< Yoshua 22 >

1 Kwa wakati huo, Yoshua aliwaita Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase.
Alors Josué appela les Rubénites, et les Gadites, et la demi-Tribu de Manassé.
2 Aliwaambia, “Mmefanya kila kitu ambacho Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi. Mmeitii sauti yangu katika yote niliyowaagiza.
Et leur dit: Vous avez gardé tout ce que Moïse serviteur de l'Eternel vous avait commandé, et vous avez obéi à ma parole, en tout ce que je vous ai commandé.
3 Bado hamjawaacha ndugu zenu hawa kwa siku zote hizi, mpaka siku hii ya leo. Na mmetimiza wajibu unaotakiwa na amri za Yahweh Mungu wenu.
Vous n'avez pas abandonné vos frères, quoiqu'il y ait longtemps [que vous êtes avec eux], jusqu'à ce jour; mais vous avez pris garde à observer le commandement de l'Eternel votre Dieu.
4 Sasa Yahweh Mungu wenu amewapa pumziko ndugu zenu, kama alivyowaahidi. Hivyo basi, rudini na mwende katika hema zenu katika nchi mnayoimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapeni katika upande mwingine wa Yordani.
Or maintenant l'Eternel votre Dieu a donné du repos à vos frères, selon qu'il leur en avait parlé. Maintenant donc retournez, et allez-vous-en dans vos demeures, en la terre de votre possession, laquelle Moïse, serviteur de l'Eternel, vous a donnée au delà du Jourdain.
5 Lakini zingatieni kuzishika amri na sheria ambazo Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi, kumpenda Yahweh Mungu wenu, kutembea katika njia zake, kuzitunza amri zake, na kuambatana naye na kumwabudu yeye kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.
Prenez seulement bien garde de faire le commandement de la Loi que Moïse serviteur de l'Eternel vous a prescrite, [qui est], que vous aimiez l'Eternel votre Dieu, et que vous marchiez dans toutes ses voies, et que vous gardiez ses commandements, et que vous vous attachiez à lui, et le serviez de tout votre cœur et de toute votre âme.
6 Basi Yoshua akawabariki na kisha akawaacha waende zao, nao wakarudi katika hema zao.
Puis Josué les bénit, et les renvoya; et ils s'en allèrent en leurs demeures.
7 Na kwa nusu ya kabila la Manase, Musa alikuwa amewapa urithi katika Bashani, lakini kwa nusu ya kabila hilo, Yoshua aliwapa urithi karibu na ndugu zao katika nchi magharibi mwa Yordani. Yoshua aliwaaga waende katika hema zao; aliwabarikia,
Or Moïse avait donné à la moitié de la Tribu de Manassé [son héritage] en Basan; et Josué donna à l'autre moitié [son héritage] avec leurs frères au deçà du Jourdain vers l'Occident. Au reste, Josué les renvoyant en leurs demeures, et les bénissant,
8 na kisha akawaambia, “Rudini katika hema zenu mkiwa na pesa nyingi, na mkiwa na mifugo mingi, pamoja na na fedha, na dhahabu, na shaba na chuma, na nguo nyingi. Gawaneni na ndugu zenu nyara mlizochukua kutoka kwa maadui zenu.
Leur parla, en disant: Vous retournez en vos demeures avec de grandes richesses, et avec une fort grande quantité de bétail, avec argent, or, airain, fer, et vêtements, en fort grande abondance; partagez le butin de vos ennemis avec vos frères.
9 Hivyo, wazawa wa Rubeni, wazawa wa Gadi na nusu ya kabila la Manase walirudi nyumbani, waliwaacha watu wa Isaeli hapo Shilo, ambayo imo ndani ya nchi ya Kanaani. Waliondoka wakaenda katika mkoa wa Gileadi, katika nchi yao, ambayo wao wenyewe waliimiliki, katika utiifu wa amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.
