< Yoshua 18 >
1 Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
and to gather all congregation son: descendant/people Israel Shiloh and to dwell there [obj] tent meeting and [the] land: country/planet to subdue to/for face: before their
2 Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
and to remain in/on/with son: descendant/people Israel which not to divide [obj] inheritance their seven tribe
3 Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
and to say Joshua to(wards) son: descendant/people Israel till where? you(m. p.) to slacken to/for to come (in): come to/for to possess: take [obj] [the] land: country/planet which to give: give to/for you LORD God father your
4 Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
to give to/for you three human to/for tribe and to send: depart them and to arise: establish and to go: walk in/on/with land: country/planet and to write [obj] her to/for lip: according inheritance their and to come (in): come to(wards) me
5 Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
and to divide [obj] her to/for seven portion Judah to stand: stand upon border: area his from south and house: household Joseph to stand: stand upon border: area their from north
6 Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
and you(m. p.) to write [obj] [the] land: country/planet seven portion and to come (in): bring to(wards) me here/thus and to shoot to/for you allotted here to/for face: before LORD God our
7 Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
for nothing portion to/for Levi in/on/with entrails: among your for priesthood LORD inheritance his and Gad and Reuben and half tribe [the] Manasseh to take: recieve inheritance their from side: beyond to/for Jordan east [to] which to give: give to/for them Moses servant/slave LORD
8 Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
and to arise: rise [the] human and to go: went and to command Joshua [obj] [the] to go: went to/for to write [obj] [the] land: country/planet to/for to say to go: went and to go: walk in/on/with land: country/planet and to write [obj] her and to return: return to(wards) me and here to throw to/for you allotted to/for face: before LORD in/on/with Shiloh
9 Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
and to go: went [the] human and to pass in/on/with land: country/planet and to write her to/for city to/for seven portion upon scroll: book and to come (in): come to(wards) Joshua to(wards) [the] camp Shiloh
10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
and to throw to/for them Joshua allotted in/on/with Shiloh to/for face: before LORD and to divide there Joshua [obj] [the] land: country/planet to/for son: descendant/people Israel like/as division their
11 Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
and to ascend: rise allotted tribe son: descendant/people Benjamin to/for family their and to come out: casting(lot) border: area allotted their between son: descendant/people Judah and between son: descendant/people Joseph
12 Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
and to be to/for them [the] border: boundary to/for side north [to] from [the] Jordan and to ascend: rise [the] border: boundary to(wards) shoulder Jericho from north and to ascend: rise in/on/with mountain: hill country sea: west [to] (and to be *Q(K)*) outgoing his wilderness [to] Beth-aven Beth-aven
13 Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
and to pass from there [the] border: boundary Luz [to] to(wards) shoulder Luz [to] south [to] he/she/it Bethel Bethel and to go down [the] border: boundary Ataroth-addar Ataroth-addar upon [the] mountain: mount which from south to/for (Lower) Beth-horon (Lower) Beth-horon Lower (Beth Horon)
14 Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
and to border [the] border: boundary and to turn: turn to/for side sea: west south [to] from [the] mountain: mount which upon face: surface Beth-horon Beth-horon south [to] (and to be *Q(K)*) outgoing his to(wards) Kiriath-baal Kiriath-baal he/she/it Kiriath-jearim Kiriath-jearim city son: descendant/people Judah this side sea: west
15 Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
and side south [to] from end Kiriath-jearim Kiriath-jearim and to come out: extends [the] border: boundary sea: west [to] and to come out: extends to(wards) spring water Nephtoah
16 Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
and to go down [the] border: boundary to(wards) end [the] mountain: mount which upon face: surface Valley son: child (Topheth of son of) Hinnom which in/on/with Valley (of Rephaim) (Valley of) Rephaim north [to] and to go down Valley (Topheth of) Hinnom to(wards) shoulder [the] Jebusite south [to] and to go down En-rogel En-rogel
17 Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
and to border from north and to come out: extends En-shemesh En-shemesh and to come out: extends to(wards) Geliloth which before ascent Adummim and to go down stone Bohan son: child Reuben
18 Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
and to pass to(wards) shoulder opposite [the] (Beth)-arabah north [to] and to go down [the] (Beth)-arabah [to]
19 Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
and to pass [the] border: boundary to(wards) shoulder Beth-hoglah Beth-hoglah north [to] (and to be outgoing *Q(K)*) [the] border: boundary to(wards) tongue: bar sea [the] Salt (Sea) north [to] to(wards) end [the] Jordan south [to] this border: boundary south
20 Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
and [the] Jordan to border [obj] him to/for side east [to] this inheritance son: descendant/people Benjamin to/for border her around to/for family their
21 Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
and to be [the] city to/for tribe son: descendant/people Benjamin to/for family their Jericho and Beth-hoglah Beth-hoglah and Emek (Emek)-keziz
22 Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
and Beth-arabah [the] Beth-arabah and (Mount) Zemaraim and Bethel Bethel
and [the] Avvim and [the] Parah and Ophrah
24 Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
and Chephar ([the] (Chephar)-ammoni *Q(K)*) and [the] Ophni and Geba city two ten and village their
25 Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
Gibeon and [the] Ramah and Beeroth
and [the] Mizpeh and [the] Chephirah and [the] Mozah
27 Rekemu, Iripeeli, Tarala,
and Rekem and Irpeel and Taralah
28 Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.
and Zela Haeleph and [the] Jebus he/she/it Jerusalem Gibeah Kiriath-jearim city four ten and village their this inheritance son: descendant/people Benjamin to/for family their