< Yoshua 19 >

1 Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
Ikkinchi chek Shiméon’gha chiqti, yeni Shiméonlar qebilisige jemet-aililiri boyiche tartildi; ularning mirasi bolsa Yehudalarning miras ülüshining arisida idi.
2 Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
Ularning érishken mirasi ichide Beer-Shéba, Shéba, Moladah,
3 Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
Hazar-Shual, Balah, Ézem,
4 Elitoladi, Bethuli na Horma.
Eltolad, Bitul, Xormah,
5 Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
Ziklag, Beyt-Markabot, Hazar-Susah,
6 Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
Beyt-Libaot we Sharuhen bolup, jemiy on üch sheher we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar idi.
7 Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
Buningdin bashqa yene Ayin, Rimmon, Éter, Ashan bolup, jemiy töt sheher we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar
8 Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
Hemde jenub tereptiki Baalat-Beer (yeni jenubdiki Ramah)ghiche bolghan bu [töt] sheherning etrapidiki hemme kent-qishlaqlarmu bar idi. Bular Shiméonlar qebilisining ülüshi bolup, jemet-aililiri boyiche érishken mirasi idi.
9 Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
Shiméonlarning miras ülüshi Yehudalarning ülüshining ichidin élip bérildi; chunki Yehudalarning miras ülüshi özlirige köplük qilghanidi, shunga Shiméonlarning miras ülüshi ularning miras ülüshining ichidin bérildi.
10 Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
Üchinchi chek Zebulunlar qebilisige jemet-aililiri boyiche tartildi; ularning miras chégrisi Saridqa baratti,
11 Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
chégrisi gherb terepte Maréalahqa bérip Dabbeshetke yétip Yoknéamning udulidiki éqin’gha tutishatti;
12 Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
U Saridtin sherq teripige qayrilip, kün chiqishqa burulup Kislot-Tabor yurtigha tutiship, Dabiratqa ötüp, Yafiyagha bardi;
13 Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
andin shu yerdin u sherq teripige kün chiqishqa [yene] burulup, Gat-Hefer we Et-Kazin’gha kélip Néahqa sozulghan Rimmon yurtigha yétip bardi.
14 Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
Andin u yerdin shimal terepke qayrilip, Hannaton’gha yétip bérip, Yiftah-Elning jilghisida axirlashti.
15 Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Ularning ülüshi yene Kattat, Nahalal, Shimron, Yidalah we Beyt-Lehemnimu orap, jemiy on ikki sheher we ulargha qarashliq kent-qishlaqlarnimu öz ichige alatti.
16 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Bu bolsa, yeni bu sheherler we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar Zebulunlarning miras ülüshi bolup, jemet-aililiri boyiche ulargha bérilgenidi.
17 Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
Tötinchi chek Issakargha chiqti, yeni Issakarlar qebilisige jemet-aililiri boyiche tartildi;
18 Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
ulargha bérilgen yurtlar Yizreelgiche bolup, Kesullot, Shunem,
19 Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
Hafarayim, Shion, Anaharat,
20 Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
Rabbit, Kishion, Ébez,
21 Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
Remet, En-Gannim, En-Haddah we Beyt-Pazzezni öz ichige aldi;
22 Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
andin chégrisi Tabor, Shahazimah we Beyt-Shemeshke yétip, Iordan deryasida axirlashti; ularning ülüshi jemiy on alte sheher we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar idi.
23 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Bu bolsa, yeni bu sheherler we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar Issakarlarning miras ülüshi bolup, jemet-aililiri boyiche ulargha bérilgenidi.
24 Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
Beshinchi chek Ashirlar qebilisige jemet-aililiri boyiche tartildi;
25 Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
ularning zémini Helkat, Hali, Beten, Aqsaf,
26 Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
Allammelek, Améad we Mishalni öz ichige aldi; chégrisi gherb terepte Karmel bilen Shihor-Libnatqa tutiship,
27 Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
andin sherq terepke qayrilip Beyt-Dagon’gha bérip, Zebulun [zémini] bilen Yiftah-El jilghisining shimal teripidin ötüp, Beyt-Émek bilen Néielge yétip bérip Kabulning shimal teripige chiqti;
28 Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
Ébron, Rehob, Hammon we Kanahni öz ichige élip Chong Zidon’gha yétip bardi.