Ainsi donc les enfants de Ruben, et les enfants de Gad, et la demi-Tribu de Manassé s'en retournèrent, et partirent de Silo, qui [est] au pays de Canaan, d'avec les enfants d'Israël, pour s'en aller au pays de Galaad, en la terre de leur possession, de laquelle on les avait fait jouir, suivant ce que l'Eternel avait commandé par le moyen de Moïse.
10 Nao walipofika hapo Yordani iliyo katika nchi ya Kanaani, Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase walijenga madhabahu karibu na Yordani, madhabahu kubwa na iliyotokeza na mashuhuri.
Or ils vinrent aux limites du Jourdain, qui étaient au pays de Canaan; et les enfants de Ruben, et les enfants de Gad, et la demi-Tribu de Manassé bâtirent là un autel, joignant le Jourdain, qui était un autel de grande apparence.
11 Watu wa Israeli walisikia habari hizo na wakaseam, “Tazama! Watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wamejenga madhabahu mbele ya nchi ya Kanaani, huko Gelilothi, katika mkoa karibu na Yordani, katika upande ambao ni miliki ya watu wa Israeli.”
Et les enfants d'Israël ouïrent dire: Voilà, les enfants de Ruben, et les enfants de Gad, et la demi-Tribu de Manassé ont bâti un autel regardant vers le pays de Canaan, sur les limites du Jourdain, du côté des enfants d'Israël.
12 Wakati watu wa Israeli waliposikia hivyo, kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika kwa pamoja huko Shilo ili wapande kupigana vita nao.
Les enfants donc d'Israël entendirent cela; et toute l'assemblée des enfants d'Israël s'assembla à Silo, pour monter en bataille contr'eux.
13 Kisha watu wa Israeli walituma wajumbe kwa Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi. Walimtuma pia Finehasi mwana wa Eliezari, kuhani,
Cependant les enfants d'Israël envoyèrent vers les enfants de Ruben, et vers les enfants de Gad, et vers la demi-Tribu de Manassé, au pays de Galaad, Phinées, fils d'Eléazar, le Sacrificateur;
14 na viongozi kumi pamoja naye, mmoja kutoka katika familia za mababa wa Israeli, na kila mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa ukoo miongoni mwa watu wa Israeli.
Et avec lui dix Seigneurs; [savoir] un Seigneur de chaque maison des pères de toutes les Tribus d'Israël; car il y avait dans tous les milliers d'Israël un chef de chaque maison de leurs pères.
15 Walienda kwa watu wa Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakawaambia:
Ceux-ci donc vinrent vers les enfants de Ruben et vers les enfants de Gad, et vers la demi-Tribu de Manassé au pays de Galaad, et leur parlèrent, en disant:
16 “Kusanyiko lote la Yahweh linasema kuwa, ' Ni jambo gani hili lisilo la uaminifu ambalo mmelitenda kinyume na Mungu wa Israeli, kwa kugeuka badala ya kumfuata Yahweh siku hii na kujijengea wenyewe madhabahu katika uasi kinyume na Yahweh katika siku hii?
Ainsi a dit toute l'assemblée de l'Eternel: Quel est ce crime que vous avez commis contre le Dieu d'Israël, vous détournant aujourd'hui de l'Eternel, en vous bâtissant un autel, pour vous révolter aujourd'hui contre l'Eternel?
17 Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha? Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo. Kwa ajili ya dhambi ile lilikuja pigo kwa kusanyiko lote la Yahweh.
Nous fut-ce peu de chose que l'iniquité de Péhor, de laquelle nous ne nous sommes pas encore bien nettoyés jusqu'à aujourd'hui, quoiqu'il en soit venu une plaie sur l'assemblée de l'Eternel?
18 Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh? Kama mtaasi kinyume na Yahweh leo, kesho atakuwa na hasira na kusanyiko lote la Israeli.
