< Yoshua 22 >
1 Kwa wakati huo, Yoshua aliwaita Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase.
Då kallade Josua till sig de Rubeniter och Gaditer, och den halfva slägtena Manasse.
2 Aliwaambia, “Mmefanya kila kitu ambacho Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi. Mmeitii sauti yangu katika yote niliyowaagiza.
Och sade till dem: I hafven hållit allt det Mose Herrans tjenare eder budit hafver, och lydt mine röst i allt det jag hafver budit eder.
3 Bado hamjawaacha ndugu zenu hawa kwa siku zote hizi, mpaka siku hii ya leo. Na mmetimiza wajibu unaotakiwa na amri za Yahweh Mungu wenu.
I hafven icke öfvergifvit edra bröder nu i en lång tid, allt intill denna dag; och hafven blifvit vid Herrans edars Guds bud.
4 Sasa Yahweh Mungu wenu amewapa pumziko ndugu zenu, kama alivyowaahidi. Hivyo basi, rudini na mwende katika hema zenu katika nchi mnayoimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapeni katika upande mwingine wa Yordani.
Efter nu Herren edar Gud hafver låtit edra bröder komma till ro, såsom han dem sagt hade; så vänder nu om igen, och drager till edra hyddor i edars arfs land, som Mose Herrans tjenare eder gifvit hafver på hinsidon Jordan;
5 Lakini zingatieni kuzishika amri na sheria ambazo Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi, kumpenda Yahweh Mungu wenu, kutembea katika njia zake, kuzitunza amri zake, na kuambatana naye na kumwabudu yeye kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.
Allenast tager der vara uppå granneliga, att I gören efter de bud och lag, som Mose Herrans tjenare eder budit hafver; att I älsken Herran edar Gud, och vandren uppå alla hans vägar, och hållen hans bud, och hållen eder intill honom, och tjenen honom af allo hjerta, och af allo själ.
6 Basi Yoshua akawabariki na kisha akawaacha waende zao, nao wakarudi katika hema zao.
Så välsignade Josua dem, och lät gå dem; och de gingo till deras hyddor.
7 Na kwa nusu ya kabila la Manase, Musa alikuwa amewapa urithi katika Bashani, lakini kwa nusu ya kabila hilo, Yoshua aliwapa urithi karibu na ndugu zao katika nchi magharibi mwa Yordani. Yoshua aliwaaga waende katika hema zao; aliwabarikia,
Den halfva slägtene Manasse hade Mose gifvit i Basan; den andra hälftene gaf Josua ibland deras bröder på desso sidone Jordan, vestantill. Och då han lät dem gå till deras hyddor, och hade välsignat dem,
8 na kisha akawaambia, “Rudini katika hema zenu mkiwa na pesa nyingi, na mkiwa na mifugo mingi, pamoja na na fedha, na dhahabu, na shaba na chuma, na nguo nyingi. Gawaneni na ndugu zenu nyara mlizochukua kutoka kwa maadui zenu.
Sade han till dem: I kommen hem igen med stora ägodelar till edra hyddor, med ganska mycken boskap, silfver, guld, koppar, jern och kläder; så skifter nu edra fiendars rof med edra bröder.
9 Hivyo, wazawa wa Rubeni, wazawa wa Gadi na nusu ya kabila la Manase walirudi nyumbani, waliwaacha watu wa Isaeli hapo Shilo, ambayo imo ndani ya nchi ya Kanaani. Waliondoka wakaenda katika mkoa wa Gileadi, katika nchi yao, ambayo wao wenyewe waliimiliki, katika utiifu wa amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.
Och så vände de Rubeniter och Gaditer, och den halfva slägten Manasse, om igen, och gingo ifrån Israels barn af Silo, som i Canaans land ligger, att de skulle draga in i Gileads land till deras arfs land, det de till arfs fått hade af Herrans befallning genom Mose.
10 Nao walipofika hapo Yordani iliyo katika nchi ya Kanaani, Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase walijenga madhabahu karibu na Yordani, madhabahu kubwa na iliyotokeza na mashuhuri.
Och då de kommo till de högar vid Jordan, som i Canaans land ligga, byggde de samme Rubeniter, Gaditer, och halfva Manasse slägt, der vid Jordan ett stort skönt altare.
11 Watu wa Israeli walisikia habari hizo na wakaseam, “Tazama! Watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wamejenga madhabahu mbele ya nchi ya Kanaani, huko Gelilothi, katika mkoa karibu na Yordani, katika upande ambao ni miliki ya watu wa Israeli.”
