< Yoshua 22 >

1 Kwa wakati huo, Yoshua aliwaita Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase.
Alors Josué manda les Rubénites, les Gadites et la demi-Tribu de Manassé,
2 Aliwaambia, “Mmefanya kila kitu ambacho Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi. Mmeitii sauti yangu katika yote niliyowaagiza.
et il leur dit: Vous avez observé tout ce que vous a prescrit Moïse, serviteur de l'Éternel, et obéi à ma voix dans tout ce que je vous ai commandé.
3 Bado hamjawaacha ndugu zenu hawa kwa siku zote hizi, mpaka siku hii ya leo. Na mmetimiza wajibu unaotakiwa na amri za Yahweh Mungu wenu.
Vous n'avez point abandonné vos frères pendant ce long temps jusqu'aujourd'hui, et vous avez observé ce qu'il fallait observer, le commandement de l'Éternel, votre Dieu.
4 Sasa Yahweh Mungu wenu amewapa pumziko ndugu zenu, kama alivyowaahidi. Hivyo basi, rudini na mwende katika hema zenu katika nchi mnayoimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapeni katika upande mwingine wa Yordani.
Et maintenant l'Éternel, votre Dieu, a accordé le repos à vos frères, comme Il le leur avait promis; retournez donc et gagnez vos tentes, le pays qui est votre propriété, que vous a concédé Moïse, serviteur de l'Éternel, au delà du Jourdain.
5 Lakini zingatieni kuzishika amri na sheria ambazo Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi, kumpenda Yahweh Mungu wenu, kutembea katika njia zake, kuzitunza amri zake, na kuambatana naye na kumwabudu yeye kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.
Seulement soyez très vigilants à mettre en pratique le commandement et la Loi que vous a prescrite Moïse, serviteur de l'Éternel, pour aimer l'Éternel, votre Dieu, et pour marcher dans toutes ses voies et garder ses commandements et vous attacher à Lui et Le servir de tout votre cœur et de toute votre âme.
6 Basi Yoshua akawabariki na kisha akawaacha waende zao, nao wakarudi katika hema zao.
Et Josué les bénit et les congédia, et ils regagnèrent leurs tentes.
7 Na kwa nusu ya kabila la Manase, Musa alikuwa amewapa urithi katika Bashani, lakini kwa nusu ya kabila hilo, Yoshua aliwapa urithi karibu na ndugu zao katika nchi magharibi mwa Yordani. Yoshua aliwaaga waende katika hema zao; aliwabarikia,
Or Moïse avait doté une moitié de la Tribu de Manassé en Basan, et Josué avait doté l'autre moitié avec leurs frères en deçà du Jourdain à l'occident. Et aussi lorsque Josué leur permit de regagner leurs tentes, il les bénit
8 na kisha akawaambia, “Rudini katika hema zenu mkiwa na pesa nyingi, na mkiwa na mifugo mingi, pamoja na na fedha, na dhahabu, na shaba na chuma, na nguo nyingi. Gawaneni na ndugu zenu nyara mlizochukua kutoka kwa maadui zenu.
et leur parla en ces termes: C'est avec de grandes richesses que vous retournez à vos tentes, et avec des bestiaux très nombreux, avec de l'argent et de l'or et de l'airain et du fer et des vêtements en très grande quantité. Partagez le butin de vos ennemis avec vos frères.
9 Hivyo, wazawa wa Rubeni, wazawa wa Gadi na nusu ya kabila la Manase walirudi nyumbani, waliwaacha watu wa Isaeli hapo Shilo, ambayo imo ndani ya nchi ya Kanaani. Waliondoka wakaenda katika mkoa wa Gileadi, katika nchi yao, ambayo wao wenyewe waliimiliki, katika utiifu wa amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.
Ainsi s'en retournèrent et partirent les fils de Ruben et les fils de Gad et une moitié de la Tribu de Manassé, d'avec les enfants d'Israël, de Silo dans le pays de Canaan, pour gagner le pays de Galaad, le pays qui était leur propriété, dont ils avaient pris possession sur l'ordre de l'Éternel, transmis par Moïse.
10 Nao walipofika hapo Yordani iliyo katika nchi ya Kanaani, Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase walijenga madhabahu karibu na Yordani, madhabahu kubwa na iliyotokeza na mashuhuri.
Et étant arrivés aux districts du Jourdain dans le pays de Canaan, les fils de Ruben et les fils de Gad et la demi-Tribu de Manassé, bâtirent là un autel sur le Jourdain, autel d'une grande apparence.
11 Watu wa Israeli walisikia habari hizo na wakaseam, “Tazama! Watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wamejenga madhabahu mbele ya nchi ya Kanaani, huko Gelilothi, katika mkoa karibu na Yordani, katika upande ambao ni miliki ya watu wa Israeli.”
Et les enfants d'Israël ouïrent dire: Voilà que les fils de Ruben et les fils de Gad et de la demi-Tribu de Manassé ont bâti l'autel en vue du pays de Canaan, dans les districts du Jourdain en face des enfants d'Israël.
