< Yoshua 19 >
1 Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
E saiu a segunda sorte por Simeão, pela tribo dos filhos de Simeão, segundo as suas famílias: e foi a sua herança no meio da herança dos filhos de Judá.
2 Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
E tiveram na sua herança: Beer-seba, e Seba, e Molada,
3 Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
E Hassar-sual, e Bala, e Asem,
4 Elitoladi, Bethuli na Horma.
E Eltholad, e Bethul, e Horma,
5 Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
E Siklag, e Beth-hammarcaboth, e Hassar-susa,
6 Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
E Beth-lebaoth, e Saruhen: treze cidades e as suas aldeias.
7 Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
Ain, e Rimmon, e Ether, e Asan: quatro cidades e as suas aldeias.
8 Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
E todas as aldeias que havia em redor destas cidades, até Baalath-beer, que é Ramath do sul: esta é a herança da tribo dos filhos de Simeão, segundo as suas famílias.
9 Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
A herança dos filhos de Simeão está entre o quinhão dos de Judá; porquanto a herança dos filhos de Judá era demasiadamente grande para eles: pelo que os filhos de Simeão tiveram a sua herança no meio deles.
10 Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
E saiu a terceira sorte pelos filhos de Zebulon, segundo as suas famílias: e foi o termo da sua herança até Sarid.
11 Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
E sobe o seu termo pelo ocidente a Marala, e chega até Dabbeseth: chega também até ao ribeiro que está defronte de Jokneam.
12 Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
E de Sarid volta para o oriente, para o nascente do sol, até ao termo de Chisloth-tabor, e sai a Dobrath, e vai subindo a Japhia.
13 Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
E dali passa pelo oriente para o nascente, a Gath-hepher, em Ethcasin; e sai a Rimmon-methoar, que é Nea.
14 Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
E torna este termo para o norte a Hannathon: e as suas saídas são o vale de Iphtah-el,
15 Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
E Cattath, e Nahalal, e Simron, e Idala, e Beth-lehem: doze cidades e as suas aldeias.
16 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta é a herança dos filhos de Zebulon, segundo as suas famílias: estas cidades e as suas aldeias.
17 Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
A quarta sorte saiu por Issacar: pelos filhos de issacar, segundo as suas famílias.
18 Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
E foi o seu termo Jezreela, e Chesulloth, e Sunem,
19 Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
E Hapharaim. e Sion, e Anacarath,
20 Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
E Rabbith, e Kision, e Ebes,
21 Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
E Remeth, e En-gannim, e En-Hadda, e Beth-patses.
22 Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
E chega este termo até Tabor, e Sahasima, e Beth-semes; e as saídas do seu termo estão para o Jordão: dezeseis cidades e as suas aldeias.
23 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta é a herança da tribo dos filhos de issacar, segundo as suas famílias: estas cidades e as suas aldeias.
24 Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
E saiu a quinta sorte pela tribo dos filhos de Aser, segundo as suas famílias.
25 Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
E foi o seu termo Helkath, e Hali, e Beten, e Acsaph,
26 Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
E Alammelech, e Amad, e Misal: e chega a Carmel para o ocidente, e a Sihor-libnath;
27 Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
E volta do nascente do sol a beth-dagOn, e chega a Zebulon e ao vale de Iphtah-el, ao norte de Beth-emek e de Neiel, e vem sair a Cabul pela esquerda,
28 Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
E Ebron, e Rehob, e Hammon, e Cana, até à grande Sidon.
29 Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
E volta este termo a Rama, e até à forte cidade de Tiro: então torna este termo a Hosa, e as suas saídas estão para o mar, desde o quinhão da terra até Achzib;
30 Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
E Uma, e Aphek, e Rechob: vinte e duas cidades e as suas aldeias.
31 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta é a herança da tribo dos filhos de Aser, segundo as suas famílias: estas cidades e as suas aldeias.
32 Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
E saiu a sexta sorte pelos filhos de Naphtali; para os filhos de Naphtali, segundo as suas famílias.
33 Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
E foi o seu termo desde Heleph e desde Allon em Saanannim, e Adami, Nekeb, e Jabneel, até Lakum: e estão as suas saídas no Jordão.
34 Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
E volta este termo pelo ocidente a Azmoth-tabor, e dali passa a Huccok: e chega a Zebulon para o sul, e chega a Aser para o ocidente, e a Judá pelo Jordão, para o nascente do sol.
35 Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
E são as cidades fortes: Siddim, Ser, e Hammath, Raccath, e Chinnereth,
E Adama, e Rama, e Hasor,
37 Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
E Kedes, e Edrei, e En-hazor,
38 Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
E Iron, e Migdal-el, Horem, e Beth-anath, e Beth-semes: dezenove cidades e as suas aldeias.
39 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
Esta é a herança da tribo dos filhos de Naphtali, segundo as suas famílias: estas cidades e as suas aldeias.
40 Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
A sétima sorte saiu pela tribo dos filhos de Dan, segundo as suas famílias.
41 Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
E foi o termo da sua herança, Sora, e Estaol, e Ir-semes,
42 Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
E Saalabbin, e Ayalon, e Ithla,
43 Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
E Elon, e Timnath, e Ekron,
44 Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
E Elteke, e Gibthon, e Baalath,
45 Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
E Jehud, e Bene-berak, e Gath-rimmon,
46 Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
E Me-jarcom, e Raccon: com o termo defronte de Japho:
47 Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
Saiu porém pequeno o termo aos filhos de Dan: pelo que subiram os filhos de Dan, e pelejaram contra Lesem, e a tomaram, e a feriram ao fio da espada, e a possuiram e habitaram nela, e a Lesem chamaram Dan, conforme ao nome de Dan seu pai.
48 Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta é a herança da tribo dos filhos de Dan, segundo as suas famílias; estas cidades e as suas aldeias.
49 Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
Acabando pois de repartir a terra em herança segundo os seus termos, deram os filhos de Israel a Josué, filho de Nun, herança no meio deles.
50 Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
Segundo o dito do Senhor lhe deram a cidade que pediu, a Timnath-serah, na montanha de Ephraim: e reedificou aquela cidade, e habitou nela.
51 Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.
Estas são as heranças que Eleazar o sacerdote, e Josué filho de Nun, e os Cabeças dos pais das famílias por sorte em herança repartiram às tribos dos filhos de Israel em Silo, perante o Senhor, à porta da tenda da congregação. E assim acabaram de repartir a terra.