29 Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
andin chégrisi Ramah teripige qayrilip, Tur dégen mustehkem shehirge bérip, Xosahqa qayrilip, Aqzib bilen Hebelge tutash bolghan déngizda axirlashti;
30 Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
zémini Ummah, Afek we Rehobnimu öz ichige alghan; jemiy yigirme ikki sheher we ulargha qarashliq kent-qishlaqlarni öz ichige alghanidi.
31 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Bu bolsa, yeni bu sheherler we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar Ashirlarning miras ülüshi bolup, jemet-aililiri boyiche ulargha bérilgenidi.
32 Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
Altinchi chek Naftaligha chiqti, yeni Naftalilar qebilisige jemet-aililiri boyiche tartildi;
33 Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
ularning chégrisi bolsa Heleftin chiqip, Zaanannimdiki dub derixidin ötüp, Adami-Nekeb we Yabneeldin chiqip, Lakkumgha yétip Iordan deryasigha bérip axirlashti.
34 Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
Andin gherb terepke qayrilip Aznot-Taborgha bérip, shu yerdin Hukkokqa chiqip, jenubta Zebulunning ülüsh zéminigha tutiship, shimalda Ashirning ülüsh zéminigha yétip, kün chiqish teripide Iordan deryasining yénida, Yehudaning ülüsh zéminigha ulashti.
35 Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
Naftalining mustehkem sheherliri Ziddim, Zer, Hammat, Rakkat, Kinneret,
36 Adama, Rama, Hazori,
Adamah, Ramah, Hazor,
37 Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
Kedesh, Edrey, En-Hazor,
38 Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
Yiron, Migdal-El, Horem, Beyt-Anat we Beyt-Shemeshler bolup, jemiy on toqquz sheher we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar idi.
39 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
Bu bolsa, yeni bu sheherler we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar Naftalilar qebilisining miras ülüshi bolup, jemet-aililiri boyiche ulargha bérilgenidi.
40 Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
Yettinchi chek Danlarning qebilisige chiqti; u ularning jemet-aililiri boyiche tartildi.
41 Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
Ularning miras zémini bolsa Zoréah, Eshtaol, Ir-Shemesh,
42 Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
Shaalabbin, Ayjalon, Yitlah,
43 Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
Élon, Timnatah, Ekron,
44 Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
El-tekeh, Gibbéton, Baalat,
45 Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
Yehud, Bene-Barak, Gat-Rimmon,
46 Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
Me-Yarkon, Rakkon we Yafoning udulidiki yurtni öz ichige aldi.
47 Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
Lékin Danlarning zémini öz qolidin ketken bolghachqa, Danlar chiqip Leshemge hujum qilip uni ishghal qildi; ahalisini qilichlap yoqitip, u yerni özining qilip makanlashti; andin ular Leshemge atisi Danning ismini qoyup, uni Dan dep atidi.
48 Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Mana bular, yeni bu sheherler we ulargha qarashliq kent-qishlaqlar Danlar qebilisige, ularning jemet-aililiri boyiche miras qilip bérilgenidi.
49 Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
Bu teriqide [Israillar] zéminni chégra-chégra boyiche bölüp boldi; andin ular Nunning oghli Yeshuagha öz arisidin miras bölüp berdi.
50 Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
Perwerdigarning buyruqi boyiche Yeshua tiliginidek uninggha Efraim taghliq yurtidiki Timnat-Sérah dégen sheherni berdi; buning bilen u sheherni qurup chiqip, uningda turdi.
51 Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.
Mana bular Eliazar kahin bilen Nunning oghli Yeshua we Israilning qebile-jemetlirining kattabashliri bir bolup Shilohda, jamaet chédirining derwazisining aldida turup, Perwerdigarning aldida chek tashlap bölüp teqsim qilghan miraslardur. Bu teriqide ular zéminning teqsimatini tügetti.

< Yoshua 19 >