< Yoshua 18 >

1 Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
Tous les enfants d’Israël s’assemblèrent à Silo, et là ils dressèrent le tabernacle de témoignage, et la terre leur fut soumise.
2 Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
Or, étaient restées sept tribus des enfants d’Israël, lesquelles n’avaient pas encore reçu leurs possessions.
3 Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
Josué leur dit: Jusqu’à quand languirez-vous dans l’inaction, et n’entrerez-vous pas, pour la posséder, dans la terre que le Seigneur Dieu de vos pères vous a donnée?
4 Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
Choisissez de chaque tribu trois hommes, afin que je les envoie, et qu’ils aillent, et parcourent cette terre; qu’ensuite ils la décrivent, selon le nombre de chaque multitude, et qu’ils me rapportent ce qu’ils auront décrit.
5 Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
Divisez entre vous la terre en sept parties: que Juda soit dans ses limites du côté austral, et Joseph du côté de l’aquilon.
6 Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
Décrivez la terre qui est au milieu d’eux en sept parts; ensuite vous viendrez ici vers moi, afin que, devant le Seigneur votre Dieu, je jette pour vous ici le sort,
7 Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
Parce qu’il n’y a point de part parmi vous pour les Lévites, mais que le sacerdoce du Seigneur est leur héritage. Quant à Gad, à Ruben et à la demi-tribu de Manassé, déjà elles avaient reçu au-delà du Jourdain, au côté oriental, leurs possessions, que leur donna Moïse, serviteur du Seigneur.
8 Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
Lorsque ces hommes se furent levés pour aller décrire la terre, Josué leur ordonna, disant: Parcourez la terre, décrivez-la, et revenez vers moi, afin qu’ici, devant le Seigneur, à Silo, je jette pour vous le sort.
9 Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
C’est pourquoi ils allèrent; et parcourant la terre avec soin, ils la divisèrent en sept parts, écrivant dans un livre; puis ils revinrent au camp, à Silo, vers Josué.
10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
Qui jeta les sorts devant le Seigneur, à Silo, et divisa la terre aux enfants d’Israël en sept parts.
11 Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
Or, le premier sort tomba sur les enfants de Benjamin, selon leurs familles, pour qu’ils possédassent la terre située entre les enfants de Juda et les enfants de Joseph.
12 Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
Et leur frontière fut vers l’aquilon à partir du Jourdain; s’avançant près du côté septentrional de Jéricho, et de là montant contre l’occident vers les montagnes, et parvenant jusqu’au désert de Bethaven;
13 Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
Puis, passant vers le midi près de Luza, qui est la même que Béthel, elle descend à Ataroth-Addar vers la montagne qui est au midi de Beth-horon la basse;
14 Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
Et s’abaisse en tournant contre la mer, au midi de la montagne qui regarde Beth-horon contre l’Africus; enfin elle se termine à Cariath-Baal, qui est appelée aussi à Cariathiarim, ville des enfants de Juda: telle est son étendue contre la mer, à l’occident.
15 Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
Mais du côté du midi, sa frontière s’avance de Cariathiarim contre la mer et parvient jusqu’à la source des eaux de Nephtoa.
16 Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
Et elle descend vers la partie de la montagne qui regarde la vallée des enfants d’Ennom, et qui est contre le côté septentrional, à l’extrémité de la vallée des Raphaïm. Elle descend aussi à Géennom (c’est-à-dire la vallée d’Ennom), à côté du Jébuséen, au midi, et elle parvient à la fontaine de Rogel,
17 Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
Passant devant l’aquilon, et allant à Ensemès, c’est-à-dire. Fontaine du soleil,
18 Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
Elle passe jusqu’aux tertres, qui sont vis-à-vis de la montée d’Adommim; elle descend à Abenboen, c’est-à-dire la pierre de Boen, fils de Ruben; elle passe du côté de l’aquilon jusqu’aux campagnes, et descend dans la plaine;
19 Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
Elle s’avance vers l’aquilon au-delà de Beth-hagla, et elle se termine à la langue de la mer très salée du côté de l’aquilon, au bout du Jourdain, vers le côté austral,
20 Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
Qui la termine du côté de l’orient: telle est la possession des enfants de Benjamin, selon leurs frontières d’alentour et leurs familles.
21 Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
Ses villes étaient: Jéricho, Beth-hagla, la vallée de Casis,
22 Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
Beth-Araba, Samaraïm, Béthel,
23 Avimu, Para, Ofra,
Avim, Aphara, Ophéra,
24 Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Le village d’Emona, Ophni et Gabée: douze villes et leurs villages;
25 Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
Gabaon, Rama, Béroth,
26 Mizpe, Kefira, Moza,
Mesphé, Caphara, Amosa,
27 Rekemu, Iripeeli, Tarala,
Récem, Jaréphel, Taréla,
28 Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.
Sala, Elaph, Jébus, qui est Jérusalem, Gabaath et Cariath: quatorze villes et leurs villages. Telle est la possession des enfants de Benjamin, selon leurs familles.

< Yoshua 18 >