12 Wakati watu wa Israeli waliposikia hivyo, kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika kwa pamoja huko Shilo ili wapande kupigana vita nao.
Et les enfants d'Israël l'ayant appris, toute l'Assemblée des enfants d'Israël se réunit à Silo pour se mettre en campagne contre eux.
13 Kisha watu wa Israeli walituma wajumbe kwa Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi. Walimtuma pia Finehasi mwana wa Eliezari, kuhani,
Et les enfants d'Israël députèrent vers les fils de Ruben et les fils de Gad et la demi-Tribu de Manassé au pays de Galaad, Phinées, fils du Prêtre Eléazar,
14 na viongozi kumi pamoja naye, mmoja kutoka katika familia za mababa wa Israeli, na kila mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa ukoo miongoni mwa watu wa Israeli.
et dix Princes avec lui, un Prince par maison de toutes les Tribus d'Israël, et ils étaient chacun chefs de leurs maisons patriarcales des divisions d'Israël.
15 Walienda kwa watu wa Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakawaambia:
Et ils se rendirent auprès des fils de Ruben et des fils de Gad et de la demi-Tribu de Manassé au pays de Galaad, et ils leur parlèrent en ces termes:
16 “Kusanyiko lote la Yahweh linasema kuwa, ' Ni jambo gani hili lisilo la uaminifu ambalo mmelitenda kinyume na Mungu wa Israeli, kwa kugeuka badala ya kumfuata Yahweh siku hii na kujijengea wenyewe madhabahu katika uasi kinyume na Yahweh katika siku hii?
Ainsi dit toute l'Assemblée de l'Éternel: Qu'est-ce que ce crime dont vous vous rendez coupables envers le Dieu d'Israël, pour vous détourner aujourd'hui de l'Éternel en vous bâtissant un autel pour vous rebeller aujourd'hui contre l'Éternel?
17 Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha? Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo. Kwa ajili ya dhambi ile lilikuja pigo kwa kusanyiko lote la Yahweh.
Est-ce trop peu pour nous que la faute de Pehor dont nous ne sommes pas purifiés jusqu'à ce jour et qui a attiré la plaie sur l'Assemblée de l'Éternel?
18 Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh? Kama mtaasi kinyume na Yahweh leo, kesho atakuwa na hasira na kusanyiko lote la Israeli.
Et vous, vous vous détournez aujourd'hui de l'Éternel! mais si vous vous rebellez aujourd'hui contre l'Éternel, demain Il se courroucera contre toute l'Assemblée d'Israël.
19 Na kama nchi ambayo mnaimiliki imetiwa unajisi, basi mwaweza kuvuka katika nchi ambayo Sanduku la Yahweh lasimama na mjichukulie kwa ajili yenu umiliki miongoni mwetu. Hamtakiwi kuasi kinyume na Yahweh tu, wala kuasi kinyume chetu kwa kujenga madhabahu kwa ajili yenu wenyewe badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wa wetu.
Cependant si le pays qui est votre lot, est impur, passez dans le pays qui est la propriété de l'Éternel où est fixée la Résidence de l'Éternel et prenez possession au milieu de nous; mais ne vous rebellez pas contre l'Éternel, et ne faites pas défection d'avec nous en vous bâtissant un autel en dehors de l'Autel de l'Éternel, notre Dieu.
20 Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli? Mtu yule hakuangamia peke yake kwa uovu wake.
Hacan, fils de Zérah, ne s'est-il pas rendu coupable de crime en touchant aux choses dévouées? et une vengeance fondit sur toute l'Assemblée d'Israël; et il n'a pas été le seul à périr en suite de sa faute.
21 Kisha makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakawajibu wazee wa koo za Israeli:
Alors les fils de Ruben et les fils de Gad et la demi-Tribu de Manassé répondirent et dirent aux Chefs des divisions d'Israël:
22 “Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yeye anajua, na Israeli naijue yenyewe! Kama ilikuwa ni katika uasi au katika kuvunja imani kinyume na Yahweh, msituache hai katika siku hii ya leo
Dieu, Dieu, l'Éternel, Dieu, Dieu, l'Éternel sait, et Israël doit savoir si c'est par une rébellion, par un crime contre l'Éternel (ne nous donne pas Ton aide en ce jour!)
23 kwa ajili ya kujenga madhabahu ili tugeuka na kuacha kumfuata Yahweh. Kama tumejenga madhabahu hii ili kutoa juu yake sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, au sadaka ya amani, basi Yahweh na atuadhibu.
que nous nous sommes bâti un autel, pour nous détourner de l'Éternel; et si c'est pour y offrir des holocaustes et des offrandes, et si c'est pour y faire des sacrifices pacifiques, que l'Éternel nous recherche!
24 La hasha, tulifanya hivyo kwa sababu ya hofu kwamba katika siku zijazo watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu, ' Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?
et si ce n'est pas par un souci, par une raison que nous l'avons fait en disant: A l'avenir vos fils diront à nos fils: « Qu'avez-vous de commun avec l'Éternel, Dieu d'Israël?