Då Israels barn hörde sägas: Si, Rubens barn, Gads barn, och den halfva slägten Manasse hafva byggt ett altare emot Canaans land, vid Jordans högar, på desso sidone vid Israels barn;
12 Wakati watu wa Israeli waliposikia hivyo, kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika kwa pamoja huko Shilo ili wapande kupigana vita nao.
Församlade de sig hela menigheten i Silo, att de skulle draga upp till dem, och strida med dem;
13 Kisha watu wa Israeli walituma wajumbe kwa Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi. Walimtuma pia Finehasi mwana wa Eliezari, kuhani,
Och sände till dem in uti Gileads land, Pinehas, Eleazars Prestens son;
14 na viongozi kumi pamoja naye, mmoja kutoka katika familia za mababa wa Israeli, na kila mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa ukoo miongoni mwa watu wa Israeli.
Och med honom tio öfversta Förstar ibland deras fäders hus, af hvarjo Israels slägt en.
15 Walienda kwa watu wa Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakawaambia:
Och när de kommo till dem i landet Gilead, talade de med dem, och sade:
16 “Kusanyiko lote la Yahweh linasema kuwa, ' Ni jambo gani hili lisilo la uaminifu ambalo mmelitenda kinyume na Mungu wa Israeli, kwa kugeuka badala ya kumfuata Yahweh siku hii na kujijengea wenyewe madhabahu katika uasi kinyume na Yahweh katika siku hii?
Så låter hela Herrans menighet säga eder: Hvi synden I så emot Israels Gud; och vänden eder i dag ifrå Herranom, dermed att I byggen eder ett altare, och fallen ifrå Herranom?
17 Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha? Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo. Kwa ajili ya dhambi ile lilikuja pigo kwa kusanyiko lote la Yahweh.
Är oss icke nog med Peors missgerning, af hvilko vi ännu på denna dag icke renade äre; och en plåga kom i Herrans menighet?
18 Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh? Kama mtaasi kinyume na Yahweh leo, kesho atakuwa na hasira na kusanyiko lote la Israeli.
Och I vänden eder i dag bort ifrå Herranom, och ären i dag affällige vordne ifrå Herranom; på det han i dag eller morgon skall vredgas öfver hela Israels menighet.
19 Na kama nchi ambayo mnaimiliki imetiwa unajisi, basi mwaweza kuvuka katika nchi ambayo Sanduku la Yahweh lasimama na mjichukulie kwa ajili yenu umiliki miongoni mwetu. Hamtakiwi kuasi kinyume na Yahweh tu, wala kuasi kinyume chetu kwa kujenga madhabahu kwa ajili yenu wenyewe badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wa wetu.
Tycker eder, att edart arfs land är orent, så kommer hitöfver i det land, som Herren hafver, der Herrans tabernakel är, och tager arf ibland oss; och träder icke ifrå Herranom, och ifrån oss, att I byggen eder ett altare, förutan Herrans vårs Guds altare.
20 Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli? Mtu yule hakuangamia peke yake kwa uovu wake.
Förbröt icke Achan, Serahs son, sig på det spillgifna; och vreden kom öfver hela Israels menighet, och han umgalt icke sina synd allena?
21 Kisha makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakawajibu wazee wa koo za Israeli:
Då svarade Rubens barn, och Gads barn, och den halfva slägten Manasse, och sade till de höfvitsmän och Förstar af Israel:
22 “Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yeye anajua, na Israeli naijue yenyewe! Kama ilikuwa ni katika uasi au katika kuvunja imani kinyume na Yahweh, msituache hai katika siku hii ya leo
Herren den starke Gud, Herren den starke Gud vet det, och Israel desslikes; är detta afträdning eller synd emot Herran, så hjelpe han oss intet i dag.
23 kwa ajili ya kujenga madhabahu ili tugeuka na kuacha kumfuata Yahweh. Kama tumejenga madhabahu hii ili kutoa juu yake sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, au sadaka ya amani, basi Yahweh na atuadhibu.
Och om vi altaret fördenskull byggt hafve, att vi vilje vända oss ifrå Herranom, offra deruppå bränneoffer och spisoffer, eller göra der tackoffer uppå, så hämnes det Herren;
24 La hasha, tulifanya hivyo kwa sababu ya hofu kwamba katika siku zijazo watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu, ' Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?