Que vous vous détourniez aujourd'hui de l'Eternel, et que vous vous révoltiez aujourd'hui contre l'Eternel, afin que demain sa colère s'allume contre toute l'assemblée d'Israël?
19 Na kama nchi ambayo mnaimiliki imetiwa unajisi, basi mwaweza kuvuka katika nchi ambayo Sanduku la Yahweh lasimama na mjichukulie kwa ajili yenu umiliki miongoni mwetu. Hamtakiwi kuasi kinyume na Yahweh tu, wala kuasi kinyume chetu kwa kujenga madhabahu kwa ajili yenu wenyewe badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wa wetu.
Toutefois si la terre de votre possession est souillée, passez en la terre de la possession de l'Eternel, dans laquelle est placé le pavillon de l'Eternel, et ayez votre possession parmi nous, et ne vous révoltez point contre l'Eternel, et ne soyez point rebelles contre nous, en vous bâtissant un autel, outre l'autel de l'Eternel notre Dieu.
20 Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli? Mtu yule hakuangamia peke yake kwa uovu wake.
Hacan, fils de Zara, ne commit-il pas un crime en prenant de l'interdit, et la colère [de l'Eternel] ne s'alluma-t-elle pas contre toute l'assemblée d'Israël? et cependant cet homme ne mourut pas seul pour son iniquité.
21 Kisha makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakawajibu wazee wa koo za Israeli:
Mais les enfants de Ruben, et les enfants de Gad, et la demi-Tribu de Manassé répondirent, et dirent aux chefs des milliers d'Israël:
22 “Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yeye anajua, na Israeli naijue yenyewe! Kama ilikuwa ni katika uasi au katika kuvunja imani kinyume na Yahweh, msituache hai katika siku hii ya leo
Le Fort, le Dieu, l'Eternel, le Fort, le Dieu, l'Eternel, sait lui-même, et Israël lui-même connaîtra si c'est par révolte, et si c'est pour commettre un crime contre l'Eternel; [en ce cas-là] ne nous protége point aujourd'hui.
23 kwa ajili ya kujenga madhabahu ili tugeuka na kuacha kumfuata Yahweh. Kama tumejenga madhabahu hii ili kutoa juu yake sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, au sadaka ya amani, basi Yahweh na atuadhibu.
Si nous nous sommes bâti un autel pour nous détourner de l'Eternel, et si ç'a été pour y offrir holocauste, ou gâteau, ou si ç'a été pour y faire des sacrifices de prospérités, que l'Eternel lui-même nous en demande compte.
24 La hasha, tulifanya hivyo kwa sababu ya hofu kwamba katika siku zijazo watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu, ' Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?
Et si plutôt nous ne l'avons pas fait, pour crainte de ceci, [savoir] que vos enfants pourraient un jour parler ainsi à nos enfants, et leur dire: Qu'avez-vous à faire avec l'Eternel le Dieu d'Israël?
25 Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi. Ninyi watu wa Rubeni na watu wa Gadi, hamna kitu chochote naYahweh.' Na kwa hali hiyo, watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.
Puisque l'Eternel a mis le Jourdain pour bornes entre nous et vous, enfants de Ruben, et enfants de Gad; vous n'avez point de part à l'Eternel. Et ainsi vos enfants feraient qu'un jour nos enfants cesseraient de craindre l'Eternel.
26 Basi tukasema, 'Hebu na tujenge sasa madhabahu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa wala si kwa sadaka yoyote ile,
C'est pourquoi nous avons dit: Mettons-nous maintenant à bâtir un autel, non pour holocauste, ni pour sacrifice;
27 ila iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi, na kati ya kizazi chetu baada yetu, kwamba tutafanya ibada ya Yahweh mbele yake, pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa na dhabihu zetu na sadaka zetu za amani, ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, “Hamna sehemu katika Yahweh.”'
