< Yoshua 19 >

1 Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
Potem padł drugi los dla Symeona, dla pokolenia synów Symeona według ich rodzin, a ich dziedzictwo znajdowało się pośród dziedzictwa synów Judy.
2 Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
A otrzymali oni w dziedzictwie: Beer-Szeba, Szeba, Molada;
3 Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
Chasar-Szual, Bala, Esem;
4 Elitoladi, Bethuli na Horma.
Eltolad, Betul, Chorma;
5 Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
Siklag, Bet-Markabot, Chasar-Susa;
6 Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
Bet-Lebaot i Szaruchen: trzynaście miast wraz z przyległymi do nich wioskami.
7 Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
Ain, Rimmon, Eter, Aszan: cztery miasta wraz z przyległymi do nich wioskami.
8 Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
Oraz wszystkie wioski, które były dokoła tych miast, aż do Baalat-Beer, Ramat południowy. To było dziedzictwo pokolenia synów Symeona według ich rodzin.
9 Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
Dziedzictwo synów Symeona zostało wzięte z działu synów Judy, ponieważ dział synów Judy był dla nich zbyt wielki. Synowie Symeona otrzymali więc dziedzictwo pośród ich dziedzictwa.
10 Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
Potem padł trzeci los dla synów Zebulona według ich rodzin, a granica ich dziedzictwa sięgała aż do Sarid.
11 Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
A ich granica wznosiła się w kierunku morza do Marala, dochodziła do Dabbeszet i ciągnęła się aż do potoku, który jest naprzeciw Jokneam.
12 Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
I zwracała się od Sarid na wschód do granicy Kislot-Tabor, a [stamtąd] biegła do Daberat i wznosiła się [do] Jafia;
13 Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
Stamtąd biegła na wschód do Gat-Chefer, do Et-Kasin, dochodziła do Rimmon i skręcała do Nea.
14 Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
Następnie granica otaczała od północy do Channaton i kończyła się w dolinie Jiftach-El.
15 Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
[Obejmowała] również Kattat, Nahalal, Szimron, Idala i Betlejem: dwanaście miast wraz z przyległymi do nich wioskami.
16 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Oto dziedzictwo synów Zebulona według ich rodzin, te miasta i przyległe do nich wioski.
17 Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
Czwarty los przypadł Issacharowi, [czyli] synom Issachara według ich rodzin.
18 Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
A ich granica obejmowała: Jizreel, Kesulot, Szunem;
19 Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
Chafaraim, Szijon, Anacharat;
20 Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
Rabbit, Kiszjon, Ebes;
21 Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
Remet, En-Gannim, En-Chadda i Bet-Passes.
22 Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
A [ich] granica dochodziła do Taboru, Szachasima i Bet-Szemesz, a kończyła się przy Jordanie: szesnaście miast i przyległe do nich wioski.
23 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Oto dziedzictwo pokolenia synów Issachara według ich rodzin, te miasta oraz przyległe do nich wioski.
24 Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
Potem padł piąty los dla pokolenia synów Aszera według ich rodzin.
25 Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
I ich granica obejmowała: Chelkat, Chali, Beten, Akszaf;
26 Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
Alammelek, Amad i Miszal, a dochodziła do Karmelu na zachodzie i do Szichor-Libnat.
27 Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
Stamtąd skręcała na wschód do Bet-Dagon i biegła aż do Zebulona i do doliny Jiftach-El na północ od Bet-Emek i Neiel i wychodziła do Kabulu po lewej stronie;
28 Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
I [do] Ebronu, Rechobu, Chammonu i Kany aż do Wielkiego Sydonu.
29 Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
Potem granica skręcała do Rama aż do warownego miasta Tyr; stamtąd skręcała do Chosa i kończyła się przy morzu, od wybrzeża do Akzibu.
30 Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
[Obejmowała] również Umma, Afek i Rechob: dwadzieścia dwa miasta oraz przyległe do nich wioski.
31 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Oto dziedzictwo pokolenia synów Aszera według ich rodzin, te miasta i przyległe do nich wioski.
32 Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
[Potem] dla synów Neftalego padł szósty los, dla synów Neftalego według ich rodzin.
33 Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
Ich granica biegła od Chelef, od Helon do Saanannim, Adami, czyli Nekeb, oraz Jabneel aż do Lakum i kończyła się [przy] Jordanie.
34 Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
Następnie ta granica skręcała na zachód [do] Aznot-Tabor, a stamtąd biegła do Chukkok i ciągnęła się na południe do Zebulona, na zachodzie dochodziła do Aszera, a do Judy nad Jordanem na wschodzie.
35 Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
A miastami warownymi [są]: Siddim, Ser, Chammat, Rakkat, Kinneret;
36 Adama, Rama, Hazori,
Adama, Rama, Chasor;
37 Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
Kedesz, Edrei, En-Chasor;
38 Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
Jereon, Migdal-El, Chorem, Bet-Anat i Bet-Szemesz: dziewiętnaście miast oraz przyległe do nich wioski.
39 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
Oto dziedzictwo pokolenia synów Neftalego według ich rodzin, te miasta oraz przyległe do nich wioski.
40 Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
[Potem] padł siódmy los dla pokolenia synów Dana według ich rodzin.
41 Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
A granica ich dziedzictwa obejmowała: Sorea, Esztaol, Ir-Szemesz;
42 Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
Szaalabin, Ajjalon, Jitla;
43 Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
Elon, Timna, Ekron;
44 Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
Elteke, Gibbeton, Baalat;
45 Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
Jehud, Bene-Berak, Gat-Rimmon;
46 Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
Me-Jarkon i Rakkon z granicą naprzeciw Jafy.
47 Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
Lecz obszar synów Dana był zbyt mały. Synowie Dana wyruszyli więc do walki z Leszem, zdobyli je, pobili je ostrzem miecza, wzięli je w dziedzictwo i mieszkali w nim. I nazwali Leszem Dan, od imienia swego ojca.
48 Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Oto dziedzictwo pokolenia synów Dana według ich rodzin, te miasta oraz przyległe do nich wioski.
49 Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
A gdy dokończyli dzielenie ziemi według jej granic, synowie Izraela dali spośród siebie dziedzictwo Jozuemu, synowi Nuna.
50 Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
Zgodnie z rozkazem PANA dali mu miasto, o które poprosił, Timnat-Serach na górze Efraim, gdzie zbudował miasto i mieszkał w nim.
51 Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.
Oto dziedzictwa, które losem podzielili w posiadanie kapłan Eleazar, Jozue, syn Nuna, i naczelnicy ojców pokoleń synów Izraela w Szilo przed PANEM, u wejścia do Namiotu Zgromadzenia, i dokończyli podział ziemi.

< Yoshua 19 >