< Yoshua 18 >

1 Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
And all the congregation of the sons of Israel is assembled [at] Shiloh, and they cause the Tent of Meeting to dwell there, and the land has been subdued before them.
2 Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
And there are seven tribes left among the sons of Israel who have not shared their inheritance,
3 Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
and Joshua says to the sons of Israel, “Until when are you remiss to go in to possess the land which He, YHWH, God of your fathers, has given to you?
4 Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
Give three men from you for [each] tribe, and I send them, and they rise and go up and down through the land, and describe it according to their inheritance, and come to me,
5 Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
and they have divided it into seven portions—Judah stays by its border on the south, and the house of Joseph stays by their border on the north—
6 Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
and you describe the land [in] seven portions, and have brought [it] to me here, and I have cast a lot for you here before our God YHWH;
7 Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
for there is no portion for the Levites in your midst, for the priesthood of YHWH [is] their inheritance, and Gad, and Reuben, and half of the tribe of Manasseh received their inheritance beyond the Jordan eastward, which Moses, servant of YHWH, gave to them.”
8 Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
And the men rise and go; and Joshua commands those who are going to describe the land, saying, “Go, and walk up and down through the land, and describe it, and return to me, and here I cast a lot for you before YHWH in Shiloh.”
9 Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
And the men go, and pass over through the land, and describe it by cities, in seven portions, on a scroll, and they come to Joshua, to the camp [at] Shiloh.
10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
And Joshua casts a lot for them in Shiloh before YHWH, and there Joshua apportions the land to the sons of Israel, according to their divisions.
11 Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
And a lot goes up [for] the tribe of the sons of Benjamin, for their families; and the border of their lot goes out between the sons of Judah and the sons of Joseph.
12 Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
And the border is for them at the north side from the Jordan, and the border has gone up to the side of Jericho on the north, and gone up through the hill-country westward, and its outgoings have been at the wilderness of Beth-Aven;
13 Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
and the border has gone over there to Luz, to the side of Luz (it [is] Beth-El) southward, and the border has gone down [to] Atroth-Addar, by the hill that [is] on the south of the lower Beth-Horon;
14 Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
and the border has been marked out, and has gone around to the corner of the sea southward, from the hill which [is] at the front of Beth-Horon southward, and its outgoings have been to Kirjath-Ba‘al (it [is] Kirjath-Jearim), a city of the sons of Judah: this [is] the west quarter.
15 Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
And the south quarter [is] from the end of Kirjath-Jearim, and the border has gone out westward, and has gone out to the fountain of the waters of Nephtoah;
16 Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
and the border has come down to the extremity of the hill which [is] on the front of the Valley of the Son of Hinnom, which [is] in the Valley of the Rephaim northward, and has gone down the Valley of Hinnom to the side of Jebusi southward, and gone down [to] En-Rogel,
17 Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
and has been marked out on the north, and gone out to En-Shemesh, and gone out to Geliloth, which [is] opposite the ascent of Adummim, and gone down [to] the stone of Bohan son of Reuben,
18 Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
and passed over to the side in front of the Arabah northward, and gone down to Arabah;
19 Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
and the border has passed over to the side of Beth-Hoglah northward, and the outgoings of the border have been to the north bay of the Salt Sea, to the south extremity of the Jordan; this [is] the south border;
20 Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
and the Jordan borders it at the east quarter; this [is] the inheritance of the sons of Benjamin, by its borders all around, for their families.
21 Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
And the cities for the tribe of the sons of Benjamin, for their families, have been Jericho, and Beth-Hoglah, and the Valley of Keziz,
22 Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
and Beth-Arabah, Zemaraim, and Beth-El,
23 Avimu, Para, Ofra,
and Avim, and Parah, and Ophrah,
24 Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
and Chephar-Haammonai, and Ophni, and Gaba; twelve cities and their villages.
25 Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
Gibeon, and Ramah, and Beeroth,
26 Mizpe, Kefira, Moza,
and Mizpeh, and Chephirah, and Mozah,
27 Rekemu, Iripeeli, Tarala,
and Rekem, and Irpeel, and Taralah,
28 Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.
and Zelah, Eleph, and Jebusi (it [is] Jerusalem), Gibeath, Kirjath; fourteen cities and their villages. This [is] the inheritance of the sons of Benjamin, for their families.

< Yoshua 18 >