< Yoshua 20 >
1 Baada ya hayo, Yahweh akamwambia Yoshua,
Or l'Éternel parla à Josué, en disant:
2 “Waambia watu wa Israeli, na kusema, 'Chagueni miji ya makimbilio ambayo niliwaambia kupitia kwa Musa.
Parle aux enfants d'Israël, et dis-leur: Établissez-vous les villes de refuge dont je vous ai parlé par l'organe de Moïse;
3 Fanyeni hivi ili mtu akiua mtu bila kukusudia aweze kwenda huko. Miji hii itakuwa ni sehemu ya kukimbilia kutoka kwa mtu yeyote yule anayetaka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu aliyeuliwa.
Afin que le meurtrier qui aura tué quelqu'un par mégarde, sans intention, puisse s'y enfuir; elles vous serviront de refuge contre le vengeur du sang.
4 Atakimbilia kwa mji mmoja miongoni mwa miji hiyo na atasimama mlangoni mwa lango la mji, na ataeleza kesi yake kwa wazee wa mji ule. Kisha watamwingiza ndani ya mji na watampatia sehemu yake ya kuishi miongoni mwao.
Et le meurtrier s'enfuira vers l'une de ces villes; il s'arrêtera à l'entrée de la porte de la ville, et il dira ses raisons aux anciens de cette ville; et ils le recueilleront chez eux dans la ville, et lui donneront un lieu, afin qu'il habite avec eux.
5 Na kama mtu akija akataka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu yule ambaye aliuliwa, ndipo watu wa mji hawatatakiwa kumtoa kwa wenye mamlaka mtu huyo aliyeua. Hawaruhusiwi kufanya hivyo kwasababu alimwua jirani bila kukusudia na hakuwa na chuki naye hapo awali.
Et si le vengeur du sang le poursuit, ils ne livreront point le meurtrier entre ses mains, car il a tué son prochain sans intention et ne le haïssait point auparavant.
6 Ni lazima akae katika mji ule mpaka pale atakapokuwa amesimama mbele ya kusanyiko kwa ajili ya kuhukumiwa, hadi pale atakapokufa mtu yule anayetumika katika nafasi ya kuhani mkuu katka siku hizo. Na kisha mtu yule aliyeua bila kukusudia aweza kurudi nyumbani kwake, katika mji ule ulikotoka.
Mais il demeurera dans cette ville jusqu'à ce qu'il comparaisse en jugement devant l'assemblée, jusqu'à la mort du souverain sacrificateur qui sera en ce temps-là. Alors le meurtrier s'en retournera, et viendra dans sa ville et dans sa maison, dans la ville d'où il se sera enfui.
7 Kwahiyo, Waisraeli wakaichaguia Kedeshi iliyoko Galilaya katika nchi ya milima ya Nafutali, Shekemu katika nchi ya milima ya Efraimu, na Kiriathi Arba (ambayo ndio Herbroni) katika nchi ya milima ya Yuda.
Ils consacrèrent donc Kédès en Galilée, dans la montagne de Nephthali; Sichem, dans la montagne d'Éphraïm; et Kirjath-Arba, qui est Hébron, dans la montagne de Juda.
8 Katika ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko, walichagua mji wa Bezeri huko nyikani katika nyanda za kabila la Rubeni; na Ramothi Gileadi kutoka kabila la Gadi; na Golani katika Bashani, kutoka katika kabila la Manase.
Et au delà du Jourdain de Jérico, au levant, ils établirent, dans la tribu de Ruben, Betser au désert, dans la plaine; Ramoth en Galaad, dans la tribu de Gad; et Golan en Bassan, dans la tribu de Manassé.
9 Hii ni miji iliyochaguliwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwao, ili kwamba mtu yeyote amwuaye mtu bila kukusudia aweza kukimbilia huko kwa ajili ya kupata usalama. Mtu huyu hatakufa kwa mkono wa mtu yule anayetake kulipiza kisasi cha damu iliyomwagwa, mpaka hapo kwanza mtuhumiwa atakaposimama mbele ya kusanyiko la watu.
Telles furent les villes assignées à tous les enfants d'Israël et à l'étranger séjournant parmi eux, afin que quiconque aurait tué quelqu'un par mégarde pût s'y enfuir, et ne mourût point par la main du vengeur du sang, jusqu'à ce qu'il comparût devant l'assemblée.