< Yoshua 2 >
1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni aliwatuma watu wawili kwa siri kama wapelelezi kutoka Shitimu. Akisema, “Nendeni mkaiangalie nchi, hasa Yeriko.” Walienda na wakafika katika nyumba ya kahaba ambaye jina lake ni Rahabu, na wakalala hapo.
And Joshua, the son of Nun, had sent out from Shittim two men as spies, secretly, saying, Go ye, view the land and especially Jericho; and they went, and came unto the house of a woman, a harlot, whose name was Rachab, and they lodged there.
2 Mfalme wa Yeriko aliambiwa, “Tazama watu wa Israeli wamekuja kuipeleleza nchi.”
And it was told unto the king of Jericho, saying, Behold, men came in hither this night, of the children of Israel, to search out the country.
3 Mfalme akatuma neno kwa Rahabu kusema, “Watoe watu waliokuja kwako ambao wameingia nyumbani mwako, kwa kuwa wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
And the king of Jericho sent to Rachab, saying, Bring forth the men who are come to thee, who came to thy house; for, to search out all the country are they come.
4 Lakini mwanamke alikuwa amekwisha kuwachukua wale watu wawili na kuwaficha. Na akasema, “Ndiyo, watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
But the woman had taken the two men, and hidden them; and she said, It is true, the men came unto me, but I knew not whence they were.
5 Ilipokuwa jioni wakati wa kufungwa kwa lango la mji, waliondoka. Sijui mahali walikoelekea. Mnaweza kuwakamata kama mtawafuata upesi.
And it came to pass, about the time of shutting the gate, when it was dark, that the men went out; I know not whither the men are gone: pursue quickly after them, for ye can overtake them.
6 Lakini yeye aliwapandisha juu darini na kuwaficha kwa mabua ya kitani ambayo alikuwa ameyalaza darini.
But she had brought them up to the roof, and had hidden them among the stalks of flax, which she had laid in order upon the roof.
7 Hivyo, watu waliwafuatilia njiani iliyoeleka katika vivuko vya Yordani. Na milango ilifungwa mara tu baada ya wale watu waliofuata kutoka nje.
And the men pursued after them, by the way to the Jordan unto the fords; and the gate was closed, as soon as those who pursued after them were gone out.
8 Wale wanaume walikuwa hajalala usiku, wakati alipowaendea kule darini.
But they had not yet laid themselves down, when she came up unto them upon the roof.
9 Akawaambia, “Ninajua kwamba Yahweh amewapa ninyi nchi na kwamba hofu juu yenu imetuingia. Watu wote wanaoishi katika nchi watayeyuka mbele yenu.
And she said unto them, I know that the Lord hath given you the land, and that the terror of you hath fallen upon us, and that all the inhabitants of the land are become faint-hearted, because of you.
10 Tumesikia jinsi ambavyo Yahweh alivyokausha maji ya Bahari ya Mianzi kwa ajili yenu wakati mkitoka Misri. Na tumesikia mlichokifanya kwa wafalme wawili wa Waamori walioko upande mwingine wa Yordani - Sihoni na Ogu - ambao mmewaangamiza kabisa.
For we have heard, how that the Lord dried up the waters of the Red Sea before you, when ye went forth out of Egypt; and what ye have done unto the two kings of the Emorites, who were on the other side of the Jordan, unto Sichon and 'Og, whom ye have utterly destroyed.
11 Mara tu tuliposikia, mioyo yetu iliyeyuka na hapakuwa na ujasiri wowote uliosalia kwa mtu yeyote - kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ni Mungu aliye juu mbinguni na chini duniani.
And when we heard this, our heart melted, and there remained not any more courage in any man, because of you; for the Lord your God is alone God in the heavens above, and upon the earth beneath.
