< Yoshua 18 >

1 Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
Og hele Israels barns menighet samlet sig i Silo og reiste der sammenkomstens telt; og landet lå undertvunget foran dem.
2 Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
Men det var ennu syv stammer tilbake blandt Israels barn som ikke hadde delt sin arv.
3 Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
Da sa Josva til Israels barn: Hvor lenge vil I ennu dryge før I drar avsted og inntar det land Herren, eders fedres Gud, har gitt eder?
4 Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
Kom nu med tre menn for hver stamme! Så vil jeg sende dem ut, og de skal gjøre sig rede og gå igjennem landet og skrive op det de ser, for utskiftningens skyld, og så komme tilbake til mig.
5 Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
Del det så mellem eder i syv deler! Juda skal bli i sitt land mot syd, og Josefs hus skal bli i sitt land mot nord.
6 Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
Og I skal skrive op alt det som er i landet, i syv deler, og komme hit til mig med det I har skrevet; så vil jeg kaste lodd for eder her, for Herrens, vår Guds åsyn.
7 Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
For levittene får ingen del blandt eder, men Herrens prestedømme er deres arv; og Gad og Ruben og den halve Manasse stamme har fått sin arv på østsiden av Jordan - den arv som Moses, Herrens tjener, gav dem.
8 Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
Så gjorde mennene sig rede og gikk; og da de drog avsted, bød Josva dem å skrive op alt det de så i landet; han sa: Gå avsted og dra omkring i landet og skriv op alt det I ser der, og kom så tilbake til mig! Så vil jeg kaste lodd for eder for Herrens åsyn her i Silo.
9 Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
Så gikk da mennene avsted og drog gjennem landet og skrev op det de så der, by for by, i en bok i syv deler; derefter kom de tilbake til Josva i leiren ved Silo.
10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
Og Josva kastet lodd for dem i Silo for Herrens åsyn; der skiftet Josva landet mellem Israels barn efter deres ættegrener.
11 Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
Først kom loddet ut for Benjamins barns stamme efter deres ætter; og det land som blev deres lodd, kom til å ligge mellem Judas barn og Josefs barn.
12 Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
Og deres grense på nordsiden gikk ut fra Jordan og drog sig opover til fjellryggen i nord for Jeriko og derefter vestover op i fjellet og frem til ørkenen ved Bet-Aven.
13 Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
Derfra gikk grensen over til Luz, til fjellryggen i syd for Luz, det er Betel; og så gikk grensen ned til Atrot-Addar over det fjell som ligger sønnenfor Nedre-Bet-Horon.
14 Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
Så gjorde grensen en sving og bøide sig på vestsiden mot syd fra det fjell som ligger rett i syd for Bet-Horon, og den endte ved Kirjat-Ba'al, det er Kirjat-Jearim, en by som tilhørte Judas barn. Dette var vestsiden.
15 Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
På sydsiden gikk grensen fra enden av Kirjat-Jearim - der var det grensen begynte i vest - og frem til Neftoah-vannets kilde.
16 Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
Så gikk grensen ned til enden av det fjell som ligger midt imot Hinnoms sønns dal, nordenfor Refa'im-dalen, og så ned i Hinnoms dal, i syd for jebusittenes fjellrygg, og derefter ned til En-Rogel.
17 Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
Så svinget den mot nord og gikk frem til En-Semes og videre til Gelilot, som ligger midt imot Adummim-skaret, og så ned til den sten som har navn efter Bohan, Rubens sønn.
18 Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
Der tok den over til den fjellrygg som ligger rett i nord for Ha'araba, og gikk derefter ned til Ha'araba.
19 Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
Så tok grensen over til nordsiden av fjellryggen ved Bet-Hogla og endte ved den nordlige bukt av Salthavet, ved Jordans sydende. Dette var sydgrensen.
20 Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
På østsiden var Jordan grensen. Dette var Benjamins barns arvelodd med dens grenser rundt omkring, efter deres ætter.
21 Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
Og de byer som tilfalt Benjamins barns stamme efter deres ætter, var: Jeriko og Bet-Hogla og Emek-Kesis
22 Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
og Bet-Ha'araba og Semara'im og Betel
23 Avimu, Para, Ofra,
og Ha'avvim og Happara og Ofra
24 Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
og Kefar-Ha'ammoni og Haofni og Geba - tolv byer med tilhørende landsbyer;
25 Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
Gibeon og Rama og Be'erot
26 Mizpe, Kefira, Moza,
og Mispe og Hakkefira og Hammosa
27 Rekemu, Iripeeli, Tarala,
og Rekem og Jirpe'el og Tarala
28 Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.
og Sela, Haelef og Jebus, det er Jerusalem, Gibat, Kirjat - fjorten byer med tilhørende landsbyer. Dette var Benjamins barns arvelodd efter deres ætter.

< Yoshua 18 >