Mais afin qu'il serve de témoignage entre nous et vous, et entre nos générations après nous, pour faire le service de l'Eternel devant lui en nos holocaustes et nos sacrifices, et en nos sacrifices de prospérités; et afin qu'à l'avenir vos enfants ne disent point à nos enfants: Vous n'avez point de part à l'Eternel.
28 Hivyo tukasema, 'kama hili litasemwa kwa kwetu au kwa watoto wetu katika siku zijazo, tutasema, “Tazama! Huu ni mfano wa madhabahu ya Yahweh, ambayo mababu zetu waliifanya, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala si kwa dhabihu, bali kwa ajili ya ushahidi kati yetu ninyi.”
C'est pourquoi nous avons dit: Lorsqu'ils nous tiendront ce discours, ou à nos générations à l'avenir, nous leur dirons: Voyez la ressemblance de l'autel de l'Eternel que nos pères ont faite, non pour holocauste, ni pour sacrifice, mais afin qu'il soit témoin entre nous et vous.
29 Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh, na kuacha kumfuata yeye kwa kujenga madhabahu kwa ajili sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka ya nafaka, au kwa dhabihu, badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wetu ambayo iko mbele ya hema la kukutania.'”
A Dieu ne plaise que nous nous révoltions contre l'Eternel, et que nous nous détournions aujourd'hui de l'Eternel, en bâtissant un autel pour l'holocauste, pour le gâteau, et pour le sacrifice, outre l'autel de l'Eternel notre Dieu, qui est devant son pavillon.
30 Finehasi kuhani na viongozi wa watu, ambao ni wakuu wa koo za Waisraeli ambao walikuwa pamoja naye, waliposikia maneno amabayo watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, kwamba yalikuwa ni mazuri machoni pao.
Or après que Phinées le Sacrificateur, et les principaux de l'assemblée, les chefs des milliers d'Israël qui étaient avec lui, eurent entendu les paroles que les enfants de Ruben, et les enfants de Gad, et les enfants de Manassé leur dirent, ils furent satisfaits.
31 Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani aliwaambia watu wa Rubeni, Gadi na Manase, “Leo tumejua kwambaYahweh yuko miongoni mwetu, kwa kuwa hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye. Sasa, mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.”
Et Phinées, fils d'Eléazar, le Sacrificateur dit aux enfants de Ruben, et aux enfants de Gad, et aux enfants de Manassé: Nous connaissons aujourd'hui que l'Eternel est parmi nous, puisque vous n'avez point commis ce crime contre l'Eternel; car dès lors vous avez délivré les enfants d'Israël de la main de l'Eternel.
32 Kisha Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani, na viongozi walirudi kutoka kwa Warubeni na Wagadi, kutoka katika nchi ya Gileadi, na kurudi katika nchi ya Kanaani, kwa watu wa Israeli, na waliwaletea taarifa.
Ainsi Phinées, fils d'Eléazar, le Sacrificateur, et ces Seigneurs-là, s'en retournèrent d'avec les enfants de Ruben, et d'avec les enfants de Gad; du pays de Galaad au pays de Canaan, vers les enfants d'Israël, et leur rapportèrent le fait.
33 Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu wa Israeli. Watu wa Israeli walimbarikia Mungu na hawakuendelea kusema tena juu ya kuinua vita dhidi ya Warubeni na Wagadi, ili kuiharibu nchi ambayo walikuwa wanaishi.
Et la chose plut aux enfants d'Israël; et les enfants d'Israël en bénirent Dieu, et ne parlèrent plus de monter en bataille contr'eux pour ruiner le pays où habitaient les enfants de Ruben, et les enfants de Gad.
34 Warubeni na Wagadi waliita ile madhabahu “Ushahidi,” kwa kuwa walisema, “Ni ushahidi miongoni mwetu kuwa Yahweh ni Mungu.”
Et les enfants de Ruben, et les enfants de Gad appelèrent l'autel, Hed; car, [dirent-ils], il est témoin entre nous que l'Eternel est le Dieu.

< Yoshua 22 >