Och om vi icke det mycket heldre för denna sakens skull gjorde, och sade: I dag eller morgon måtte edor barn säga till vår barn: Hvad hafven I göra med Herranom Israels Gud?
25 Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi. Ninyi watu wa Rubeni na watu wa Gadi, hamna kitu chochote naYahweh.' Na kwa hali hiyo, watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.
Herren hafver satt Jordan till ett landamäre emellan oss och eder; I Rubens och Gads barn, I hafven ingen del med Herranom; och så måtte edor barn komma vår barn ifrå Herrans fruktan.
26 Basi tukasema, 'Hebu na tujenge sasa madhabahu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa wala si kwa sadaka yoyote ile,
Derföre sade vi: Låt oss bygga ett altare, icke till något offer eller bränneoffer;
27 ila iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi, na kati ya kizazi chetu baada yetu, kwamba tutafanya ibada ya Yahweh mbele yake, pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa na dhabihu zetu na sadaka zetu za amani, ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, “Hamna sehemu katika Yahweh.”'
Utan på det att det må vara ett vittnesbörd emellan oss och eder, och våra efterkommande, att vi måge tjena Herranom för honom med vårt bränneoffer, tackoffer och annor offer; och edor barn icke behöfva i dag eller morgon säga till vår barn: I hafven ingen del med Herranom.
28 Hivyo tukasema, 'kama hili litasemwa kwa kwetu au kwa watoto wetu katika siku zijazo, tutasema, “Tazama! Huu ni mfano wa madhabahu ya Yahweh, ambayo mababu zetu waliifanya, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala si kwa dhabihu, bali kwa ajili ya ushahidi kati yetu ninyi.”
När de nu vordo sägande till oss, eller våra efterkommande i dag eller morgon, så kunna de säga: Ser liknelsen till Herrans altare, hvilket våre fäder gjort hafva; icke till offer eller bränneoffer, utan till ett vittnesbörd emellan oss och eder.
29 Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh, na kuacha kumfuata yeye kwa kujenga madhabahu kwa ajili sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka ya nafaka, au kwa dhabihu, badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wetu ambayo iko mbele ya hema la kukutania.'”
Bort det ifrån oss, att vi skulle träda ifrå Herranom, så att vi i dag skulle vända oss ifrå Herranom, och bygga ett altare till bränneoffer, och till spisoffer, och annor offer, förutan Herrans vårs Guds altare, som står för hans tabernakel.
30 Finehasi kuhani na viongozi wa watu, ambao ni wakuu wa koo za Waisraeli ambao walikuwa pamoja naye, waliposikia maneno amabayo watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, kwamba yalikuwa ni mazuri machoni pao.
Då nu Pinehas Presten, och de öfverste för menighetene, Israels Förstar, som med honom voro, detta hörde, täcktes dem väl Rubens barnas, Gads, och den halfva Manasse slägts ord.
31 Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani aliwaambia watu wa Rubeni, Gadi na Manase, “Leo tumejua kwambaYahweh yuko miongoni mwetu, kwa kuwa hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye. Sasa, mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.”
Och Pinehas, Prestens Eleazars son, sade till Rubens, Gads, och Manasse barn: I dag förstå vi, att Herren är med oss, att I icke hafven syndat emot Herran med denna gerning; nu hafven I frälst Israels barn utu Herrans hand.
32 Kisha Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani, na viongozi walirudi kutoka kwa Warubeni na Wagadi, kutoka katika nchi ya Gileadi, na kurudi katika nchi ya Kanaani, kwa watu wa Israeli, na waliwaletea taarifa.
Så drog Pinehas, Prestens Eleazars son, och de öfverste, utu Gileads land, ifrå Rubens och Gads barn, åter in uti Canaans land, till Israels barn, och sade dem det igen.
33 Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu wa Israeli. Watu wa Israeli walimbarikia Mungu na hawakuendelea kusema tena juu ya kuinua vita dhidi ya Warubeni na Wagadi, ili kuiharibu nchi ambayo walikuwa wanaishi.
Då behagade det Israels barnom väl, och lofvade Israels barnas Gud; och sade intet mer, att de ville draga upp emot dem till slags, till att förderfva landet, som Rubens och Gads barn uti bodde.
34 Warubeni na Wagadi waliita ile madhabahu “Ushahidi,” kwa kuwa walisema, “Ni ushahidi miongoni mwetu kuwa Yahweh ni Mungu.”
Och Rubens och Gads barn kallade det altaret, att det skall vara ett vittne emellan oss, och att Herren är Gud.