25 Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi. Ninyi watu wa Rubeni na watu wa Gadi, hamna kitu chochote naYahweh.' Na kwa hali hiyo, watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.
Aussi bien l'Éternel a mis entre nous et vous, fils de Ruben et fils de Gad, pour limite le Jourdain: vous n'avez point part à l'Éternel. » Et ainsi vos fils empêcheront nos fils de craindre l'Éternel.
26 Basi tukasema, 'Hebu na tujenge sasa madhabahu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa wala si kwa sadaka yoyote ile,
C'est pourquoi nous avons dit: Mettons-nous donc à bâtir un autel, non point pour holocaustes et victimes,
27 ila iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi, na kati ya kizazi chetu baada yetu, kwamba tutafanya ibada ya Yahweh mbele yake, pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa na dhabihu zetu na sadaka zetu za amani, ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, “Hamna sehemu katika Yahweh.”'
mais afin qu'il soit un témoin entre nous et vos fils, et nos descendants après nous, que nous pratiquons le culte de l'Éternel devant Lui avec nos holocaustes et nos victimes et nos sacrifices pacifiques, pour que dans l'avenir vos fils ne disent pas à nos fils: « Vous n'avez point part à l'Éternel! »
28 Hivyo tukasema, 'kama hili litasemwa kwa kwetu au kwa watoto wetu katika siku zijazo, tutasema, “Tazama! Huu ni mfano wa madhabahu ya Yahweh, ambayo mababu zetu waliifanya, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala si kwa dhabihu, bali kwa ajili ya ushahidi kati yetu ninyi.”
Et nous dîmes: Dans le cas où ils tiendraient ce langage à nous ou à nos descendants dans l'avenir, nous répondrons: Voyez la structure de l'autel de l'Éternel qu'ont fait nos pères, non point pour y offrir des holocaustes et des victimes, mais il est un témoin entre nous et vous.
29 Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh, na kuacha kumfuata yeye kwa kujenga madhabahu kwa ajili sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka ya nafaka, au kwa dhabihu, badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wetu ambayo iko mbele ya hema la kukutania.'”
Loin de nous la pensée de nous rebeller contre l'Éternel, et de nous détourner aujourd'hui de l'Éternel en bâtissant un autel pour holocaustes, offrandes et victimes, en dehors de l'Autel de l'Éternel, notre Dieu, qui est devant sa Résidence!
30 Finehasi kuhani na viongozi wa watu, ambao ni wakuu wa koo za Waisraeli ambao walikuwa pamoja naye, waliposikia maneno amabayo watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, kwamba yalikuwa ni mazuri machoni pao.
Et lorsque le Prêtre Phinées et les Princes de l'Assemblée et les Chefs des divisions d'Israël qui l'accompagnaient, eurent entendu les paroles que prononcèrent les fils de Ruben et les fils de Gad et les fils de Manassé, ils furent satisfaits.
31 Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani aliwaambia watu wa Rubeni, Gadi na Manase, “Leo tumejua kwambaYahweh yuko miongoni mwetu, kwa kuwa hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye. Sasa, mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.”
Et Phinées, fils du Prêtre Eléazar, dit aux fils de Ruben et aux fils de Gad et aux fils de Manassé: Aujourd'hui nous reconnaissons que l'Éternel est au milieu de nous, puisque vous ne vous êtes pas rendus coupables envers l'Éternel d'un tel crime. Maintenant vous avez sauvé les enfants d'Israël de la main de l'Éternel.
32 Kisha Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani, na viongozi walirudi kutoka kwa Warubeni na Wagadi, kutoka katika nchi ya Gileadi, na kurudi katika nchi ya Kanaani, kwa watu wa Israeli, na waliwaletea taarifa.
Alors Phinées, fils du Prêtre Eléazar, et les Princes quittant les fils de Ruben et les fils de Gad, revinrent du pays de Galaad dans le pays de Canaan auprès des enfants d'Israël, et ils leur rendirent compte.
33 Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu wa Israeli. Watu wa Israeli walimbarikia Mungu na hawakuendelea kusema tena juu ya kuinua vita dhidi ya Warubeni na Wagadi, ili kuiharibu nchi ambayo walikuwa wanaishi.
Et les enfants d'Israël furent satisfaits, et les enfants d'Israël bénirent Dieu et ils ne parlèrent plus de marcher contre eux pour ravager le pays qu'habitaient les fils de Ruben et les fils de Gad.
34 Warubeni na Wagadi waliita ile madhabahu “Ushahidi,” kwa kuwa walisema, “Ni ushahidi miongoni mwetu kuwa Yahweh ni Mungu.”
Et les fils de Ruben et les fils de Gad donnèrent à l'autel ce nom: « Car il est témoin entre nous que l'Éternel est Dieu. »

< Yoshua 22 >