the Lord your God has been fighting for you.
4 Tazama! Nimeshawakabidhi kwenu mataifa yaliyosalia ili kuyateka kwa ajili ya kupata urithi ya makabila yenu, sambasamba na mataifa yote ambayo tayari nimeshayaangamiza, tangu Yordani hadi Bahari kuu katika upande wa magharibi.
I have allotted the land of the remaining nations for you to own, as well as the nations already conquered, from the Jordan to the Mediterranean Sea.
5 Yahweh Mungu wenu atayaondoa. Atayafukuzia mbali kutoka kwenu. Ataiteka nchi yao, nanyi mtaimiliki nchi yao, kama vile Yahweh Mungu wenu alivyowaahidi ninyi.
The Lord your God will make them retreat from you. He will drive them out before you and you will take possession of their land, as the Lord your God promised you.
6 Hivyo, iweni jasiri, ili kwamba mtunze na kuyafanya yale yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa, msikengeuke upande wa kulia wala upande wa kushoto,
Be sure to observe everything that is written in the book of the Law of Moses. Don't stray from it, either to the left or to the right.
7 basi msichanganyikane na mataifa haya ambayo yamesalia miongoni mwenu, wala msiyataje majina ya miungu yao, wala msiape kwayo, wala msiiabudu, wala msiipigie magoti.
Don't associate with the nations that are left. Don't mention the names of their gods, and don't swear by them, worship them, or bow down to them.
8 Badala yake, mnatakiwa kumshika sana Yahweh Mungu wenu kama vile mlivyofanya siku hii ya leo.
Stay close to the Lord your God, as you have done up to now.
9 Kwa kuwa Yahweh ameyafukuzia mbali mbele yenu mataifa makubwa yenye nguvu. Hakuna hata mmoja aliyeweza kusimama mbele yenu hata siku hii ya leo.
The Lord has driven out strong, powerful nations before you. No one has been able to stand up to you to this day.
10 Mtu yeyote mmoja wa kwenu atawafanya watu elfu wakimbie mbali, kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ndiye anayepigania ninyi, kama vile alivyowaahidi.
Just one of you can chase away a thousand enemies, for the Lord your God is fighting for you, as he promised you.
11 Zingatieni kwa uangalifu ili mmpende Yahweh Mungu wenu.
Take great care to love the Lord your God.
12 Lakini kama mkiegeuka na kushikamana na watu walioalia wa mataifa haya waliobaki miongoni mwenu, au kuoana nao, au kama mkishirikiana pamoja nao, na wao pamoja nanyi,
For if you do turn from him, and adopt the ways of the nations that are left, if you intermarry with them, associating with one other,
13 jueni kwa hakika kwamba Yahweh Mungu wenu hatayafukuzia mbali mataifa haya yatoke kati yenu. Badala yake, watakuwa kitanzi na mtego kwenu, viboko migongoni mwenu na miiba machoni mwenu, mpaka pale mtakapoangamia katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
you can be absolutely sure that the Lord your God will definitely not drive out these nations before you. On the contrary, they will be a trap and a snare to you, a whip on you back and thorns in your eyes until you die out completely from this good land the Lord your God has given you.
14 Na sasa ninaenda katika njia ya dunia yote, na mnajua kwa moyo na roho zenu zote kwamba hakuna hata neno moja ambalo halijatimia kati ya mambo yote mazuri ambayo Yahweh Mungu wenu aliyaahidi juu yenu. Vitu hivi vyote vimetokea kwa ajili yenu. Hakuna hata moja lililoshindikana.
Now I am about to die, the fate of every living thing on the earth. Deep down you know that not a single one of the Lord's good promises has failed. Everything has come true. Not one has failed.
15 Lakini kama kila neno ambalo Yahweh Mungu wenu alilowaahidi limekwisha kutimia, hivyo Yahweh atawaletea juu yenu mabaya yote mpaka pale atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
But in the same way that you received all the good things that the Lord you God promised, the Lord will bring on you all the bad things he has threatened until you're completely wiped out from this good land the Lord your God has given you.
16 Atafanya hivi kama mtalivunja agano la Yahweh Mungu wenu, ambalo aliwaagizeni kulitunza. Kama mtaenda na kuiabudu miungu mingine na kuiinamia, ndipo hasira ya Yahweh itawaka kinyume nanyi, na ninyi mtaangamia upesi katika nchi nzuri ambayo amekwisha kuwapeni ninyi.”
If you break the agreement the Lord your God made with you, and you go and worship other gods, bowing down before them, then the Lord will become angry with you, and you will be quickly wiped out from the good land he has given you.”