12 Sasa basi, tafadhali mniapie kwa Yahweh kwamba kama nilivyokuwa mwema kweu, nanyi pia mtaitendea mema nyumba ya baba yangu. Nipeni ishara ya uhakika
And now swear, I pray you, unto me by the Lord, because I have shown you kindness, that ye will also, for your part, show kindness, unto my father's house; and give me a sure token,
13 kwamba mtanihifadhi maisha ya baba, mama, kaka, dada zangu na famiie zao, na kwamba mtatuokoa kutoka katika kifo.
That ye will preserve the life of my father, and my mother, and my brothers, and my sisters, and all that they have, and deliver our lives from death.
14 Wanaume wakamjibu, “maisha yetu kwa ajili ya yenu, hata kifo! Kama hamtasema habari zetu, na Yahweh akisha kutupa nchi hii, tutakuwa wenye huruma na waaminifu kwenu.”
And the men said unto her, Our life shall be [doomed] to death instead of yours, if ye tell not this our business; and it shall be, when the Lord giveth us the land, that we will show thee kindness and truth.
15 hivyo aliwashusha chini kwa kupitia dirishani kwa kutumia kamba. Nyumba ambayo alikuwa anaishi ilijengwa katika ukuta wa mji.
Then she let them down by a cord through the window; for her house was within the town wall, and within the wall she dwelt.
16 Akawaambia, “Nendeni milimani la sivyo watu waliowafuata watawaona. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watu waliowafuata watakaporudi. Kisha nendeni zenu.”
And she said unto them, Get you to the mountain, lest the pursuers meet with you; and hide yourselves there three days, until the pursuers be returned; and afterward ye may go your way.
17 Wanaume wakamwambia, “Hatutakuwa tumefungwa na ahadi ulizotufanya tuape mbele zako, kama hautalifanya hili.
And the men said unto her, We will be blameless of this thy oath which thou hast caused us to swear.
18 Tutakapokuja katika nchi, ni lazima uifunge kamba hii nyekundu katika dirisha ulilotushushia chini, na utawakusanya katika nyumba baba yako, mama yako, kaka zako na wote wa nyumba ya baba yako.
Behold, when we come into the land, this line of scarlet thread shalt thou bind in the window by which thou hast let us down; and thy father, and thy mother, and thy brothers, and all thy father's household, thou must bring together unto thee into the house.
19 Na yeyote aendaye mtaani nje ya milango ya nyumba yako, damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao na hatutakuwa na hatia yoyote. Lakini kama mkono utanyoshwa juu ya mtu yeyote aliye pamoja nawe katika nyumba, damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
And it shall be, that whosoever will go out of the doors of thy house into the street, his blood shall be upon his head, and we will be guiltless; and whosoever will remain with thee in the house, his blood shall be on our head, if a hand be laid upon him.
20 Na ikiwa utaongea juu ya suala letu, tutakuwa huru dhidi ya kiapo ulichotuapisha.
And if thou tell this our business, then will we be free of thy oath which thou hast caused us to swear.
21 Rahabu akawajibu, “Yote mliyosema nayatimie.” Akawatoa mbali na wakaondoka. Kisha akaifunga kamba nyekundu katika dirisha.
And she said, According unto your words, so be it; and she dismissed them, and they departed; and she bound the scarlet line in the window.
22 Wakaondoka na kwenda juu milimani na walikaa huko kwa siku tatu hadi pale wale waliowafuatilia waliporudi. Wale waliowafuata walitafuta njiani pote bila kuwaona.
And they went, and came unto the mountain, and they remained there three days, until the pursuers were returned; and the pursuers sought throughout all the way, but found nothing.
23 Wale watu wawili walirudi na kuvuka mto na wakafika kwa Yoshua mwana wa Nuni, na walimwambia kila kitu kilichotokea kwao.
And the two men returned, and descended from the mountain, and passed over, and came to Joshua the son of Nun, and related to him all the things that had befallen them.
24 Nao wakasema kwa Joshua, “kwa kweli Yahweh ametupa nchi hii. Wenyeji wote wa nchi wanayeyuka kwasababu yetu.
And they said unto Joshua, Truly the Lord hath given up into our hand all the country; for all the inhabitants of the country are already become faint-hearted because of us.